Yaliyojiri bungeni Dodoma: Alhamisi tarehe 11 Septemba, 2014 - Kikao cha 38

Yaliyojiri bungeni Dodoma: Alhamisi tarehe 11 Septemba, 2014 - Kikao cha 38

Asante cheyo kumbe Jamaa mbele ya Raisi wanaufyata wakija barabarani wanabwekaaa
 
Leo huyu mzee kawananga UKAWA , kasema Kama vipi atamuomba mzee wa kaya aiweke video wazi kujua kilichozungumzwa kwenye kikao CHA TCD na mkuu wa kaya. Ameweka mambo openly baada ya jana ukawa kupindisha tone Yao. UKAWA wanania gani kwa msingi wa maelezo ya bwana mapesa Cheyo?
 
Eti kuna mambo mazuri bmk,unataja wavuvi na wakulima!ujinga mtupu,taja kuondoa ukomo wa ubunge,taja kuondoa kutowajibishwa wabunge na wananchi!
 
Waseng'e kweli,hapa 2namalizwa wananchi,si ukawa!
Kusingekuwa na security ningelichoma moto bunge na waliomo,nyambafu!
 
Bila shaka sote hatujambo ... Jamani mi naomba kupata maoni yaliyotolewa na mkongwe wa siasa nchini Mzee Kingunge kuhusu maendeleo ya uchumi wa nchi yetu. Mchango wake umenivutia sana ila sijaupata wote na wala sikutazama wakati anachangia bali nimeskia tu jinsi wajumbe wanavyom-quote. Pls kama kuna mtu ana full doc au link ya mchango wake naomba tafadhali.
 
Hawa itabidi wakitoka huko bungeni watafute kisiwa chao wakaishi huko,
la sivyo warudi na hela zetu mkononi.

Watanzania huu uwoga sijui tumeridhi toka wapi mijitu inakula hela ovyo, kujadili katiba isiyopatikana,na wakifika kwenye majimbo yao wataonekana wafalme wanalakiwa kama majemadari wamerudi toka vitani kumbe wahujumu uchumi wakubwa hao.
 
Kuna wamama wawili jana walichangia utumbo kabisa, nilijikuta mahali natizama tv ya watu,
tena ni watoto wa watu wenye majina makubwa, yaani hakuna kitu hakuna kitu, mbali ya kuuza
sura zao na kutuonyesha mabatiki waliovaa.

Watanzania huu uwoga sijui tumeridhi toka wapi mijitu inakula hela ovyo, kujadili katiba isiyopatikana,na wakifika kwenye majimbo yao wataonekana wafalme wanalakiwa kama majemadari wamerudi toka vitani kumbe wahujumu uchumi wakubwa hao.
 
Mheshimiwa Sita amesema kuwaitakapofika muda wa kuipigia kura katiba inayopendekezwa, wabunge wa BMK wasiokuwepo bungeni kwa ruhusa au ugonjwa watatakiwa wapige kura kwa njia ya simu. Sitaameweza kunukuu Kanuni ya Bunge inayosema, “Akidi” maana yakeni idadi ya wajumbe inayoruhusiwa kwa madhumuni ya kuanza kikao cha BungeMaalumu, Kamati au kufanya uamuzi wa Bunge Maalumu au wa Kamatiya Bunge Maalumu. Je mheshimiwaSita ametafsiri sawasawa hiyo kanuni?
Kwa uelewa wangu ni kuwaakidi inaweza patikana kabla ya kuanza kikao na kikao kikaanza kufanyika lakiniinaweza tokea wakati mnaendelea na kikao wajumbe ndani ya kikao wakapungua kwasababu yoyote ile na hivyo akidi ikapungua. Kwa upungufu huo wa akidi wajumbewaliopo hawatakuwa na uwezo wa kufanya maamuzi kwa njia ya kura. Kama tafsiriyangu ni sahihi wajumbe ambao hawapo ndani ya kikao hawahitajiki kutafutwa kwasimu ili wapige kura wakati hawakuwepo kwenye mjadala wa jambo au mamboyaliyokuwa yakijadiliwa hata kama waliwahi kushiriki hapo kabla kwanihawakuweza kushiriki mpaka mwisho ya jambo husika.
 
