Yusomwasha
JF-Expert Member
- Dec 5, 2014
- 2,092
- 839
Jamani watanzania wenzangu tusubiri tu watangaze achani kutoa taarifa za uongo bila evidence..
Mwaka huu mtashudia ccm inavyopasuka vipande viwili mamvi anaondoka na nusu ya ya mataycoon kuanzisha chama kipya endapo mazungumzo na ukawa yakiferi kumbuka ukawa bado hawajatangaza mgombea wao kinachooendelea Dodoma kinawahusu sana kwa kuanzia kuna gari 60 zimeagizwa na timu mamvi kabla ya September zinatakiwa kuanza kazi moja tu kila MTU anaijua tusubiri ........
ilikuwa kuvuana maGAMBA sasa hivi kumKATAFaizaFoxy
Tetesi 5 bora ni hii hapa
1. Pinda
2. Bilal
3. Jaji Ramadhani
4. Membe
5. Asha Migiro
habari wanajanvi, mda huu dodoma hali si ya kawaida kama ilivyozoeleka , wapambe watia nia mbali mbali wameonekana kusononeka sana na wengine kutoweka kabisa karibia na eneo la tukio la mchakato mzima wa kumpata mtia nia, wameanza kuwapunguza wengi hasa ambao hawana vigezo kamili na mlolongo wa ukataji ulikuwa hivi
1. ametolewa ambaye elimu yake si sawa na anayetakiwa, yule mtia nia wa kigoma mr mahale,
2.wakatolewa wenye kashfa nzito sana na ni vigumu kuwasafisha hapa tuna, edward lowassa..richmond, . sospeter muhongo ,, tegeta escrow, sumaye.. uuzwaji wa nyumba zza serikali na uuzaji wa mashirika ya umma ovyo, membe kaponea chupuchupu kukatwa ana makundi ya kukigawa chama, wasira ana kashfa ya rushwa mwaka 1995,
3.uzoefu na umri, japo wote wametimiza umri lakini bado hawajawa na uzoefu wa kutosha, hapa ni kigwangala, na mwigulu nchemba.
waliotangulia kuingizwa kwenye list ni
1.asha rose migiro gender factor , uwajibikaji wake na usafi wake
2.augustino ramadhan zanzibar factor na kutokuwa na makundi na uwajibikaji wake,
3.makongoro nyerere, uwajibikaji na kuchukia rushwa kukemea hadharani wala rushwa na hali ya juu ya uthubutu kwenye maslahi ya wengi hana woga, pia nyerere factor usafi na kumuenzi mwalimu nyerere,
4.pombe magufuri, uwajibikaji wake na hasa kutekeleza sheria bila kupindishwa, na muwajibikaji wa hali ya juu
5. mizengo pinda , ni kiongozi mkuu wa serikali imekuwa vigumu serikali yenyewe kushindwa kutompitisha mtekelezaji mkuu wa ilan ya chama hicho bungeni na pia akikatwa itaonekana serikali nzima ilikuwa haifai, pia ni mtu msafi mwenye busara
6. samwel sitta, kwakuwa anasimamia sana matakwa ya chama na ameweza kutoyumbishwa wakati wa katiba mpya, amepitisha mapendekezo asilimia kubwa yaliyokuwa yanapendelewa na chama chake,mbali ya hapo ana uthubutu na ni mwajibikaji,
7.mark mwandosya
8.bernad membe
hapo ndo itatoka tano bora ,tatu mpaka moja bora,
Hata wao wapo jf
Kingunge, Kone na Msindai wanaratibu mpango wa kumng'oa Mwenyekiti wa CCM,KIKWETE
Wadau amani iwe kwenu.
