Nilishasema toka mwanzo CCM hata wangemsimamisha yule mkulima bado watashinda tu sababu UKAWA hamna mgombea makini Dr.Slaa atabikia kuwa rais kivuli tu.
Nape mkali jamani anaulizwa maswali na waandishi wa habari anawaambia wakitaka wakasome katiba ya chama inasemaje...
Kawa mkali kama Mbogo...
Wanabodi,
Yale Mafuriko yaliyosumbua kwa muda mrefu katika kipindi cha karibuni hatimaye yamezuiwa Rasmi kwa Kalamu ya Sh.200 tuu pale Dodoma, baada ya Mamvi kukatwa kirahisi mno.
Ni simanzi kubwa sana, safari ya matamanio iliyokuwa na mafuriko makubwa kila pembe ya Jamhuri yetu, hatimaye imebaki kuwa Historia.
Cc: Pasco MUSSA ALLAN na wengine wote Team Lowassa.
Mbona hapachimbiki jamani au mpo ICU?
Kwanza nitangaze msimamo wangu kuwa sio shabiki wa CCM. Ningependa kuona CCM inapumzishwa angaa kwa muhula mmoja ili tujaribishe utawala mbadala na yenyewe ijifunze kuwajibika. Lakini kwa uamuzi wa kukata jina la mzee wa maamuzi magumu mapema ni hatua moja ya kihistoria katika uhai wa chama kwa kuzima utamaduni, tena utamaduni mbaya, ambao alikuwa ameuasisi kuwa ili ufanikiwe kuteuliwa ni lazima kwanza ufisidi (maana hatujawahi kuelezwa mzee wa maamuzi magumu hufanya biashara gani wakati toka akiwa kijana ni mtumishi wa umma) ili upate hela za kukufanya 'ukubalike', yaani ununue ukubalifu!!! Kuzima utamaduni huu kunaweza kuwasaidia kurejesha imani ya baadhi ya wanaCCM waliokuwa wameanza kukata tamaa kuwa wenye chama sasa ni vibaka.Wakuu hapa Dodoma ni kama kumepita ugonjwa wa mnyoofu sababu hali si muhali hata kidogo!
Watu wamenyong'onyea sana and keep my word CCM inaenda kupitia kipindi kigumu sana.
walisema hawakukutana barabarani
Zaidi Lowasa alivokuwa bagamoyo akasema kwa kikwete pia ni kwake
Ile kauli niliitafakari sana.
Ina maana na Salma pia Ni wa kwake Lowasa
mkuu ungeachana kwanza na kutuwekea hayo mavideo yako,, nani ana muda wa kuyaangalia sasa hivi?
Halafu asubuhi hii wanakimbilia St Gasper Hotel wameenda kujipanga walete (sijui ni fujo huko NEC?)waliokuwa wanasema patachimbika nasubir pachimbike, sasa naona kimyaaaa! walikopotelea hata sijui!
Si alituambia hakuna Rufaa???
Ametengua lini kauli yake??