Yaliyo Mbele na Nyuma ya Simba SC -Last Part

Mk54

JF-Expert Member
Joined
Dec 29, 2016
Posts
1,996
Reaction score
3,950
Kwanza napenda kuuliza swali.

Je kuna Mtanzania yeyote aliyekuwa anaamini Simba SC itafuzu kwenye Michuano hii?

Kama yupo basi ni wale wasioupenda Uhalisia Wa Maisha. Yaani SSC iitoe Tout Puissant!!!

Kwa hesabu za uhalisia haiwezekani, ni ukichaa kuwaza hivyo

1. Kikosi cha Tout Puissant( Nguvu Kama Zote) kina gharimu zaidi ya Bil 20, wakati kikosi cha SSC kina gharimu chini ya Bil 2.5

2. Tout Puissant ina nyota Tano, SSC haina nyota hata moja.

3. Almost every year Tout Puissant anashiriki michuano hii, how long does it take SSC kushiriki michuano hii?


Kocha wa Tout Puissant alisema wazi siku ile pale Taifa, wao wamekuja kuifundisha SSC mpira, kwamba Simba ipo kwenye kujifunza pamoja na tuhuma za kuhonga wapija filimbi. Alisisitiza kwamba kiwango cha SSC bado ni kidogo na mwisho wao utakuwa ni Lumumbashi, alilisema hili kwa yakini kabisa.


Ukitembea Social Media za Timu kubwa zote ikiwemo Al ahly, hukuti mambo ya Inshallah, sijui Mungu tusaidie kwa sababu haya mambo hayana athari yoyote Kwenye uhalisia wa Soka.

Simba ni kikosi dhaifu sana mbele ya timu kama Tout Puissant, ni kikosi ambacho hakina Investment.

Kocha wa Yanga, Ndugu Mwinyi alisema kwa hakika SSC kuitoa Mazembe pale Congo ni Treblement De Terre, akiwa na maana Tetemeko la Ardhi. He was very Honesty, white and black.

Lakini Wanasimba wasioupenda ukweli mchungu walimshambulia na kuzidisha maneno kama Inshallah, Kwa jina La mwenyezi Mungu, Mwingi wa rehema sijui nini na nini ...

. Nani kasema haya mambo yanaleta athari Kwenye uhalisia? Ni Mambo ya ajabu ajabu sana badala yake mnasahau investment walizofanya watu ili wapate matokeo waliyopata leo.

Pamoja na yote kwa kiwango cha Simba imejitahidi kufika ilipofia, mwanzo wake ni mzuri na ni sehemu nzuri kwa kuanza safari ya Matumaini ikiwa ni pamoja na kupunguza Inshallah zote badala yake kufanya Investment na kuacha soka la mitandao linaloendeshwa na ndugu Haji Sunday Manara.


Muhammad Dewji ni wakati wake sasa wa kuunda kikosi chenye Tija ambacho kitakuwa na uwezo wa kuleta matokeo sehemu yoyote. Kikosi ambacho kitaundwa na wachezaji makini wa kimataifa huku wakishirikiana na wachezaji bora wa ndani.

Hakuna uchawi Kwenye mpira ni Investment tu . Waweke nidhamu kwa wachezaji kwa kuingia mikataba migumu ikiwa ni pamoja na kuwakata mishahara yao kama timu haifikii lengo.

Aidha, Kwenye usajili, SSC iachane na madadali wa kipuuzi, wafanye utafiti wa kutosha juu ya mchezaji wanaetaka kumchukua hasa wa kimataifa.


Mpira ni pesa, sio Inshallah na kelele za mitandaoni sijui eti kujaza uwanja, my foot!

Tumeona uwanja wa Tout Puisant unaingiza watu 18K tu na wameleta Tremblement de Terre.

————————

Jumamosi 13, Aprili 2019.
 
Wame invest kwenye social media zaidi.bado tuna safari ndefu sana kwakweli
 
Mleta Uzi naona hili neno "INSHAALLAH" Linakuumiza sana... Labda nikuambie tu kuwa jambo lolote lile hata kama utatumia ujuzi, ufundi au taaluma yoyote ile Bila kumuomba Allah ni kazi bure tu... Kumtanguliza Mungu kwenye kila ufanyalo kuna faida. Hushangai kwa nini hata wachezaji wakubwa tu Duniani huwa wanamuomba Mungu kabla au baada ya mechi? Uwe na uwezo au usiwe nao... ALLAH IS ABOVE EVERYTHING!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Fukuza kocha na professional wote uchwara.. Wamewaangusha sana. Mechi ya kufa na kupona mnapata kadi mbili tu za njano
 
Fukuza kocha na professional wote uchwara.. Wamewaangusha sana. Mechi ya kufa na kupona mnapata kadi mbili tu za njano
Yaani uungie kwenye tornament ya kufa na kupona halafu uogope scratches, unataka utoke bila scratches?
Hata ingekuwa ni ya kujafurahisha tu but yet, you are subjected to scratches.
 
Wewe ni boya kweli kweli kwa hiyo ulitaka Simba isipeleke timu uwanjani kisa TP ni timu kubwa?? Poor analysis with average or low IQ

Sent using Jamii Forums mobile app
 
hangaikeni na yanga yenu: simba tumeshapiga hatua tunajua tunaelekea wapi na tunatakiwa tufanye nini: stage ya kuchangisha michango tumeshaachana nayo sshivi, kuwa ndani ya timu nane bora katika afrika ni hatua kubwa sana. sasahivi tumewawezesha na nyie majirani hata kama hamtachukua ubingwa mataenda kushiriki klabu bingwa africa kwa mbeleko inayotokana na jitihada za simba
 

Umekariri sana.
 
