JamiiTalks Yaliyojiri kwenye Warsha ya Wadau wa TEHAMA iliyoandaliwa na Jamii Media na CIPESA

JamiiTalks Yaliyojiri kwenye Warsha ya Wadau wa TEHAMA iliyoandaliwa na Jamii Media na CIPESA

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
JAMII_-138.jpg

Wadau wa Warsha/Kongamano wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Bw. Maxence Melo

Hii ni warsha ya siku moja ambayo inawakutanisha wadau mbalimbali wa Teknolojia na mawasiliano-TEHAMA katika kujadili masuala mbali kuhusu sekta hii.

CMAC.jpg

Meneja Mikakati na Uendeshaji wa Jamii Media, Bi. Asha Abinallah(Wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Washiriki wa Warsha hiyo Carol Ndosi, Maria Sarungi(Moderator) na Catherinerose Barretto

Akiongea katika warsha hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Media, Maxence Melo amesisitiza kuwa tatizo kubwa katika nchi sio Jeshi la Polisi bali ni Sheria zinazosimamia Mitandao ya Kijamii.

Hivyo watu wasijikite katika kuwalaumu Polisi bali lengo kuu liwe katika kuziangalia Sheria zinazosimamia mitandao hiyo.

maxence_akiongea.jpg

Mkurugenzi wa JamiiMedia, ndugu Maxence Melo akichangia wakati wa warsha hiyo
Wananchi ndio haswa wanaopaswa kuitengeneza Serikali badala ya kuenenda kwa mujibu wa matakwa ya Serikali.

Tunahitaji kubadili namna Watu wa Serikali inafikiri wakati inapitisha Sheria zenye makosa. Raia wanapaswa kulinda.

JAMII_-105.jpg

Mdau wa Tehama akichangia
Erick Kabendera amewataka watumiaji wa mitandao ya kijamii(Watu wazima) kuwa mfano wa kuigwa kwa vijana kwa matumizi chanya ya mitandao.

JAMII_-117.jpg

Naye mwakilishi toka Kitengo cha Makosa ya Mtandao cha Jeshi la Polisi, Dawson Msongalani kwa nafasi yake amesema kuwa ni kweli kukosekana kwa kanuni za usimamizi wa Sheria ya [HASHTAG]#CyberCrimeLaw[/HASHTAG] ni changamoto kubwa! Na kwamba suala hilo linalifanyiwa kazi.

index.jpeg

Bw. Dawson Msongaleli(CyberCrime Depertment Tanzania)

Naye Dr. Wakabi kutoka CIPESA anasema Pale watumiaji wa mtandao wanapokuwa na uoga wa kutambuliwa, inazuia utumiaji mzuri.

Julieth Namfuka(CIPESA): Katiba ya Tanzania inatoa uhuru wa kujieleza bila kuingiliwa

Julieth Namfuka(CIPESA): Kuchuja taarifa kupitia miundombinu ya TEHAMA inakuwa sana katika nchi za kiafrika.

Erick Kabendera: Watu wanahisi mazungumzo yao yanasikilizwa; hii inaturudisha nyuma kama nchi

Erick Kabendera: Suala la watu kukamatwa kwa ajili ya kujieleza na kutoa maoni yao linaturusha sana nyuma.

Pascal Mayalla amelezea jinsi ambavyo amekuwa akitumia huduma ya JamiiForums kwa takribani miaka 11 hadi sasa.

Erick Kabendera: Serikali itumie mitandao ya kijamii kama JamiiForums kupata maoni ya wananchi wake.

CarolNdosi: Kumekuwa na changamoto ya kupata taarifa serikalini kwa ajili ya kushughulika matatizo ya jamii

carol_ndosi_panelist.jpg

Bi. Carol Ndosi siku ya Warsha ya Jamii Media/CIPESA jijini Dar

Wakili msomi, Jebra Kambole akiongelea changamoto zilizopo kufuatilia Sheria zilizopo na uhuru wa kujieleza nchini Tanzania.

Wakili James Marenga: Sheria hutengenezwa/tungwa kwa ajili ya watawala, huo ndio ukweli wenyewe! Anasisitiza kanuni ni muhimu

Wakili Jebra: Lengo la kupitisha #CyberCrimeLaw kwa hati ya dharura halijawa wazi. Ni 2% ya watanzania wanaoijua sheria yenyewe!

Chambi Chachage kutoka @Udadisi: Watu wengi wanaandika maudhui mazuri wanapotumia utambulisho usiojulikana mtandaoni

->Kwa maudhui ya mtandaoni inabidi tujikite zaidi na ujumbe kuliko mwandishi wa huo ujumbe.
->Nimekuwa mtumiaji wa mtandao wa Jamiiforums kwa miaka kumi sasa, najua jinsi usiri ulivyo muhimu.

Wakili Jeremiah Mtobesya: Nimesimamia kesi nyingi za Makosa ya Mtandao na EPOCA na nimebaini nyingi zina msukumo wa kisiasa

group_selfie_jamiiforums.jpg

Wadau wa kongamano wakichukua picha ya pamoja (selfie) na Mkurugenzi wa Jamii Media, Bw. Maxence

YAZ.jpg

Meneja Mikakati na Uendeshaji wa Jamii Media, Bi. Asha Abinallah(Wa pili kulia) akiwa kwenye picha ya pamoja na Wafanyakazi wa Jamii Media katika Warsha ya Jamii Media/CIPESA

==========​

Kampuni ya Jamii Media ya Tanzania inayoendesha mitandao ya JamiiForums na FikraPevu kwa kushirikiana na CIPESA(The Collaboration on International ICT Policy in East and Southern Africa) iliyo na makao makuu yake nchini Uganda imefanya Kongamano la kuwakutanisha wadau wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (ICT) nchini hasa wanaohusika moja kwa moja katika kulinda faragha za wateja wao ili kujadili masuala mbalimbali ya Huduma za Habari na Mawasiliano katika jukumu lao kuwa kiunganishi kati ya mteja na huduma watoazo pamoja na namna ya kulinda usiri wa taarifa za wateja wanaotumia huduma hizo.