Taarifa nilizopata hivi punde kutoka Dodoma zinasema kuwa baada ya Team Lowasa, Friends of Lowasa na 4U MOVEMENT kubaini kuwa jitihada za mafisadi za kufanikisha Lowasa anaenda Magogoni zinagonga mwanba, mawakala wa mafisadi hao chini ya uratibu wa Kingunge Ngombale Mwiru na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Kone wanaratibu mpango wa kumuondoa Madarakani Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete. Taarifa zinasema kuwa mawakala hao wa mafisadi wameshindwa kutekeleza mpango wao huo ndani ya kikao cha Kamati Kuu na sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ambao utafanyika hivi punde.
Taarifa zinasema pia kuwa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai naye amejiunga kwenye harakati hizo ili kuhakikisha kuwa kubwa la mafisadi nchini, Edward Lowasa linaenda Ikulu iwe kwa amani au kwa shari. Katika kuhakikisha kuwa lengo hilo linafanikiwa, muda mfupi uliopita Kingunge, Kone na Msindai wameonekana maeneo ya Chuo Kikuu cha St Gasper wakigawa fedha ambapo taarifa mjumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu aliyejiunga kwenye timu ya mafisadi amepewa shilingi milioni 5. Aidha, wajumbe hao wameahidiwa shilingi milioni tano nyingine ambazo wameahidiwa kupewa ikiwa watafanikiwa lengo lao hilo.
Baadhi ya wajumbe ambao wamepenyeza taarifa hizi wamedai kuwa wanachofanya akina Kingunge ni cha kipuuzi hasa baada ya Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa kuziba mianya yote ya mafisadi kumpitisha mtu wao. Kwamba Rais Kikwete anasimamia haki na wamempongeza kwa kusimamia misingi ya chama.
Wadau, hawa ndio mafisadi. Wameamua liwalo na liwe kuhakikisha kuwa fisadi lao linaenda Ikulu. Nawaomba Watanzania kusimama imara kupinga mkakati huu ovu ili chama chetu na nchi yetu isingie kwenye machafuko. Bahati nzuri wanaofanya vitendo hivi wanafahamika. Watambue kuwa kumchezea Mwenyekiti wa CCM ni kumchezea Mkuu wa nchi kwa vile Kikwete ana kofia mbili.
Ratiba inavyosema,
Saa 4-7 mchana
kamati ya maadili (tayari)√
Saa 8- 12 jioni
Kamati kuu CC - majina matano (tayari)√
Je kwanini majina yameshindwa kutajwa?
Saa 2 usiku
NEC - majina matatu (kikao kinaendelea)
manyumbu wengi
Nape atatangaza matokeo baada ya DAKU. ikifika asubuhi yatakuwa yamebaki majina 3. magazeti yatapata nafasi ya kuandika JINA MOJA Jumapili.... Hii ndio taiming ya kumchinja Lowassa bila kuwa na madhara ya kipropaganda za kina Kingunge. Wamebanwa kila kona. Hawafurukuti.....
Lowassa sasa wanamunywesha gulukosi....
kwani haijajulikana,mbona taarifa zimezagaa.Team Lowasa wameshapoteana hawawezi kuchomoza tena.ni kama Yanga ikibutulia 5 bila na Simba unadhani Jeri Muro ataleta kidomo domo
mpaka saa tano hakuna lolote. laleni, ccm wametuudhi bungeni, wasubiri uchaguzi tuwalipe malipo yao
Tetesi 5 bora ni hii hapa
1. Pinda
2. Bilal
3. Jaji Ramadhani
4. Membe
5. Asha Migiro
Wanatafuta mtu atakayeweka historia ya chama kumfia mikononi
Taarifa nilizozipata kutoka Dodoma ni kwamba kuna mvutano mkali sana miongoni mwa wajumbe wa NEC,wafuasi wa Lowassa wamechachamaa na kumweka Mwenyekiti ktk wakati mgumu sana,uwezekano ni kwamba huenda jina la Lowassa likaingia kwenye 5 bora ili kuepusha vurugu zitakazoweza kutokea endapo jina lake litakatwa.Hali ni mbaya kuliko ilivyotarajiwa.