Yaliyojiri Bungeni Dodoma: Jumatatu, Tarehe 10 Machi 2014

Hahahaaaaaaa jamani mbavu zangu mieeee. Mambo ya antisuzi yamefika na huku! Ee yangu macho.
Skype,Kuna watu wengine wanaboa,hata mtoto wa chekechea anawazidi upeo wa kuelewa!
 
Last edited by a moderator:
Kuna upuuzi gani unaendelea saa hizi huko? Wallah watatiana mimba tu trust me
 
M/kiti wa kamati ya marekebisho kanuni bunge la katiba Costa Mahalu leo Hili mambo yaende katoa marekebisho yanayotakiwa kuchukuliwa tahadhari; KIFUNGU; 37 MAAMUZI YOYOTE NDANI YA BUNGE LA KATIBA YATAFANYIKA KWA KUPIGA KURA; KIFUNGU 38; MWENYEKITI WA KUDUMU NDIYE ATAKAYEAMUA NI AINA GANI YA KURA IPIGWE . TAHADHARI ;kama m/kiti akiamua iwe ya wazi au ya siri hakuna mjumbe/au mbunge yeyote atakae pingana nae kwa kuwa kanuni zinampa mamlaka iwe iwavyo. Poleni Wajumbe kwa kuuziwa mbuzi kwenye Gunia leo hii
 
Ni mtazamao wa chama Tawala baada ya kuchekecha kila aina ya uwezekano wa kupitisha kifungu cha upigaji kura ya wazi au siri. Chama kimeona haitakuwa rahisi kwa sasa kupitisha kipengele chao cha kura ya wazi kwa kuwa wajumbe walio wengi (the 201) hawafahamiki tabia zao na misimamo yao.

Chama kimejipanga kama inavyoelekea kuamuliwa kwamba Bunge lianze, na kipengele hicho kirudiwe wakati bunge likiendelea. Ktk kipindi cha bunge kuendelea, CCM watajipanga jinsi ya kuwaingia wajumbe wengine walio nje ya chama. Watawashawishi kwa ahadi na itakapobidi pesa zitatumika kuwashawishi. Pia wanategemea kumtumia Sitta kwanza ajenge uaminifu kwa wajumbe, wamuone ana niya njema kama dalili zinavyijiojyesha sasa hivi, baadaye atumie uzoefu wake kuwarubuni wajumbe. Rais atakapofungua rasmi bunge pia atatumika kuwaonyesha kwamba wananchi wanahitaji kuwaona kila hatua wanayopitia. Ataonyesha umuhimu wa kura ya wazi ili mitaani pia waone ni njia nzuri. CCM watakapokuwa wamejiridhisha wataomba kura zipingwe kuamua hicho kipengele.

Msiri wetu amasema hayo wakati pia akiwa na wasiwasi kwamba "......hata kama milioni mia moja kwa kila mjumbe anayekubali zitatolewa, hakuna aliye na uhakika kwamba wakipiga kura watafanya kama watakavyoahidi, maana bunge hili lina wasomi ambao misimamo yao mingine ni migumu kuigeuza...."

Huo ndo muujiza unaosubiliwa. Hakika kuna tatizo hapa maana jioni hii, M/kiti anasema wajumbe waje wamevaa kibunge. Bunge linaelekea kuanza wakati hakuna kanuni zilizo kamili. yaani zikiwa na utata. Kila mjadala mwisho wake ni kura, kura yenyewe haieleweki. Binafsi nadhani pia M/kiti Pandu kisha choka matusi ya wazoefu wa bungeni.

Tusubiri.
 
Hivi hakuna mtu tunaweza kutengeneza bomu la nyuki lililochanganyikana na m.a.v.&*, tuwashikishe adabu kidogo?? Hii ni dharau kwa watanzania. Nilijikuta napata hasira sana wakati naangalia hiyo "komedi"
 

I cannot believe this .Yaani Mahalu ? Naye ni Prof au ni nani ?
 
Mimi niliangalia bunge session ya asubuhi nikashindwa kuelewa walikutana kujadili nini hasa????
Manake wanaanza wanabishana then ghafla wanahairisha hadi jioni...

hao hata wakipewa mwaka hawatamaliza kudiscuss hiyo katiba mpya wallah

sipendi kabisa kuliangalia hili bunge huwa napata na kichefu chefu
 
Huyo mwenyekiti wa Kudumu ni Samweli Sitta Mbunge wa CCM, akiamua kusema iwe kura ya Siri itajulikana kabisa amepewa Shinikizo na Chama chake cha CCM maana ndo msimamo wao. Italeta mzozo tu tena, njia hapa ilikuwa ni kukubali utaratibu uliozoeleka siku zote KURA ya SIRI. Hata Katiba itakapo letwa kwa wananchi itapigiwa kura ya Siri, siyo ya wazi. Kura ya wazi ni kwa maslahi ya kundi flani, ila kura ya siri ni kwa maslahi ya Taifa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…