Hiki ni kioja. je ni nani atahakiki kura hizo ili kujiridhisha kuwa zimewekwa panapopasa ?!! na je kama kanuni ipo hiyo, hao watu wa nje wa nchi wanatumia kanuni ipi? Kwani Tanzania hakuna sheria ya uchaguzi inayoruhusu mtu kupiga kura akiwa nje ya nchi na hata nje ya kituo chake alichojiandikisha.
 
Hivi jamani hii nchi vijana tumeamua kuwaachia vijizee ambavyo vilipewa dhamana ya kutuongoza miaka hiyo vikashindwa ndio vituamulie mustakali wa nchi yetu miaka 50 ijayo just kwa ulafi wao wa madaraka?!!! haka kazee kanaitwa SITTA kalishafeli siku nyingi sana ila kwa sababu ya his stu..pid ambitions anataka kutuona watanzania milioni 50 ni wapuuzi kama yeye???!!! huyu mzee na vigagula wengine wote wanaoendelea kufuja pesa zetu huko bungeti inatakiwa wazalendo twende Ddodma tukawatoe huko bungeni kwa bakora......hawa ni sawa na panyabuku wenye njaa kali
 
Hivi nyie huko dodoma mnajuwa kuwa mnatukera sana?
Haki ya nani ngoja tuje huko na bakora tu ndo mtaelewa kuwa tumewachoka.
Mnakula pesa yetu for nothing.......... grrrrrrp!!!!!!!!!!
Hawajitambui, wasamehe bure.
 
Haya ndo matatizo ya kupiga picha na mwizi. Usipoangalia vizuri anaitumia picha hiyo kujisafisha. Tusubili hizo cd zenye sauti za viongozi hao.
 
Ni baada ya kupewa nafasi na Makamo Mwenyekiti Samiya Suluhu Hassan aweze kuchangia maoni yake kwa Kamati za Bunge Maalum na kuanza kumshukuru Rais JK na Mwenyekiti wa bunge na Makamu mwenyekiti wa bunge hilo kwa kutokutetereka kwao na maneno ya nje kuhusu uendeshaji wa bunge hilo.

Lakini pia mama huyu akapenda kueleza kile ambacho anasema kimesemwa na mtu mmoja ambaye akieleleza watu watamfahamu jina lake (maalim seif) aliposema katika chombo flani cha habari kwamba bunge maalum la katiba linawakilishwa na watanganyika pamoja na ccm wa unguja tu.

Mama huyu alishika karatasi na kutaja list ya majina ya wapemba ambao wamo ndani ya bunge maalum akiwamo moh'd aboud pia na yeye akijinadi kuwa ni mpemba wa wete kaskazini pemba.


Star TV Live:

My Take: Maalim seif alisema katika Bunge Maalum la Katiba kwa sasa hakuna mbunge yeyote na mwakilishi wa kuchaguliwa ambaye ni Mpemba kwa maana ya kwamba anaiwakilisha Pemba. Je huyu mama kweli alimfahamu makamu wa Kwanza wa Rais Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad?
 
Ilitokana na sababu za mfumo wa vyama vingi ambavyo vilileta mkanganyiko ufuatao:
1. Inaweza kutokea Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoka chama kimoja na Rais wa Zanzibar chama kingine
2.Ikitokea Rais wa Jamhuri ameugua , kufariki au kufukuzwa kazi, Rais wa Zanzibar ataongozaje nchi nzima wakati amechaguliwa na watu wa Zanzibar tu?

MH. Hatib amenukuu viongozi mbalimbali wa CUF akiwemo SEIF SHARIF HAMAD waliposema kuwa kuondolewa kwa Rais wa Zanzibar kuwa Makamu wa Rais wa Jamnhuri ni pigo kwa Zanzibar na kusema sasa nafasi hiyo imerudishwa na rasimu inayojadiliwa na Wapinzani watafute kisingizio kingine.
 
Ivi kuna mtu kweli anaweza kufungua TV kumsikiliza huyu mama? angekuwa na thamani angesimama kuitetea Zanzibar yake iliyomezwa ni Tanganyika miaka nenda miaka rudi, badala kujenga hoja anasema yeye anaunga mkono tu maoni ya wengi
 
Back
Top Bottom