Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 3,984
- 13,760
HISTORIA
Mkoa wa Arusha ni moja kati ya Mikoa 26 ya Tanzania Bara, wenye ukubwa wa KM za mraba 34,515.5. Idadi ya watu kwa ongezeko la 2.7% kwa mwaka na inakadiriwa kufikia jumla ya watu wapatao 1,835,787 ambapo wanawake wakiwa sawa na 51.5% na wanaume 48.5%
Mkoa wa Arusha umepakana na Mkoa wa Manyara kwa upande wa Kusini, upande wa Mashariki umepakana na Mkoa wa Kilimanjaro, kwa upande wa Kaskazini umepakana na Nchi ya Kenya na kwa upande wa Magharibi umepakana na Mkoa wa Simiyu na Mara.
MUHTASARI WA MAENEO YA UTAWALA, MKOA WA ARUSHAKatika Mkoa wa Arusha, kuna mgawanyo wa kiutawala ambao unahusisha mamlaka za miji na wilaya. Mamlaka hizi zimegawanywa kulingana na idadi ya kata, mitaa, vijiji, na vitongoji vinavyopatikana ndani ya maeneo yao.
Chanzo: TAMISEMI
Mamlaka za Miji
Jiji la Arusha linajumuisha jumla ya kata 25 na mitaa 154. Hata hivyo, hakuna vijiji wala vitongoji ndani ya Jiji la Arusha, kwani linaendeshwa zaidi kwa mfumo wa mijini. Hii inaonyesha kuwa jiji hili ni kitovu cha mijini katika mkoa huu, bila kuwa na maeneo ya vijijini.
Mamlaka za Wilaya
Kwa upande wa wilaya za Mkoa wa Arusha, kuna mgawanyo wa utawala ambao unahusisha wilaya sita;
1. Wilaya ya Arusha ina kata 27, vijiji 67, na vitongoji 259.
2. Wilaya ya Karatu ina kata 14, vijiji 57, na vitongoji 262.
3. Wilaya ya Longido ina kata 18, vijiji 51, na vitongoji 176.
4. Wilaya ya Meru ina kata 26, vijiji 90, na vitongoji 330.
5. Wilaya ya Monduli ikiwa na kata 20, vijiji 62, na vitongoji 236.
6. Wilaya ya Ngorongoro ina kata 28, vijiji 65, na vitongoji 242.
Kwa ujumla, Mkoa wa Arusha una mamlaka za wilaya tano zenye jumla ya kata 133, vijiji 392, na vitongoji 1,505.
MAJIMBO YA KIUCHAGUZI
Katika muktadha wa kisiasa, Mkoa wa Arusha umegawanyika katika majimbo saba (7) ya uchaguzi, ambayo yana jukumu muhimu katika kuwakilisha maslahi ya wananchi katika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Majimbo haya ni yafuatavyo: Arusha Mjini, Longido, Karatu, Ngorongoro, Arumeru Mashariki, Arumeru Magharibi, Monduli.
SOMA PIA: Special Thread: Orodha ya Nyuzi za Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
HALI YA KISIASA
Mkoa wa Arusha ni moja kati ya mikoa muhimu ktoka kanda ya Kaskazini ambapo umekuwa ukitajwa kuwa ni kambi ya chama kikuu cha upinzani CHADEMA ambapo uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 CHADEMA waliambulia majimbo sita 6 kati ya saba 7.
Uchaguzi wa serikali za mitaa 2019 pamoja na uchaguzi mkuu 2020 ni moja ya sababu zinazoonesha kutaka kuzorotesha nguvu ya vyama vya upinzani katika mkoa wa Arusha kama ilivyokuwa katika mikoa mingine kwani mchakato wa uchaguzi huo uliwaondoa wagombea kwa kigezo cha kukosa sifa, na kupelekea baadhi ya vyama vya siasa kujitoa katika uchaguzi huo kwa kutokuwa huru na haki huku wagombea kutoka Chama Cha Mapinduzi CCM kupita bila kupingwa.
Uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 uliwaondosha wabunge wote kutoka CHADEMA bungeni, kwani uchaguzi huo uliwapa ushindi mkubwa wabunge wa chama tawala CCM katika mkoa huo.
Kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa 2024 na uchaguzi mkuu 2025 Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA mara kadhaa kimekuwa kikifanya mikutano ya hadhara katika mkoa wa Arusha ili kujiandaa kuelekea katika chaguzi hizo huku ukitegemewa kuwa uchaguzi wenye ushindani tofauti na ule wa 2019 na 2020.
YANAYOJIRI KUELEKEA NOVEMBA 27
- Kuelekea 2025 - Arusha: Benki yatoa pikipiki 20 kwa Jeshi la Polisi, RC Makonda awakabidhi
- Waziri Mchengerwa: Arusha Mlijichelewesha Wenyewe Kwa Siasa za Majitaka
- Arusha: Mrisho Gambo amuahidi Rais Samia kulinda mitaa kwenye Uchaguzi Wa Serikali Za Mitaa ili kutengeneza jeshi kwenye Uchaguzi Mkuu
- LGE2024 - Rais Samia Kuzindua Rasmi Zoezi la Kuandikisha Wapiga Kura wa Serikali za Mitaa
- CCM Arusha: Mgombea Serikali za Mitaa lazima awe na kazi ya kufanya inayomuingizia kipato halali la sivyo ataufanya Uenyekiti ndio kazi
- LIVE - Rais Samia anashiriki zoezi la Uandikishaji kwenye Daftari la Wapiga Kura kuelekea Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
- Kuelekea 2025 - Kwa tamko hili Makonda anahamasisha uvunjifu wa sheria barabarani na ongezeko la ajali
- Godbless Lema: Land Rover Festival ni mkakati wa watu wasijiandikishe
- Mkurugenzi Jiji la Arusha: CHADEMA wasilalamike mitandaoni uandikisha daftari la mpiga kura, walete malalamiko ofisi kwangu
- LGE2024 - News Alert: - Waziri Mchengerwa afafanua kuhusu mchakato wa Uchaguzi wa Serikali za Mtaa, leo Oktoba 15, 2024
- John Mrema: Watoto wanaotaka kujiandikisha waende na cheti cha kuzaliwa
- Karatu: Kijana Jasiri aibua Kashfa, Msimamizi wa kituo aondoka na daftari la wapiga kura ajaza majina kivyake!
- Arusha: CHADEMA yatangaza Maandamano kupinga Ukiukwaji wa Taratibu za Uandikishaji
- RC Makonda apiga chai na maandazi wakati akitoa wito kwa wananchi wa mkoa huo kujitokeza kujiandikisha kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa
- Arusha: Makonda awakumbusha wananchi umuhimu wa kujiandikisha. Asema kama hujajiandikisha hauna haki ya kulalamika
- LGE2024 - Waziri Mchengerwa: Jumla ya wapiga kura milioni 31, 282,331 wamejiandikisha kupiga kura Uchaguzi Serikali za Mitaa 2024
- Kuelekea 2025 - LGE2024 - Mahakama yaipa Ruhusa TAMISEMI kusimamia Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
- LGE2024 - Kura za maoni zazua 'mtiti' Unga Limited – Arusha, wengine watishia kutompa kura kada wao wa CCM
- Rais Samia ampa Sheikh wa Arusha Land Rover Discovery limsaidie kwenye shughuli za kidini. Hii si Rushwa kabisa?
