Huyu ndo goodluck wasiku zote au huyu ni mpya?Leo kizimbani tunaye Goodluck kutoka kitengo maalumu cha crucifixion
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Huyu ndo goodluck wasiku zote au huyu ni mpya?Leo kizimbani tunaye Goodluck kutoka kitengo maalumu cha crucifixion
huyu huyu wa siku zote mtesajiHuyu ndo goodluck wasiku zote au huyu ni mpya?
Naona sisi hatutajwi!Mh The Sheriff na sisi tuko kama tulivyo kufatilia Shauri
Kumbe ni yeye; nilijua ni mtu mwenye cheo kikubwa.Huyu ndo goodluck wasiku zote au huyu
Mahakama inatutambua indirectlyNaona sisi hatutajwi!
Ibarikiwe sanaMungu Ibariki CHADEMA
Mungu aibariki familia yake na kizazi chake chote.Ninamsubiri Kibatala na nduguze
Wakili msomi Matata kaenda wapi jamani?Anatakiwa kuonekana kwenye hiyo list ya Kibatala.Salaam Wakuu,
Leo tarehe 21/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.
Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.
Kujua kesi ilipoishia soma: Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe na Wenzake leo 20/01/2022. Shahidi 10 amaliza, shahidi wa 11 mwingine kuanza ushahidi kesho 21/01/2022
UPDATES
Jaji ameingia Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na
Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Mawakili wa Serikali Waandamizi Na
Tulimanywa Majige Wakili wa Serikali
Wakili Peter Kibatala Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na
wakili Nashon Nkungu
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Michael Mwangasa
Michael Lugina
Khadija Aron
Maria Mushi
- Jaji anaita washitakiwa Wote Wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja, Tupo tayari Kuendelea
Peter Kibatala: Mheshimiwa Na sisi Pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea
- Jaji anaandika
- Shahidi anaingia, ni kijana mrefu mweusi
Jaji: Jina Lako
Shahidi: Naitwa H4347 Goodluck
Jaji: Umri
Shahidi: Miaka 32
Jaji: Dini yako
Shahidi: Mkristo
Jaji: kazi yako
Shahidi: Askari Polisi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ataongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shahidi Unaitwa Nani
Shahidi: Naitwa namba H 4347 Detective Afande Goodluck
Wakili wa Serikali: Wewe ni Polisi tangu lini
Shahidi: 2013
Wakili wa Serikali: Kituo cha Kazi ni wapi
Shahidi: Nipo Central Arusha
Wakili wa Serikali: Una Cheo gani
Shahidi: Nina Cheo Cha sergeant
Wakili wa Serikali: Ulikipata lini
Shahidi: Mwaka 2021 Mwezi wa Nane
Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama Central Police Arusha una nafasi gani
Shahidi: Ni Mpelelezi Wa Makosa ya Jinai
Wakili wa Serikali: Ukiwa Kama Askari Polisi una Majukumu gani
Shahidi: Kukamata Wahalifu Kuhoji, Kupekua, Kukamata Vielelezo Husika, Kutekeleza Majukumu Mbalimbali ninayopewa na Wakubwa Zangu
Wakili wa Serikali: Unasema Unapeleleza Kitu gani Shahidi
Shahidi: Napeleleza Makosa Ya Jinai
Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama Tarehe 04 August 2020 ulikuwa wapi
Shahidi: Nakumbuka Nilikuwa Kazini Kituoni Central Arusha Nikiendelea na Majukumu Yangu ya Kazi
Wakili wa Serikali: Eleza Majira Ya Jioni Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Majira ya Jioni nilipata Maelekezo Kutoka Kwa Afande Mahita Nilikuwa nahitajika Kwa Afande RCO
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unahitajika wewe na nani
Shahidi: Mimi na koplo Francis
Wakili wa Serikali: Afande Mahita ni nani hapo Kituoni
Shahidi: Ni Msaidizi Wa OC CID
Wakili wa Serikali: Maelekezo hayo uliyatekeleza Kwa Namna gani
Shahidi: Tuliondoka Mimi na Afande Mahita Tukaenda Kwa Afande RCO
Wakili wa Serikali: Mlienda Wapi
Shahidi: Mkoani, Makao Makuu ya Polisi
Wakili wa Serikali: Wakati huo RCO Mkoa wa Arusha alikuwa ni nani
Shahidi: Alikuwa Afande Ramadhan Kingai
Wakili wa Serikali: Malipo wasili Kwa RCO Kitu gani Kilitokea
Shahidi: Tulipo fika Kwa Afande RCO Afande alisema Kuna kazi inatakiwa Kufanywa Kwa hiyo tujiandae
Wakili wa Serikali: Maelezo Ya Kujiandaa na Kitu gani
Shahidi: Mimi na Afande Francis Tulienda Kituoni Tukachukua Silaha
Wakili wa Serikali: Wewe Ulichukua Silaha gani
Shahidi: Mimi nili chukua Silaha aina ya AK 47
Wakili wa Serikali: Na Mwenzio naye alichukua Silaha gani
Shahidi: Na Yeye alichukua AK47
Wakili wa Serikali: Baada ya Kuchukua Silaha wewe Na Mwenzio Mlielekea Wapi
Shahidi: Tulielekea Kwa Afande RCO Mkoani
Shahidi: alituelekeza Tuelekee Kituo cha Polisi USA RIVER Wilaya Ya Arumeru
Wakili wa Serikali: Unakumbuka Ilikuwa Mida ya Saa ngapi?
Shahidi: Majira ya Saa 12 Jioni
Wakili wa Serikali: Safari ya Kuelekea USA RIVER ilihusisha Watu gani?
Shahidi: Afande RCO mwenyewe, Mahita, Mimi Mwenyewe pamoja na Afande Francis
Wakili wa Serikali: Baada ya Kufika USA RIVER Kilikuwaje
Shahidi: Tulielekea Kituoni Tukamkuta OC CID pale Kituoni
Wakili wa Serikali: ambaye alikuwa ni nani
Shahidi: alikuwa Afande JUMANNE
Wakili wa Serikali: Mlimkuta Eneo gani
Shahidi: Nje ya Kituo
Wakili wa Serikali: Baada ya Hapo
Shahidi: Afande alitukaribisha Ofisini Kwake, Tukaingia Wote
Wakili wa Serikali: Mkiwa Ofisini Kitu gani Kilifanyika