Yajue baadhi ya mambo ya Upagani yaliyoingizwa na kufuatawa katika Ukristo.

Yajue baadhi ya mambo ya Upagani yaliyoingizwa na kufuatawa katika Ukristo.

Yaani watu wengi wapo shallow hata kujua TU Ukristo umeanzia Africa na kuenea huko kwengine na kurudi(ikiwa kwenye maandiko).
 
Dini imenifanya niwe mpumbavu sana. Yani Mimi wa kupiga Magotti na kulia mbele ya Dangote Cement iliyopakwa rangi..

Huu ugonjwa utuachie.
Naumiaa sana kila nikikumbuka.
Kutubu dhambi kwa Jamaa kafichama kwa Kibanda.

mshamba_hachekwi
Kuna video naotafuta nikiipata utalia machozi na kuona Bora wewe , Kuna watu wanagalagala mbele ya sanamu wakilia na kulilamba kama wehu vile.
 
Mbona kumjua huyo Kristo kupo complex sana mara Mungu , mara mwana wa Mungu mara mpk upitiwe na roho mitakatifu ndio ulewe vizuri ...yaani basi mambo hayaeleweki.

Nikifanya research fupi kwa Wateja wangu na rafiki zangu kuhusu Imani ya Yesu , mmoja nikamuuliza je Yesu ndiye Mungu aliyekuumba ? akakataa akasema yeye ana amini ni mwana wa Mungu, mwengine Yeye akashikilia kuwa ni Mungu ....yaani watu wanapingana kila mtu na lake
Mungu ni mmoja na YESU kristo ndio jina lake.
 
Dini hizi Balaa sana niishie kusema ivyoo tu, Ila mm kama mwafrika Din yangu ya kwanza ni "Africanism" hizo nyingine ni saporting tuu japo hatuna Manyuscript au gaidence of the way of livingi ila najua Hao whites (EUROPEANS & ARABS)walifanya juhudi kubwa kuficha dini ya mwafrika Rejea kitabu cha ENOCK kwann hawakukiingiza kwenye Biblia
Najaribu kuwaza tuu ila jibu sipati
 
Mungu ni mmoja na YESU kristo ndio jina lake.
Haya ni maoni ya Mkiristo mwenzenu Jf , suala la Yesu kuwa Mungu na utatu ni jambo tata sana .

IMG_20221004_163506.jpg
 
Taja dhehebu la kikristo ambalo halikutokanaachoitwa na Roman Catholic ?

Weka historia yake lilianzia wapi?
Jacobians, st Thomas christians in India.
Tatizo iliporasimishwa kuwa dini ya serikali na wakina mfalme constantine ilikuwa ni uhaini kuonekana mtu anakitu chochote kinachoitwa ukristo nje ya dini ya kaisali. Walipotezwa na wengine wakawa undercover wakaibuka baada ya hilo vuguvugu kufa. Hiyo ndio nguvu ya kuhoji uwepo wa dhehebu lingine inakopatikania.
 
Mbona kumjua huyo Kristo kupo complex sana mara Mungu , mara mwana wa Mungu mara mpk upitiwe na roho mitakatifu ndio ulewe vizuri ...yaani basi mambo hayaeleweki.

Nikifanya research fupi kwa Wateja wangu na rafiki zangu kuhusu Imani ya Yesu , mmoja nikamuuliza je Yesu ndiye Mungu aliyekuumba ? akakataa akasema yeye ana amini ni mwana wa Mungu, mwengine Yeye akashikilia kuwa ni Mungu ....yaani watu wanapingana kila mtu na lake
Akili ipo limited..

Yesu ni Mungu
Jina la Mungu ni Yesu, neno Mungu linabeba sifa.

akili inakataa kwasababu inawezekanaje Mungu awe mwanadamu? Na hapo unaona limitation ya akili. Uumbaji wake Mungu na matendo yake na maamuzi yake yapo beyond na fikra zetu zote.

