IRINGA MOJA
JF-Expert Member
- Nov 13, 2014
- 503
- 229
mi naona bora hata angesema Ngereja au Muhongo.Membe??
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
mi naona bora hata angesema Ngereja au Muhongo.Membe??
kajipange story yako nzuri kusoma ila haina mashiko coz imekaa kisiada zaidi bila fact za maana wataje waliopewa tuwajue na sio waliotoa peke yao.Kingunge, Kone na Msindai wanaratibu mpango wa kumng'oa Mwenyekiti wa CCM,KIKWETE
Wadau amani iwe kwenu.
Taarifa nilizopata hivi punde kutoka Dodoma zinasema kuwa baada ya Team Lowasa, Friends of Lowasa na 4U MOVEMENT kubaini kuwa jitihada za mafisadi za kufanikisha Lowasa anaenda Magogoni zinagonga mwanba, mawakala wa mafisadi hao chini ya uratibu wa Kingunge Ngombale Mwiru na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Kone wanaratibu mpango wa kumuondoa Madarakani Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete. Taarifa zinasema kuwa mawakala hao wa mafisadi wameshindwa kutekeleza mpango wao huo ndani ya kikao cha Kamati Kuu na sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ambao utafanyika hivi punde.
Taarifa zinasema pia kuwa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai naye amejiunga kwenye harakati hizo ili kuhakikisha kuwa kubwa la mafisadi nchini, Edward Lowasa linaenda Ikulu iwe kwa amani au kwa shari. Katika kuhakikisha kuwa lengo hilo linafanikiwa, muda mfupi uliopita Kingunge, Kone na Msindai wameonekana maeneo ya Chuo Kikuu cha St Gasper wakigawa fedha ambapo taarifa mjumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu aliyejiunga kwenye timu ya mafisadi amepewa shilingi milioni 5. Aidha, wajumbe hao wameahidiwa shilingi milioni tano nyingine ambazo wameahidiwa kupewa ikiwa watafanikiwa lengo lao hilo.
Baadhi ya wajumbe ambao wamepenyeza taarifa hizi wamedai kuwa wanachofanya akina Kingunge ni cha kipuuzi hasa baada ya Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa kuziba mianya yote ya mafisadi kumpitisha mtu wao. Kwamba Rais Kikwete anasimamia haki na wamempongeza kwa kusimamia misingi ya chama.
Wadau, hawa ndio mafisadi. Wameamua liwalo na liwe kuhakikisha kuwa fisadi lao linaenda Ikulu. Nawaomba Watanzania kusimama imara kupinga mkakati huu ovu ili chama chetu na nchi yetu isingie kwenye machafuko. Bahati nzuri wanaofanya vitendo hivi wanafahamika. Watambue kuwa kumchezea Mwenyekiti wa CCM ni kumchezea Mkuu wa nchi kwa vile Kikwete ana kofia mbili.
Kwa akili yako finyu, unadhani bila mgombea imara kutoka CCM, kuna ushindi? Huo ujinga, umaskini, maradhi..etc utapambana nao vipi? Hapa tunazungumzia uchaguzi.
Wamechelewa jamvini karamu imeshaliwa.
kumbe upo mbona upo kimya sana unaacha vijana wa lowasa wanamchezea jk?Wamechelewa jamvini karamu imeshaliwa.
......Zidumuuu fikira za mwenyekiti wa CCCMM.
kajipange story yako nzuri kusoma ila haina mashiko coz imekaa kisiada zaidi bila fact za maana wataje waliopewa tuwajue na sio waliotoa peke yao.
maana na wewe utakuwa vuvuzera tuu
Bado tu... Mweeeh! Ngoja nishushe chandarua. Alamsiki wadau, kesho panapo majaaliwa ya Mwenyezi Mungu...
mi naona bora hata angesema Ngereja au Muhongo.
Haya sasa jamani hatulali tunataka MKONO