Yaliyojiri katika Chaguzi Ndogo: Uchaguzi wa ubunge jimbo la Dimani na madiwani Tanzania Bara

Huo muhuri hapo chini nilitegemea uwe wa ZEC mkuu
Huu ni uchaguzi wa m-bunge wa bunge la jamhuri ya muungano wa Tanzania, sio wa baraza la uwakilishi Zanzibar, hivyo usimamiwa na tume ya taifa ya uchaguzi
 
Wewe endelea kusubiri yenye Tarehe acha sie tuendelee kushangilia na ukishapata yenye Tarehe usisahau kuwa Tume si huru na kura zenu zimeibiwa!
Tarehe ipo nyuma ya karatasi.
 
Mbona hukusema haya kabla ya uchaguzi?
 
Jecha ni SI Unit

Leo akiwa na Tido Mhando kwny Mahojiano amesema yeye akiwa Kama Nahodha akiona Mawimbi Makali chombo Kinakwenda Mrama hatohitaji ruhusa ya Mmiliki wa Meli kuchukua hatua za dharura kunusuru Chombo
 
Umepanic
Mbona jamaa kaeleza vizuri
Umemuelewa vibaya.

Cdm mlikalia kick poleni
Ikiwa ni kiki au vyovyote vile lkn kumbuka refa siku zote unaweza kumzani kumbe makaratas mliyoyaandika ndiyo anayofuata na kumbe tena makosa lkn kadili siku zinavyokwenda si kweli akili zitakuwa zile za zamani ndipo utakaposema kwnn haikuwa vile lkn mungu akujalie hekima tena.
 
Mtaisoma namba tu. Uchaguzi mdogo umekwisha na mwenye macho haambiwi tazama. Ukawa hamna kitu. Porojo nyingi tu. Pigeni kelele za njaa feki Dr JPM huyooooo njia nyeupe 2020
 
hahahaha eti CCM wameshinda kata zote ila chadema wameshinda wana kata line za Vodacom....teh teh
 
Lembeni, Mateves,kijichi,kiwanja cha ndege,kahama na Geita CHADEMA wameshashinda hata kabla ya uchaguzi, watangazwe tu washndi hakuna namna!
Wapinzani washinde kwa sera za tetemeko, njaa, kauli za rais hazifurahishi, majipu yanaonewa, kuvunja line za vodacom, mtasubili sana hadi pale mtakapo kubali kutumia akili zenu.
 
Kuna watu huwa wanajaribu kufananisha ngozi nyeupe na nyeusi..huwa nawaona kama machizi...apa ndo uone tofauti ya ngozi hizi mbili
 
Wapinzani washinde kwa sera za tetemeko, njaa, kauli za rais hazifurahishi, majipu yanaonewa, kuvunja line za vodacom, mtasubili sana hadi pale mtakapo kubali kutumia akili zenu.

Waambie hao
 
Hakika ninepatwa na simanzi kubwa baada ya baadhi ya matokeo ya uchaguzi katika maeneo mbalimbali ya nchi yetu kwa nafasi za udiwani na ubunge kule Dimani Zanzibar.

Kwa yaliyotokea kwa CCM kushinda viti vingi vya Udiwani na jimbo la Dimani kule Zanzibar ni wazi kuwa yalishaonekana na yalijulikana mapema hata kabla ya uchaguzi.Rafu zimechezwa na wapinzani kwa unyonge wameinamisha shingo kusubiri kisu kiwapitie.Mwelekeo ulishaonekana tangu awali.....

Mkurugenzi ambaye ndiye msimamzi wa uchaguzi katika jimbo amepata cheo hicho kama hisani ya ukada wake kutoka chama tawala na bado wapinzani wanapoteza muda wao na fedha zao kushiriki uchaguzi ambao mshindi tayari ameshajulikana..

Mpinzani umefungwa kamba mikono na miguu unaingizwa ulingoni upambane na mtu ambaye hajafungwa kamba na anasaidiwa na dola na bado una matumaini ya kushinda......haiwezekaniii.

Ushauri wangu wa kipuuzi kwenu Wapinzani Msishiriki uchaguzi wa aina yoyote waachieni hao wanaoona utawala wa nchi hii ni alfa na omega na kwamba wao ndiyo wana stahiki ya kutawala nchi hii milele.Kwani kwa kushiriki uchaguz ambao mshindi anajulikana ni kujitia matope mbele ya sisi wapiga kura;oneni sasa wanawaambia siasa zenu za kusambaza uchochezi zimewacost [HASHTAG]#NJAA[/HASHTAG] [HASHTAG]#DEMOKRASIA[/HASHTAG] ......[HASHTAG]#MWAFAA[/HASHTAG]

Yangu ya kipuuzi ni hayo
Tchao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…