Yahusu: Utapeli unaofanywa na Kampuni ya Kimchina iliyopo Salasala, Dar es salaam

Yahusu: Utapeli unaofanywa na Kampuni ya Kimchina iliyopo Salasala, Dar es salaam

ww kweli boya yaani utoe 200,000 kuagiza simu china na bado eti ukatoa 98,000 kwa ajili ya usafiri toka china..kwanza simu gani gharama ya kuisafirisha inafika 98,000 kwa simu ya laki mbili tu..sasa itakuwa vp kwa wale wanaoagiza simu za milion 1 hadi 2 wanachajiwa gharama gani za usafiri..ebu tuambie ni simu aina gani uliagiza huko china ambayo kwa laki 3 uliyotoa ungeikosa hapa bongo.

Kuna vitu ukisafirisha huchajiwi kwa value yake.Price ya usafiri ni constant.Smartphone husafirishwa kwa dola 20-23$/pc,iwe ni ya laki moja au milioni tatu.Ingawa hapo bei alipigwa 98,000 tsh kwa usafiri pekee.

Wafanyabiashara wengi wanatumia kutokujua kwa wateja wao kuwapiga.
 
Habari ya leo wana JamiiForums wenzangu na waTanzania wenzangu,

Napenda kuwaletea habari hii inayuhusu kampuni moja inayoitwa Agiza Kimchina ambayo ipo maeneo ya Salasala katika jengo la Kimchina Dar es Salaam, Mke wangu aliagiza simu kutoka china kupitia kampuni hiyo toka mwaka jana mwezi wa sita na mpaka mwaka huu simu hazijafika, mke wangu alitake trouble ya kufuatilia baada ya kufika ofisini kwao wakamuambia kuwa simu zilikuja lakini zikawa mbovu so zikarudishwa China

Wakamuahidi baada ya mwezi watampigia cha kushangaza ukiwapigia simu hawapokei na hawana ushirikiano wowote

Naomba kutoa angalizo kwa waTanzania wenzangu hawa watu ni matapeli na maamuzi nilichukua ni kwenda ofisini kwao na Polisi, kwa sasa naelekea kituo cha Polisi kwa ajiri ya kuchukua RB na kufanya utaratibu wa kwenda ofisini kwao ili nipate kurudishiwa pesa zangu ambayo ilikuwa 200,000/= ya simu pamoja na 98,000/= ya usafiri.

Naomba mnisaidie kusambaza hii taarifa.
Hiyo ni kesi ya madai broda.
Polisi wanaingiaje hapo wakati mna mkataba
 
Polisi hawajakukula kidogo? Namaanisha hujawapa hata kaalfu hamsini ka maji?
 
Pole kwa yaliokukuta tunashukuru andiko lako linaweza saidia wengine wanaotarajia kuagiziwa na watu ama taasisi zisizo rasmi.
 
Kimchina ni tapeli aliyekubuhu toka sikunyingi watu wamempost instergram Kila siku lakin watu hawasikii bado wanaenda kuagiza acha mtapeliwe tu
 
Kakimbia goba kahamia salasala bado mmemfata hukohuko,aki wabongo mnapenda mtelezo s24 ultra za kichina zimewacost pole
 
Kimchina ni tapeli aliyekubuhu toka sikunyingi watu wamempost instergram Kila siku lakin watu hawasikii bado wanaenda kuagiza acha mtapeliwe tu
Simu za laki mbili zipo kibao, Ila hadi waagize China hahahaa ushamba mzigo! Alafu sijui mchawi yule, mbona kalalamikiwa muda sana?
 
Simu za laki mbili zipo kibao, Ila hadi waagize China hahahaa ushamba mzigo! Alafu sijui mchawi yule, mbona kalalamikiwa muda sana?
Watu wanapenda vya dezo ndo vinawaumiza nakuwatokea puan
 
wakati wa kuagiza simu mlipiga kimya mkijiona ninyi wajanja first baada ya kuangukia pua mnakuja kujiliza kwetu, kumbuka mchuma janga hula na wa kwao.
 
