Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Elections 2015 Yaliyojiri katika vikao vya CCM Dodoma - Julai 10-12, 2015. Magufuli achaguliwa kuwa mgombea Urais

Kingunge, Kone na Msindai wanaratibu mpango wa kumng'oa Mwenyekiti wa CCM,KIKWETE
Wadau amani iwe kwenu.


Taarifa nilizopata hivi punde kutoka Dodoma zinasema kuwa baada ya Team Lowasa, Friends of Lowasa na 4U MOVEMENT kubaini kuwa jitihada za mafisadi za kufanikisha Lowasa anaenda Magogoni zinagonga mwanba, mawakala wa mafisadi hao chini ya uratibu wa Kingunge Ngombale Mwiru na Mkuu wa Mkoa wa Singida, Parseko Kone wanaratibu mpango wa kumuondoa Madarakani Mwenyekiti wa CCM Taifa, Rais Jakaya Kikwete. Taarifa zinasema kuwa mawakala hao wa mafisadi wameshindwa kutekeleza mpango wao huo ndani ya kikao cha Kamati Kuu na sasa wanaelekeza nguvu zao kwenye Mkutano wa Halmashauri Kuu ambao utafanyika hivi punde.


Taarifa zinasema pia kuwa, Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Singida, Mgana Msindai naye amejiunga kwenye harakati hizo ili kuhakikisha kuwa kubwa la mafisadi nchini, Edward Lowasa linaenda Ikulu iwe kwa amani au kwa shari. Katika kuhakikisha kuwa lengo hilo linafanikiwa, muda mfupi uliopita Kingunge, Kone na Msindai wameonekana maeneo ya Chuo Kikuu cha St Gasper wakigawa fedha ambapo taarifa mjumbe wa Mkutano wa Halmashauri Kuu aliyejiunga kwenye timu ya mafisadi amepewa shilingi milioni 5. Aidha, wajumbe hao wameahidiwa shilingi milioni tano nyingine ambazo wameahidiwa kupewa ikiwa watafanikiwa lengo lao hilo.


Baadhi ya wajumbe ambao wamepenyeza taarifa hizi wamedai kuwa wanachofanya akina Kingunge ni cha kipuuzi hasa baada ya Mwenyekiti huyo wa CCM Taifa kuziba mianya yote ya mafisadi kumpitisha mtu wao. Kwamba Rais Kikwete anasimamia haki na wamempongeza kwa kusimamia misingi ya chama.


Wadau, hawa ndio mafisadi. Wameamua liwalo na liwe kuhakikisha kuwa fisadi lao linaenda Ikulu. Nawaomba Watanzania kusimama imara kupinga mkakati huu ovu ili chama chetu na nchi yetu isingie kwenye machafuko. Bahati nzuri wanaofanya vitendo hivi wanafahamika. Watambue kuwa kumchezea Mwenyekiti wa CCM ni kumchezea Mkuu wa nchi kwa vile Kikwete ana kofia mbili.
kajipange story yako nzuri kusoma ila haina mashiko coz imekaa kisiada zaidi bila fact za maana wataje waliopewa tuwajue na sio waliotoa peke yao.

maana na wewe utakuwa vuvuzera tuu
 
Kwa akili yako finyu, unadhani bila mgombea imara kutoka CCM, kuna ushindi? Huo ujinga, umaskini, maradhi..etc utapambana nao vipi? Hapa tunazungumzia uchaguzi.

Haya sasa jamani hatulali tunataka MKONO
 
Bado tu... Mweeeh! Ngoja nishushe chandarua. Alamsiki wadau, kesho panapo majaaliwa ya Mwenyezi Mungu...
 
Jamani watanzania wenzangu tusubiri tu watangaze achani kutoa taarifa za uongo bila evidence..
 
mpaka saa tano hakuna lolote. laleni, ccm wametuudhi bungeni, wasubiri uchaguzi tuwalipe malipo yao
 
Tetesi 5 bora ni hii hapa
1. Pinda
2. Bilal
3. Jaji Ramadhani
4. Membe
5. Asha Migiro
 
Haya sasa jamani hatulali tunataka MKONO

Nape atatangaza matokeo baada ya DAKU. ikifika asubuhi yatakuwa yamebaki majina 3. magazeti yatapata nafasi ya kuandika JINA MOJA Jumapili.... Hii ndio taiming ya kumchinja Lowassa bila kuwa na madhara ya kipropaganda za kina Kingunge. Wamebanwa kila kona. Hawafurukuti.....
Lowassa sasa wanamunywesha gulukosi....
 
Back
Top Bottom