Kabla ya kufanyika kwa Kongamano hilo siku ya Jumatano tarehe 12 Julai, Jamii Media ilifanya mafunzo ya siku mbili kuanzia tarehe 10 hadi 11 Julai kwa vijana mbalimbali wakiwemo wanasheria, wanaharakati na wadau wa Teknolojia ya Habari na Mawasiliano. Mafunzo hayo yalilenga kujenga uelewa kuhusu sera zinazohusu Teknolojia ya Habari na Mawasiliano, Usalama wa Data Mtandaoni, Hali ya Uhuru Mitandaoni na Mambo yanayoathiri uhuru Mitandaoni nchini Tanzania.

Katika Kongamano hilo, Mwakilishi wa Jeshi la Polisi Tanzania, Dawson Msongaleli kutoka kitengo cha Makosa ya Mtandaoni alifanya pia Uwasilishaji kuhusu Sheria ya Makosa Mtandaoni na kueleza kuwa Usiri na Usalama wa taarifa za watumiaji wa mtandao ni vitu viwili vinavyokanganya na kwamba inafika wakati ili kutekeleza kimoja inabidi misingi ya kingine ivunjwe.

Aidha, alibainisha kuwa kukosekana kwa kanuni za usimamizi wa Sheria ya Makosa ya Mtandao (The Cyber Crimes Act, 2015) ni changamoto kubwa kwani inapelekea tafsri ya Sheria hiyo kubadilika kulingana na mazingira na mtu anayetafsiri kitu ambacho kinaathiri kazi yao kama watekelezaji wa Sheria na kuahidi kuwa mamlaka zinashughulikia chamgamoto hiyo.

Mara baada ya kumalizika kwa kongamano hilo, Mkurugenzi wa Jamii Media, Bw. Maxence Melo alisema hili ni Kongamano la kwanza la aina hii kufanyika tangu kuanzishwa kwa JamiiForums miaka 11 iliyopita na limekuwa na matokeo chanya baada ya wadau kujadili kwa kina masuala mbalimbali yahusuyo usalama wa watumiaji. Aliongeza kuwa wadau wengi kwenye kongamano hilo wameunga mkono hatua ya uwekaji wa sheria za kusimamia huduma nzima ya matumizi ya mitandao lakini wakashauri ufanywe kwa kutoa fursa za maendeleo na si kuminya ubunifu wala uhuru na usiri wa watumiaji wa huduma hizo.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa kampuni yake itaendelea kutoa mafunzo kwa wadau mbalimbali wa huduma za mawasiliano wakiwemo wamiliki wa blogu na watumiaji wa kawaida wa mitandaonya kijamii ili kuhakikisha wanakuwa na matumizi mazuri ya huduma hiyo ili kupunguza mkanganyiko kwao na kuwapa fursa adhimu ya kunufaika na uwepo wa mitandao hiyo.
 
mbona mm hawajaniita kabisa hapo kwenye mjadala nami nikatoa yangu machache
 
Wakuu,

Nilibahatika kufuatilia kikao hicho kwenye mtandao wa Twitter, ulikuwa ni wenye kuhabarisha sana na ulikuwa shirikishi. Nilitamani kushiriki lakini sikujua utaratibu wa mwaliko ulikuwaje. Wakati mwingine tupo tunaopenda kushiriki na kuchangia kwenye mijadala kama hiyo.

Kaka ...
 
Replies Chache lakini post ipo kwenye post zinazotrend🙂
Kweli wahenga walisema ukubwa ni dawa..*Just kidding )
 
Replies Chache lakini post ipo kwenye post zinazotrend🙂
Kweli wahenga walisema ukubwa ni dawa..*Just kidding )
Negative news sells!

Hii lazima ipate wachangiaji wachache kutokana na heading ya thread ilivyo.Ukianza na heading "Njoo tupeane maujanja" vijana kibao lazima washushe comment si chini ya mia.

Back to the topic, warsha ilikuwa nzuri na wamezungumza masuala ya msingi.

Big up sana kwa washiriki.
 
Jamii forums wangefungua milango kwa uhuru wa kutoa maoni kwa vijana kuhusu changamoto za maisha na strategies kuwasaidia kujikwamua kifikra dhidi ya utegemezi wa ajira, na kuongeza kipato,..

Isiishie hapa tu, Bali itengeneze mchanganuo mkubwa zaidi wa kusaidia vijana kwa nfano south Korea kabla ya viwanda walianzisha mchanganuo wa kutoa capital kwa vijana kwa masharti nafuu kwa kuendeleza viwanda,..

Ipatikane jukwaa ambapo vijana washirikishwe kujadili mfumo mzima wa rasilimali watu, pamoja na ubunifu wa bidhaa,.. Halafu serikali itumike kama garentor kuwasaidia kupata mikopo ya masharti nafuu kuendeleza viwanda vidogo vidogo, lakin sio kuwaacha tu wakikata tamaa, kama tatizo ni mitaji basi Ilo litatuliwe kwa njia hiyo
 
Back
Top Bottom