Wewe ni boya kweli kweli kwa hiyo ulitaka Simba isipeleke timu uwanjani kisa TP ni timu kubwa?? Poor analysis with average or low IQ

Sent using Jamii Forums mobile app

Average or low ? Mbona huna stand. Tatizo lenu nyie mashabiki uchwara ndio hilo. Hampendi ukweli
 

Ni imani yako. Sikupingi. Above everything [emoji23][emoji23]. So hakutaka kuwasaidia hata droo?

Poor mind, above everything bila Investment ni uwendawazimu. Face the truth .
 
Soka letu linarudi nyuma kwa kupenda kudanganywa!! Sisi watanzania hatupendi kuambiwa ukweli na ndo maana viongozi wa klabu zetu wanatuletea machezaji ya ovyo wanayapamba kwenye media uongo mwingi hatimaye tunaishia kupigwa vipigo vya mbwa koko nakujifariji kwingi pasipo faida yoyote.
 
Kwa hatua simba iliyofikia inahitaji pongezi. Ziko timu zilizopata hio nafasi miaka minne mfulilizo lakini hazikuweza kususa ata nusu ya hapo. Badala yake ziliishia kujipa majina wakimataifa na kumpa kumpa tena n.k. so hebu tuipongeze simba na tuishauri kijiandaa kufika juu zaidi. Hata mkuyu ulianza kama mchicha. Tz imeziacha nchi zote za africa mashariki na kati kwa ubora kwwnye level ya vilabu. Tuache kuponda tusifu na kushukuru kwa hatua tuliyofikia. Unapompanda manara kwa style yake ya kujaza uwanja unakosea maana kila nchi inakuja na style yake but lengo ni moja. Mchezaji yoyote star anahitaji pia motisha ili aweze kufanya vzr na ndicho simba walichokifanya. Hata tukiwa na wachezaji wenye level ya Real madrid bado mashabiki wana nafasi yake.


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Average or low ? Mbona huna stand. Tatizo lenu nyie mashabiki uchwara ndio hilo. Hampendi ukweli
It can be both unakuja eti TP mazembe kikosi chao 20bilion while simba sijui 2.5 bilion hiyo siyo sababu Al Ahly kapigwa 5 nil kikosi chake cha bilion ngapi?? Woverhmpton kikosi chake cha Bei gani mbona kawapiga vigogo epl?? Analysis yako angetakiwa aongee barabarani mtu ambaye ni extremely idiot siyo kutuletea humu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mo aanze na viporo kwa hisani ya TFF.
 

Kwanza hatujaiponda Simba labda Kama hujaelewa vyema Ujumbe. Katika andiko tumeshauri pia nini Simba inapaswa kufanya kwa sasa, Manara aendelee na kelele zake lakini pia ukweli ujulikane kuwa mpira sio maneno mengi bali ni Investment. Ikiwa Timu itafanya investment na kuchukua wachezaji walio bora ndiyo tutahitaji motisha za kutosha.

Kuendelea kuaminisha watu kuwa eti tutaitoa Mazembe kwa nguvu za Mungu ni ukichaa kwa Sababu Mazembe imefanya Investment za kutosha na wao pia wanamuomba Mungu.
 

Trust me una uwezo mdogo wa kuelewa.

Nyie ndo wale Makapi wasioelewa alichosema Zahera, tremblement de terre.

Nikusaidie kuelewa,

Nimemaanisha hivi,

kiuhalisia kwanza mnatakiwa kufanya Investment ili kuwa na matokeo kwa asilimia kubwa, lakini haimaanishi kwamba hamtokuja kufungwa au kutolewa Kwenye michuano japo mme invest. Football ni mashindano na anything can happen.

Kuilinganisha Al ahly na Simba kwa Sababu zote zimetolewa ni uwendawazimu.

1. Inachukua muda gani simba kushiriki mashindano haya , nyie kushiriki mashindano haya ni sherehe kwa timu kama Al ahly kuvuka kwenye makundi ni kawaida sana, unajua kwa nini ?

3. Al ahly ina nyota 8 , ilikuwa kwenye mbio za kutafuta nyota ya tisa, Simba haina nyota hata moja, na ilikuwa inatafuta japo kushiriki nusu fainal tu inatosha, unajua ni kwanini ?

3. Al ahly imetolewa kimpira, kwamba pamoja na Investment, sometimes yes sometimes no , Simba haijatolewa kimpira, Simba imetolewa kwa Sababu hai deserve Kuendelea kuwepo, sio level zake. Simba ilikuwa ipo Kwenye kujifunza na sio Kwenye kusaka Kombe, that is naked truth, Gadem!

Simba inakikosi ambacho mchezaji anapata nafasi 5 za yeye na kipa, na hashindi hata moja, TP Mazembe au Al ahly haiwezi kumpanga mtu kama huyo, anatia hasara timu.

Ni mara ngapi Mchezaji kama Bocco anapata nafasi yeye na kipa zaidi ya tatu na hashindi hata moja, lakini ndo mchezaji pendwa, ndo ujue simba inahitaji Mapinduzi na sio unazi.

Kama siku ile Bocco angekuwa ni mchezaji makini mngeipiga Mazembe goli tatu bila na mngesonga mbele. Mmekazana na Mungu saidia, sijui nini na nini, Trust me mnapoteza muda.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…