Modestproposal
Senior Member
- Jan 6, 2022
- 127
- 228
Kwa majina yao au kwa idadi tu,kwamba watakuwa 20 au nazaidi?Orodha ya mashahidi lazima ijulikane wakati wa committal proceedings. Hawawezi kuleta Shahidi ambaye hayuko kwenye orodha bila kibali cha Mahakama.
Ni kweli. Siku za kiama kwa CCM zinajongea. Uongo na dhuruma huangamiza.Tunashukuru kwa juhudi zenu, kwa kutujuza yanao ajili uko japo ni aibu kwa nchi yetu pendwa lla hamna namna endeleeni tu.
kama mimi yaaniHizi siku mbili zilikuwa ngumu sana kwangu. Mawakili wa serikali walitukatili sana kutoleta mashahidi. Kufuatilia hii kesi inanikumbusha uhondo niliokuwa naupata enzi nikisoma novel za Willy Gamba.
Naweka kambi hapa kufuatilia michongo.
Mungu ibariki JF na mleta mchongo kwa updates zako zilizotukuka
Ziko karibuNi kweli. Siku za kiama kwa CCM zinajongea. Uongo na dhuruma huangamiza.
Kila mtu anashangaa hata Hakimu anashangaaJamani kila siku shaihidi ni Polisi anaelezea ukamataji hakuna raiya aliona uwo ugaidi.
Toka mashahidi waanze kutoa ushahidi wao wanaongelea ukamataji, uwekaji mahabusu, kuandika maelezo, kusafrisha washitakiwa, kuharibika kwa gari njiani, detention register,miala ya simu shs 500,000/- Kama fidia ya nauli n.k. Hakuna ushahidi unaotolewa unaoonyesha mwelekeo wa ugaidi, hata mashahidi muhimu kina Kingai, Mahita,Urio na huyu anayeendele hawaonyeshi. Sasa ugaidi utaelezwa lini na nani?Najiuliza: Kwa nini wanaleta mashahidi kama huyu? Alisema chochote kinachoweza kuthibitisha mashtaki? Nje ya kwamba aliambiwa Mbowe aliandaa Ugaidi?
UTI na tezi dume.Shahidi wa jana ilibidi aombe awe anatoka toka kwenda kwa short call na kuna wakati inaonesha aliomba tu ruhusa kabla Mh. Jaji hajamalizia kumjibu akawa ametoka mkuku!
Huyu n yule wa wakati ule hivi watakuwa na maradhi gani yanayowafanya wasiweze kustahimili kubana mkojo kizimbani mpaka wamalize. Wameshindwa kuiga mfano wa MaWakili ambao wao wakianza examination ni mpaka wanamaliza hamna kuomba ruhusa?
Lakini hata hivyo Acha ikae hivyo hivyo!