Wonderful
JF-Expert Member
- Apr 8, 2015
- 7,347
- 5,986
Leo ni leo.
Wale jamaa wataalamu wa kupiga mtu kwa kufata tar huku wafungaji wao wakitupia kwa kufuata mwezi watakua taifa jioni ya leo kupambana na wagonga nyundo wa nyanda za juu kudini(MCC) Tuwe pamoja bila kukosa.
kuhusu viwanja vingine matakoe wekeni hapa pia. Mwenye ratiba ya viwanja vingine aiweke hapa pia!!!
=====================
UPDATES:
Mechi ilikuwa tamu dakika 45 za kwanza. Zimekamilika huku wenyeji Yanga wakiwa wanaongoza kwa mabao 2-1.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara imekuwa tamu kutokana na timu zote kucheza vizuri na kushambuliana kwa zamu.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Mliberia, Kpah Sherman na Salum Telela aliyepiga shuti kali baada ya kupokea pasi ya Haruna Niyonzima.
Bao la Mbeya City limefungwa na mkongwe Themi Felix aliyewatoka mabeki Nadir Haroub na Oscar Joshua kabla ya kufunga kiufundi kabisa
Timu zimekwenda mapumziko Yanga ikiwa inaongoza kwa mabao 2-1.
Dk 46, Yanga wanaanza mashambulizi kwa kasi wakionyesha wamepania kiuongeza bao.
Dk 47, Msuva anapiga shuti akiwa nje kidogo ya lango la Mbeya City, mpira unatoka.
GOOOOO Dk 49, Cannavaro anaunganisha krosi safi ya mpira wa faulo wa Niyonzima na kufunga kwa kichwa safi
Dk 52, kipa Mbeya City anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa faulo wa Niyonzima
Telela KADI NYEKUNDU Dk 53, Themi Felix anapigwa kadi nyekundu kwa kumchezea madhambi .
DK 56, Nonga napiga shuti kali, lakini Barthez anadaka kwa mbwembwe kabisa.
Dk 59, Peter Mapunda anaingia kuchukua nafasi ya Deus Kaseke upande wa City
Dk 60, anaingia Salum Telela kuchukua nafasi ya Salum Telela kwa Yanga
Dk 61&64, Yanga wanaonekana kutawala zaidi mpira huku wakifika langoni mwa City mara nne na City wanaonekana kujilinda zaidi.
Dk 69, krosi safi ya Joshua, MSuva anapiga kichwa cha kuparaza, kinagonga mwamba na kurejea uwanjani
Dk 78, Yanga wanaonekana kumiliki mpira zaidi huku Mbeya City wakiwa wanaathirika kutokana na kuwa pungufu.
Dk 83, Ngassa anaingia vizuri na kushindwa kufunga akiwa hatua chache
Dk 87, Mwagane Yeya anajaribu kuwatoka mabeki wa Yanga lakini Barthez anakuwa mwepesi kuwahi
Dk 89, Ngassa tena anaingia eneo la hatari lakini mabeki wanambana vizuri.
MPIRA UMEKWISHAAA...!!
Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva akiwatika Mabeki wa Timu ya Mbeya City wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara unaoendelea kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga inaongoza Bao 3 - 1. Picha na Othman Michuzi.
Kiungo Mchezeshaji wa timu ya Yanga, Haroun Niyonzima akiangalia kwa kupeleka mpira wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara unaoendelea kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga inaongoza Bao 3 - 1.
Kipa wa Timu ya Mbeya City, Hanington Kalyesubula akiangalia mpira wavuni huku washabiki wa Yanga wakishangilia ushindi.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakisangilia ushindi ushindi na washabiki wao.
Mashabiki wa yanga
Mashabiki wa Mbeya. Picha kwa hisani ya presstz
Full time:
Yanga 3 - 1 Mbeya City.
Matokeo ya Mechi za leo 2015-04-12
STAND UNITED 1 : 0 POLISI MORO
YANGA 3 : 1 MBEYA CITY
http://ww.jamiiforums.com/sports/834828-mwambusi-tunaweza-kufungwa-na-yanga-lakini-si-nane.html
Wale jamaa wataalamu wa kupiga mtu kwa kufata tar huku wafungaji wao wakitupia kwa kufuata mwezi watakua taifa jioni ya leo kupambana na wagonga nyundo wa nyanda za juu kudini(MCC) Tuwe pamoja bila kukosa.
kuhusu viwanja vingine matakoe wekeni hapa pia. Mwenye ratiba ya viwanja vingine aiweke hapa pia!!!