Habari ya leo wana JamiiForums wenzangu na waTanzania wenzangu,

Napenda kuwaletea habari hii inayuhusu kampuni moja inayoitwa Agiza Kimchina ambayo ipo maeneo ya Salasala katika jengo la Kimchina Dar es Salaam, Mke wangu aliagiza simu kutoka china kupitia kampuni hiyo toka mwaka jana mwezi wa sita na mpaka mwaka huu simu hazijafika, mke wangu alitake trouble ya kufuatilia baada ya kufika ofisini kwao wakamuambia kuwa simu zilikuja lakini zikawa mbovu so zikarudishwa China

Wakamuahidi baada ya mwezi watampigia cha kushangaza ukiwapigia simu hawapokei na hawana ushirikiano wowote

Naomba kutoa angalizo kwa waTanzania wenzangu hawa watu ni matapeli na maamuzi nilichukua ni kwenda ofisini kwao na Polisi, kwa sasa naelekea kituo cha Polisi kwa ajiri ya kuchukua RB na kufanya utaratibu wa kwenda ofisini kwao ili nipate kurudishiwa pesa zangu ambayo ilikuwa 200,000/= ya simu pamoja na 98,000/= ya usafiri.

Naomba mnisaidie kusambaza hii taarifa.
Laki mbili au milioni mbili?
 
Bila shaka ulinunua iPhone 15 high copy hizo simu ni mbovu balaaa na huyo kim China anatajirika kwa hiyo hela ya usafiri. Wenzie usafiri ni 30k kwa simu moja lakini yeye usafiri ni 98k na bado kuna nyumbu wanaenda huko kwa kuwa tu anatangaza vizuri. Huyu demu wala hatakatishi hela kama wengi wanavyosema yeye anapiga kwenye usafiri tu ndio tobo lake lilipo.

Kwa mfano flana za mtumba unaagiza kwa 500 ila usafiri kwa flana mona ni 2300 hapo ukiwa na flana 500 ambazo ni wastani wa balo moja na nusu usafiri unakuwa 460k. Imagine yeye anapata ngapi hilo balo kwa meli ni hata nusu cbm halifiki lakin yeye kashakata chake 460k. Utakuwa watu kama 10 hivi mnachangia cbm 1 yeye ndio kula yake wazee hakuna biashara ya hasara.

Mimi nimemstukia siagizi tena kwake kutoka usafiri wake uko juu sana

Narudia huyu binti hadangi wala hatapeli mtu mnamsingizia tu

Alafu brother huyo mkeo huenda pia alichelewa kulipa transport mana kwa sheria zake ni kuwa ukichelewa kulipa transport hana refund.

Piga kazi kimchina

Wajinga ndio waliwao.
 
Kimchina bila kutaperi watu asingetoboa. Tena anataperi sana watu wa mikoani wasioweza kuja dsm. Mpaka anafungua jengo lile. Muacheni alete vitu bongo mnunue hapo.
 
ww kweli boya yaani utoe 200,000 kuagiza simu china na bado eti ukatoa 98,000 kwa ajili ya usafiri toka china..kwanza simu gani gharama ya kuisafirisha inafika 98,000 kwa simu ya laki mbili tu..sasa itakuwa vp kwa wale wanaoagiza simu za milion 1 hadi 2 wanachajiwa gharama gani za usafiri..ebu tuambie ni simu aina gani uliagiza huko china ambayo kwa laki 3 uliyotoa ungeikosa hapa bongo.
Tecno canon 30 pro bongo 700. Kule 200 plus plus 50k
 
Manina ha ha haa

Ndege wanao fanana huruka pamoja we na mkeo ni Viazi wote ,salamu za pole ziende .kwa watoto wenu
Watoto wao ndio mtaji wa CCM wa miaka ijayo, maana akili hizo za wazazi, basi watoto lazima wawe "CCM" mara elfu.

CCM sasa walivyo.
 

Attachments

  • downloadfile-18.jpg
    downloadfile-18.jpg
    216.9 KB · Views: 1
Ni stahiki yako kuibiwa. Maduka ya simu yaliyojaa nchi hii, ulikuwa na haja gani ya kuagizia toka China kwa mtu ambae hata humjui mbali ya kumuona Instagram.

Mimi nipo Korea, nitumie laki moja tu, nakuletea Samsung S25 Ultra, 1TB Storage. Tena wala hulipii usafiri.
Unataka umnyooshe sio 😀
 
ww kweli boya yaani utoe 200,000 kuagiza simu china na bado eti ukatoa 98,000 kwa ajili ya usafiri toka china..kwanza simu gani gharama ya kuisafirisha inafika 98,000 kwa simu ya laki mbili tu..sasa itakuwa vp kwa wale wanaoagiza simu za milion 1 hadi 2 wanachajiwa gharama gani za usafiri..ebu tuambie ni simu aina gani uliagiza huko china ambayo kwa laki 3 uliyotoa ungeikosa hapa bongo.
Mnatucheka Wasukuma ushamba, sasa huyu tunamsemaje? Naamini angekuwa Msukuma leo mngetuua! Naomba asije akasema yeye kweli ni Msukuma!😁😁
 
Back
Top Bottom