Wapi amesema hivyo lete hiyo hoja yake hapa tuone.
Jaji: Shahidi tunakushukuru kwa ushahidi.
Wakili Kidando: Baada ya ushahidi wa shahidi huyu wa kumi na tatu tunaialika Mahakama yako chini ya kifungu 41 (1) cha sheria ya Uhujumu Uchumi ione washtakiwa wote wanne wana kesi ya kujibu hivyo hatua nyingine kwaajili ya kujitetea ifuate kwa upande wetu tunafunga kesi hii.
Jaji: Mahakama imekubaliana na maombi ya upande wa mashitaka kufunga kesi hii.
Wakili Kibatala: Baada ya upande wa mashtaka kufunga kupitia kifungu hicho cha 41 tunaomba mahakama hii itupe nafasi ya kufanya mawasilisho ya mwisho.
Lakini pia tuna maombi mawili ombi la kwanza Mahakama itupe mwenendo wa kesi lakini pili tupewe nafasi yakufanya mawasilisho ya mwisho oral.
Jaji: Kwanini unataka kufanya mawasilisho orally.
Kibatala: Tulikuwa tumeshajadiliana mwanzoni na kunafaida fulani fulani tutazipata.
Wakili Nashon Nkungu: Kwa niaba ya mshtakiwa wa kwanza: Tunaomba mawasilisho ya mwisho tuyafanye kwa njia ya mdomo na kupewa mwenendo wa kesi.
Wakili John Mally: Niunge mkono hoja za mawakili wenzangu na kuomba kufanya mawasilisho ya mwisho kama kuna kesi ya kujibu au la.
Wakili Fredrik Khiwelo: Kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu: Niungane na wenzangu lakini pia na mimi ningeomba kupatiwa mwenendo wa kesi kwaajili ya kufanya mawasilisho ya mwisho kwa njia ya mdomo.
Wakili Kidando: Tukirejea kifungu cha 41 bado upande wa mashtaka tunaomba kufanya kwa nija ya maandishi
Shauri hili ukizingatia limeanza Septemba mwaka jana hatujajua itachukua muda gani kupata mwenendo wa kesi.
Jaji: Hadi leo PS wangu ameshachapa kurasa 1,400 nikichanganya za jana na leo zinaweza kufika 1,600 nilikuwa nafikiria hapa nadhani nipatiwe dakika kumi tukajadiliane.
Mahakama imerejea baada ya majadiliano na mawakili wa pande zote.
Jaji: Baada ya kusikiliza na kupitia hoja za pande zote mbili na kuzingatia kifungu cha 41 cha Sheria ya Uhujumu Uchumi, Mahakama hii itatoa uamuzi Februari 18, 2022 kama washtakiwa wana kesi ya kujibu au la saa nane mchana na washtakiwa mtaaendelea kubaki chini ya uangalizi wa Magereza.