Yaliyojiri katika kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na Wenzake tarehe21/01/2021. Kesi imeahirishwa hadi 24/ 01/ 2022

Yaliyojiri katika kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na Wenzake tarehe21/01/2021. Kesi imeahirishwa hadi 24/ 01/ 2022

Huyu jamaa hapa lazima izaliwe kesi ndogo na kukataliwa baadhi ya ushahidi. Huyu lazima akumbane na mapigo hatari ya PK.
 
Hatimaye Goodluck yupo kizimba cha ushahidi leo...
 
Salaam Wakuu,

Leo tarehe 21/01/2022 kesi ya Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe inaendelea.

Ungana nami katika uzi huu ili kujua kila kinachojiri Mahakamani.

Kujua kesi ilipoishia soma: Yaliyojiri katika kesi ya Mbowe na Wenzake leo 20/01/2022. Shahidi 10 amaliza, shahidi wa 11 mwingine kuanza ushahidi kesho 21/01/2022

UPDATES


Jaji ameingia Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani

Wakili wa Serikali Robert Kidando Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na

Pius Hilla
Abdallah Chavula
Jenitreza Kitali
Nassoro Katuga
Esther Martin
Ignasi Mwinuka
Mawakili wa Serikali Waandamizi Na
Tulimanywa Majige Wakili wa Serikali

Wakili Peter Kibatala Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na

wakili Nashon Nkungu
John Mallya
Fredrick Kihwelo
Michael Mwangasa
Michael Lugina
Khadija Aron
Maria Mushi

- Jaji anaita washitakiwa Wote Wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani

Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kusikilizwa na Leo tuna shahidi Mmoja, Tupo tayari Kuendelea

Peter Kibatala: Mheshimiwa Na sisi Pia Mheshimiwa Jaji tupo tayari Kuendelea

- Jaji anaandika

- Shahidi anaingia, ni kijana mrefu mweusi


Jaji: Jina Lako

Shahidi: Naitwa H4347 Goodluck

Jaji: Umri

Shahidi: Miaka 32

Jaji: Dini yako

Shahidi: Mkristo

Jaji: kazi yako

Shahidi: Askari Polisi

Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ataongozwa na Wakili wa Serikali Pius Hilla

Wakili wa Serikali Pius Hilla: Shahidi Unaitwa Nani

Shahidi: Naitwa namba H 4347 Detective Afande Goodluck

Wakili wa Serikali: Wewe ni Polisi tangu lini

Shahidi: 2013

Wakili wa Serikali: Kituo cha Kazi ni wapi

Shahidi: Nipo Central Arusha

Wakili wa Serikali: Una Cheo gani

Shahidi: Nina Cheo Cha sergeant

Wakili wa Serikali: Ulikipata lini

Shahidi: Mwaka 2021 Mwezi wa Nane

Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama Central Police Arusha una nafasi gani

Shahidi: Ni Mpelelezi Wa Makosa ya Jinai

Wakili wa Serikali: Ukiwa Kama Askari Polisi una Majukumu gani

Shahidi: Kukamata Wahalifu Kuhoji, Kupekua, Kukamata Vielelezo Husika, Kutekeleza Majukumu Mbalimbali ninayopewa na Wakubwa Zangu

Wakili wa Serikali: Unasema Unapeleleza Kitu gani Shahidi

Shahidi: Napeleleza Makosa Ya Jinai

Wakili wa Serikali: Eleza Mahakama Tarehe 04 August 2020 ulikuwa wapi

Shahidi: Nakumbuka Nilikuwa Kazini Kituoni Central Arusha Nikiendelea na Majukumu Yangu ya Kazi

Wakili wa Serikali: Eleza Majira Ya Jioni Kitu gani Kilitokea

Shahidi: Majira ya Jioni nilipata Maelekezo Kutoka Kwa Afande Mahita Nilikuwa nahitajika Kwa Afande RCO

Wakili wa Serikali: Ulikuwa unahitajika wewe na nani

Shahidi: Mimi na koplo Francis

Wakili wa Serikali: Afande Mahita ni nani hapo Kituoni

Shahidi: Ni Msaidizi Wa OC CID

Wakili wa Serikali: Maelekezo hayo uliyatekeleza Kwa Namna gani

Shahidi: Tuliondoka Mimi na Afande Mahita Tukaenda Kwa Afande RCO

Wakili wa Serikali: Mlienda Wapi

Shahidi: Mkoani, Makao Makuu ya Polisi

Wakili wa Serikali: Wakati huo RCO Mkoa wa Arusha alikuwa ni nani

Shahidi: Alikuwa Afande Ramadhan Kingai

Wakili wa Serikali: Malipo wasili Kwa RCO Kitu gani Kilitokea

Shahidi: Tulipo fika Kwa Afande RCO Afande alisema Kuna kazi inatakiwa Kufanywa Kwa hiyo tujiandae

Wakili wa Serikali: Maelezo Ya Kujiandaa na Kitu gani

Shahidi: Mimi na Afande Francis Tulienda Kituoni Tukachukua Silaha

Wakili wa Serikali: Wewe Ulichukua Silaha gani

Shahidi: Mimi nili chukua Silaha aina ya AK 47

Wakili wa Serikali: Na Mwenzio naye alichukua Silaha gani

Shahidi: Na Yeye alichukua AK47

Wakili wa Serikali: Baada ya Kuchukua Silaha wewe Na Mwenzio Mlielekea Wapi

Shahidi: Tulielekea Kwa Afande RCO Mkoani

Shahidi: alituelekeza Tuelekee Kituo cha Polisi USA RIVER Wilaya Ya Arumeru

Wakili wa Serikali: Unakumbuka Ilikuwa Mida ya Saa ngapi?

Shahidi: Majira ya Saa 12 Jioni

Wakili wa Serikali: Safari ya Kuelekea USA RIVER ilihusisha Watu gani?

Shahidi: Afande RCO mwenyewe, Mahita, Mimi Mwenyewe pamoja na Afande Francis

Wakili wa Serikali:
Baada ya Kufika USA RIVER Kilikuwaje

Shahidi: Tulielekea Kituoni Tukamkuta OC CID pale Kituoni

Wakili wa Serikali: ambaye alikuwa ni nani

Shahidi: alikuwa Afande JUMANNE

Wakili wa Serikali:
Mlimkuta Eneo gani

Shahidi:
Nje ya Kituo

Wakili wa Serikali: Baada ya Hapo

Shahidi: Afande alitukaribisha Ofisini Kwake, Tukaingia Wote

Wakili wa Serikali: Mkiwa Ofisini Kitu gani Kilifanyika
Wakili msomi Matata kaenda wapi jamani?Anatakiwa kuonekana kwenye hiyo list ya Kibatala.
 
Back
Top Bottom