=====================
UPDATES:
Mechi ilikuwa tamu dakika 45 za kwanza. Zimekamilika huku wenyeji Yanga wakiwa wanaongoza kwa mabao 2-1.
Mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara imekuwa tamu kutokana na timu zote kucheza vizuri na kushambuliana kwa zamu.
Mabao ya Yanga yamefungwa na Mliberia, Kpah Sherman na Salum Telela aliyepiga shuti kali baada ya kupokea pasi ya Haruna Niyonzima.
Bao la Mbeya City limefungwa na mkongwe Themi Felix aliyewatoka mabeki Nadir Haroub na Oscar Joshua kabla ya kufunga kiufundi kabisa
Timu zimekwenda mapumziko Yanga ikiwa inaongoza kwa mabao 2-1.
Dk 46, Yanga wanaanza mashambulizi kwa kasi wakionyesha wamepania kiuongeza bao.
Dk 47, Msuva anapiga shuti akiwa nje kidogo ya lango la Mbeya City, mpira unatoka.
GOOOOO Dk 49, Cannavaro anaunganisha krosi safi ya mpira wa faulo wa Niyonzima na kufunga kwa kichwa safi
Dk 52, kipa Mbeya City anafanya kazi ya ziada kuokoa mpira wa faulo wa Niyonzima
Telela KADI NYEKUNDU Dk 53, Themi Felix anapigwa kadi nyekundu kwa kumchezea madhambi .
DK 56, Nonga napiga shuti kali, lakini Barthez anadaka kwa mbwembwe kabisa.
Dk 59, Peter Mapunda anaingia kuchukua nafasi ya Deus Kaseke upande wa City
Dk 60, anaingia Salum Telela kuchukua nafasi ya Salum Telela kwa Yanga
Dk 61&64, Yanga wanaonekana kutawala zaidi mpira huku wakifika langoni mwa City mara nne na City wanaonekana kujilinda zaidi.
Dk 69, krosi safi ya Joshua, MSuva anapiga kichwa cha kuparaza, kinagonga mwamba na kurejea uwanjani
Dk 78, Yanga wanaonekana kumiliki mpira zaidi huku Mbeya City wakiwa wanaathirika kutokana na kuwa pungufu.
Dk 83, Ngassa anaingia vizuri na kushindwa kufunga akiwa hatua chache
Dk 87, Mwagane Yeya anajaribu kuwatoka mabeki wa Yanga lakini Barthez anakuwa mwepesi kuwahi
Dk 89, Ngassa tena anaingia eneo la hatari lakini mabeki wanambana vizuri.
MPIRA UMEKWISHAAA...!!
Mshambuliaji wa Yanga, Simon Msuva akiwatika Mabeki wa Timu ya Mbeya City wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara unaoendelea kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga inaongoza Bao 3 - 1. Picha na Othman Michuzi.
Kiungo Mchezeshaji wa timu ya Yanga, Haroun Niyonzima akiangalia kwa kupeleka mpira wakati wa mchezo wa ligi kuu Tanzania Bara unaoendelea kwenye Uwanja wa Taifa hivi sasa.Yanga inaongoza Bao 3 - 1.
Kipa wa Timu ya Mbeya City, Hanington Kalyesubula akiangalia mpira wavuni huku washabiki wa Yanga wakishangilia ushindi.
Wachezaji wa timu ya Yanga wakisangilia ushindi ushindi na washabiki wao.
Mashabiki wa yanga
Mashabiki wa Mbeya. Picha kwa hisani ya presstz
Full time:
Yanga 3 - 1 Mbeya City.
Matokeo ya Mechi za leo 2015-04-12
STAND UNITED 1 : 0 POLISI MORO
YANGA 3 : 1 MBEYA CITY
http://ww.jamiiforums.com/sports/834828-mwambusi-tunaweza-kufungwa-na-yanga-lakini-si-nane.html