Lakini ndio ukweli aliiba ubinadamu ili kuukomboa ulimwengu na kutu lipia deni letu la dhambi.
 
Kaka, una uelewa mdogo sana wa mambo ya Mungu but una elimu kubwa sana ya mambo ya DINI.
Kwamba pasaka ni sherehe za kipagani? Kwamba mavazi ya kikuhani na yenyewe ni upagani? Mnasomaga Biblia gani nyie?
 
Akili ipo limited..

Yesu ni Mungu
Jina la Mungu ni Yesu, neno Mungu linabeba sifa.

akili inakataa kwasababu inawezekanaje Mungu awe mwanadamu? Na hapo unaona limitation ya akili. Uumbaji wake Mungu na matendo yake na maamuzi yake yapo beyond na fikra zetu zote.

Lakini ndio ukweli aliiba ubinadamu ili kuukomboa ulimwengu na kutu lipia deni letu la dhambi.
Kwa hiyo sasa hatuna dhambi ? kaa ufikiri kwa makini suala la kuamini Uungu wa Yesu ni Imani potofu ya kiwango Cha juu kabisa.
 
Mara zote nikisikia mambo kama haya,najiuliza mbona hili Kanisa lina nguvu mahali pote duniani kama kama liko tofauti na Biblia? Maana Mungu tunayemuamini hawezi ruhusu Kanisa hili kutawala Ulimwengu wote ikiwa halifuati maagizo yake. Mfano kidogo tu ni siku ya jumapili ambayo Dunia nzima huwa mapumziko. Je ni Kanisa gani limeiweka hii siku na ikawa Ulimwenguni pote? Kanisa ni Moja Katoliki la Kitume,huko kwingine ni usumbufu.
 
Kwa hiyo sasa hatuna dhambi ? kaa ufikiri kwa makini suala la kuamini Uungu wa Yesu ni Imani potofu ya kiwango Cha juu kabisa.
Pole mkuu.. Tatizo la dhambi limetatuliwa miaka 2000 iliyopitia.. Kilichopo sasa ni kumkubali huyo Yesu maana yeye peke yake ndio njia kweli na uzima.. Ili uweze kuishi pasipo kutawaliwa na tamaa za mwili lazima ukubali huyo kama Bwana na Mwokozi wako.. Uta mkataa sasa hivi lakini huwezi kukwepa..
 
Bila kupoteza muda...

Hapa kuna baadhi ya mafundisho ya kipagani ambayo yamekuwa yakihusishwa na Ukristo kutokana na mchanganyiko wa tamaduni za kipagani na imani za Kikristo kupitia historia. Mafundisho haya mara nyingi yamechukuliwa kutoka katika dini za kipagani na kuingizwa katika taratibu au desturi za Kikristo:

1. Kusheherekea Krismasi Desemba 25

Tarehe hii ilichaguliwa ili kufanana na sherehe za kipagani kama Saturnalia na Sol Invictus, zilizoadhimisha kuzaliwa kwa jua lisiloshindwa. Hakuna ushahidi wa kibiblia kwamba Yesu alizaliwa tarehe hii.


2. Ibada ya sanamu na picha

Tamaduni za kipagani zilihusisha matumizi ya sanamu na picha katika ibada. Katika baadhi ya madhehebu ya Kikristo, sanamu za watakatifu, Maria, na Yesu hutumiwa kama sehemu ya ibada, jambo ambalo linapingwa na amri ya pili katika Biblia (Kutoka 20:4-5).


3. Maombi kwa wafu (Watakatifu na Bikira Maria)

Katika dini nyingi za kipagani, watu waliomba msaada kutoka kwa roho za wafu au miungu mbalimbali. Hili limeonekana pia katika baadhi ya desturi za Kikristo ambapo watu huomba msaada wa watakatifu au Bikira Maria badala ya kumwomba Mungu moja kwa moja.


