Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,897
- 6,925
Wauaume kuota maziwa kama wanawake
Wanawake kuota ndevu kama wanaume
Idara ya afya manispaa ya Sumbawanga imewaonya wakazi kujiepusha na matumizi ya vipodozi vilivyotengenezwa na viambatanishi vyenye sumu aina ya "Steroids." Vipodozi hivyo vimeshapigwa marufuku nchini na wenye kutumia wapo hatarini kupata athari zilizo kinyume na jinsia ya maumbile yao ikiwa ni pamoja na wanaume kuota matiti na wanawake kuota ndevu.
Hayo yalibainishwa na Mganga Mkuu wa Manispaa ya Sumbawanga Dr. Ali Musa Makori alipokuwa anasimamia zoezi la kuteketeza kwa moto tani moja ya vyakula na vipodozi vya thamani ya shilingi milioni nne na nusu. Alisisitiza wakati wanaponunua bidhaa kusoma maelezo, kuepuka kununua bidhaa ambazo muda wake umeisha na kuwa makini kutonunua bidhaa bandia.
Source: Habari Leo