- Makada wa CCM wajitupa chini watoa shutuma kwa wanaokata majina katika kura za maoni Arusha
- Msimamizi wa Uchaguzi Karatu: Hakuna wagombea waliolazimishwa kujitoa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa Karatu
- Arusha: Godbless Lema awatimua Maofisa wa TAKUKURU kwenye semina ya Wagombea wa CHADEMA, adai Wameacha uozo ufanywe kwenye Uandikishaji
- Mchengerwa: Wagombea ambao hawajaridhishwa na uteuzi, waweke pingamizi
- Arumeru: Wagombea wa ACT Wazalendo Kata ya Seela Sing’isi waenguliwa kwa kuto dhaminiwa na kutokujiandikisha orodha ya Wapiga Kura
- Arumeru: Inasemekana Kata ya Poli Mtendaji wa Kijiji kaogopa kubandika matokeo wa wagombea waliopita, wananchi wamefurika, polisi wa ghasia wafika
- Polisi: Kuna chama cha Siasa kinapanga kufanya Vurugu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
- Arusha: Wagombea 9 wa CCM waenguliwa kwenye mchakato wa Serikali za Mitaa kwa kukosa sifa
- CCM: TAMISEMI itambue demokrasia yetu ni changa, ipuuze makosa madogomadogo katika hatua ya rufaa uchaguzi Serikali za mitaa
- Arusha: TLP walia na wagombea wake kuenguliwa, wakata rufaa
- Arumeru: Wagombea CHADEMA Mbuguni waenguliwa, huenda wakasusa!
- Arusha: CHADEMA wachapana ngumi, Lawama kwa Lema
- LGE2024 - Wanachama wa CHADEMA Arusha waliodaiwa kupigana wamjibu Lema, "Lema amekuwa mtu wa sarakasi, anachukua watu vichochoroni"
- Makalla: Chagueni wagombea wa CCM wale wa CHADEMA Mbowe kasema hawana ILANI ni hatari kuwa na kiongozi bila kuwa na Mkataba wa atakufanyia nini
- Wanachama wa CHADEMA Arusha waliodaiwa kupigana wamjibu Lema, "Lema amekuwa mtu wa sarakasi, anachukua watu vichochoroni"
- Katibu mwenezi Arusha: Wao wanaokoteza wagombea, CCM ina demokrasia
- Godbless Lema: Mkishindwa kuwa na nidhamu hiki chama kitapotea
- Gambo aonya wenyeviti wa Serikali za mitaa kutumia mihuri ya serikali kujinufaisha
- Arusha: Aliyehamia CCM asema, wanaosema wagombea wa CHADEMA walienguliwa si kweli
- Godbless Lema: Viongozi wa CHADEMA Arusha wamenyimwa Viapo vya Mawakala siku moja kabla ya Uchaguzi
- Kituko: Aliyepitishwa Kugombea CHADEMA ahamia CCM
- Mawakala wa CHADEMA Arusha ngoma nzito, wadai kukosa fomu za kiapo
- Lema: Nina taarifa kuna kura zimeshapigwa, wanatafuta namna ya kuingiza kura feki
- Msimamizi Uchaguzi Arusha: CHADEMA walikosea, tukawaita kuwasaidia wakatugomea
- Arusha: Makonda apiga kura. Akataza kulinda kura, asema wasiingilie majukumu ya watu wengine, ni kazi ya mamlaka
- Mchengerwa: Matokeo ya uchaguzi kutangazwa ndani ya saa 72
- Arusha: Godbless Lema ameamua kususia na kujitenga kwenye Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa
- ARUSHA: Umati wa wananchi bado uko kwenye foleni ndefu katika kituo cha kupiga kura cha Polling Station
- Meru: CHADEMA Wadai kupata ushindi katikaa kijiji cha Nshupu
- ACT Wazalendo waelezea rafu walizokutana nazo katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa
- Arumeru Mashariki: Chama cha ACT Wazalendo chadai kushinda Wenyekiti Kata ya Leguriki
- Arusha: Godbless Lema ameamua kususia na kujitenga kwenye Uchaguzi wa Serikali Za Mitaa
- Arusha: CHADEMA wapinga matokeo uchaguzi serikali za mitaa
- Arusha: Mbunge Ole Shangai alivyokumbana na Wananchi Ngorongoro wakimtaka aondoke Kituo cha Kura Endulen
- Arusha: CCM yashinda Mitaa yote Minne ya Kata ya Osunyai Jr
- Arusha: CHADEMA wapinga matokeo uchaguzi serikali za mitaa
- LGE2024 - News Alert: - CCM yashinda 98.83% Wenyeviti Serikali za Mitaa