4. Siku ya Jumapili kama siku ya ibada

Ibada ya jua ilikuwa maarufu katika tamaduni za kipagani. Badala ya Sabato ya Jumamosi kama ilivyoagizwa katika Biblia, Jumapili ilikubalika kama siku ya ibada kutokana na ushawishi wa ibada ya jua ya kipagani.


5. Utatu wa Miungu

Ingawa fundisho la Utatu (Mungu Baba, Mungu Mwana, na Mungu Roho Mtakatifu) lina misingi katika Ukristo, baadhi ya wakosoaji wanasema linafanana na dhana za kipagani kama vile Utatu wa miungu katika dini za Wamisri (Osiris, Isis, na Horus) au dini za Kihindi.


6. Sherehe ya Pasaka (Easter)

Neno "Easter" linahusishwa na mungu wa kike wa kipagani aitwaye Ēostre, ambaye alihusishwa na majira ya kuchipua na uzazi. Desturi kama za mayai ya Pasaka na sungura zilitoka katika tamaduni za kipagani.


7. Kuzimu kama mahali pa mateso ya milele

Wazo la kuzimu lilihusiana sana na mafundisho ya Kipagani kama katika hadithi za Kigiriki za Hades. Katika Biblia, "kuzimu" mara nyingi hurejelea kaburi au mahali pa wafu, lakini dhana ya mahali pa moto wa milele ilisambazwa kupitia ushawishi wa kipagani.


8. Sherehe za watakatifu na maadhimisho ya miungu

Katika tamaduni za kipagani, kulikuwa na maadhimisho ya miungu mbalimbali kwa nyakati tofauti. Ukristo ulipitisha desturi kama zile za kuadhimisha watakatifu katika siku maalum, mfano All Saints’ Day (Siku ya Watakatifu Wote).


9. Maji ya Baraka

Matumizi ya maji ya baraka yanafanana na tamaduni za kipagani ambapo maji ya mito, chemchemi, au mialiko mingine ilihesabiwa kuwa takatifu.


10. Ibada za mishumaa na kadhi

Mishumaa na kadhi vilikuwa sehemu ya ibada za kipagani, hasa katika kuwakilisha nuru au roho za wafu. Desturi hii ilijumuishwa katika baadhi ya taratibu za Kikristo, hasa ibada za Kanisa Katoliki.


11. Kuvaa mavazi maalum ya kidini (kanzu, kofia, na mkufu wa makuhani)

Mavazi haya yanahusiana na tamaduni za kipagani, ambapo makuhani walivaa mavazi maalum ya kifahari kuonyesha mamlaka yao ya kiroho.


12. Kuadhimisha Siku ya Wapendanao (Valentine’s Day)

Siku hii ina mizizi ya kipagani, hasa sherehe za Warumi za Lupercalia, zilizohusiana na uzazi na mapenzi

Credit: hamis77

View attachment 3188747

Nakaribisha maoni tujadili kwa hoja na kistaarabu , Uzi Tayari.
Iyas au yaas inahusishwa na ushoga lakini hapa unaposti kwa kutumia Mtandao wa yaas.

Je wewe ni shoga?
 
Mnahangaika sana,ulizaliwa ukazikuta hizi taratibu utakufa utaziacha,fanya mambo yako
Kuzaliwa kuzikuta na kufa kuziacha, Haimaanishi kwamba ndio haziwezi kukosolewa. Au kwamba ndio zitadumu milele.

Zita endelea kukosolewa vizazi kwa vizazi hadi zitakuja kufutika.

A lie must surely perish.
 
11. Kuvaa mavazi maalum ya kidini (kanzu, kofia, na mkufu wa makuhani)
Yesu naye alivaa kanzu kumbe naye kaiga wapagani!

Walokole hubadilisha bar kuwa makanisa unasemaje hapo wamekosea?

Basi ni kazi ya Ukristo kubadilisha kila kilichokuwa cha kipagani kuwa cha Mungu Mwenyezi kwani vyote ni mali yake.
 
Back
Top Bottom