Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe 26 Jan 2022. Shahidi wa 12 Luteni Denis Urio kuendelea kutoa ushahidi wake

Mimi sijaelewa kabisa huo muunganiko asee. Wale mashahidi wengine wote walikana kabisa kukuta mawasiliano sala viashiria vya ugaidi kwa washtakiwa, huyu aliyetegemewa nae leo ndo anasema aliwaambia wanaenda kufanya kazi ya ulinzi anaulizwa sasa kwanini uliwadanganya wanaenda kufanya kazi ya ulinzi eti jibu ni ili mission ifanikiwe! So mission ni kumkamatisha mbowe tu
 
Mahakamani, Urio kasema aliwapa pesa hizo wakafanye uhalifu. Wakati anawapa pesa hizo, aliwaambia ni kwenda kufanya kazi ya ulinzi kwa Freeman. Kwamba ni za kufidia usafiri pamoja na kujikimu na wengine kusafiri kutoka Morogoro kwenda Dar. Hayo mengine yote unayosema haya make any sense.

Wote tunasoma kitu kimoja lakini uelewa ni wa tofauti. Nakushangaa.
 
Fuatilia mwenendo wa kesi, utapata majibu yake soon! BTW: They were apprehended before their dirty mission went to effect!
Unafuatilia kesi hii hii? Maana kama una ushahidi wa tofauti nenda mahakamani ama mtafute Kingai akuunganishe kwenye jopo la mashahidi wa upande wa mashitaka.
 
Huyo jamaa Jasmoni Tegga uelewa wake unamashaka huenda ndio kingai mwenyewe
 
Bwire ndo alumwambia urio kuwa madogo wameenda moshi kum Term sabaya,
Urio akatoa ripoti faster kwa kingai kwamba kuna wet mission iko on progress, nadhani kina kingai wakampanick na kupelekea kukamatwa kwa madogo kabla hajatekeleza mission(if true)
Kabla ya hapo si tayari Urio alikuwa ameshaambiwa awatafute watu Kwa ajili ya kutenda uhalifu!Halafu Urio akawatafuta watu aliowatrain Kisha akawaficha lengo hasa,akawadanganya wanaenda kufanya kazi ya ulinzi!
Kuna kitu hakiko sawa hapo!Kesho na ifike!
 
Hivi kweli Mbowe apange kufanya ugaidi halafu chama chake Cha CHADEMA kisihusike kwa namna yoyote?


Imetumika akili ndogo sana kupanga haya mashitaka.
Kweli ni kichekesho cha hali ya juu sana, lakini unategemea nini kutoka kwa serikali inayosema hadharani mawaziri wale kwa urefu wa kamba zao
 
Sasa mtaalamu wa "Cellebrite" ambaye anafanya kazi ya ethical hacking alisema hakuona viashiria vyovyote vya ugaidi!
Wewe unasemaje?
Mie sisemi kitu, nachojua kipindi hicho wangetaka maongezi ya simu zote kati ya mbowe na urio yangekuwa recorder
 
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 26/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani....
Yaani Mbowe atafute makomandoo kabla hajawapata aseme anataka watu wa kuja kufanya fujo, nchi isitawalike, kuchoma masoko na Vitua vya mafuta? Huyo huyo anasema tunatafuta kushima dola na wakati uchaguzi bado aanza kulipua vituo vya mafuta na kutandika magogo??

Ltn Ltn Ltn usiaibishae jeshi letu.
 
Angekuwa undercover Adamoo asingeweza kusema tulimsikia Urio akilia kwa uchungu Tazara katika case ndani ya kesi... Anyway watu hawaifuatilii hii kesi..
Huyo Urio kala kibano cha kimataifa.. kuna kitu hapo
Ltn Urio anatumika tu. Sema hii senema ilitungwa kishamba sana.

Hata mimi nisiye hata na usungu sungu siwezi kufanya maigizo haya.
 
Mtunga senema Jambazi Sabaya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…