Kiongozi naimani uko salama,
Yes, niko ok
naomba niulize maana nimefwatilia hii kesi leo japo kwa twitter ila kuna jambo sijaelewa...
Bila shaka, nitakujibu kwa kadiri ya uelewa wangu...
Kwann mawakili (hasa wakili wa shahidi mr kiwelo) baada ya kujua kwamba hii ni very critical issue kwann hakusaini mwenyewe barua? Au ni nini alikwepa kusaini mwenye mpaka akamuachia mr kibatala?
Kama unakumbuka, Adv. Kihwelu ameshalitetea hili kwa kusema;
1. Toka mwanzo kule mahakama ya Kisutu wakati wa committal proceedings, Kibatala ndiye alikuwa wakili wa washitakiwa wote watatu
2. Hata sasa katika steji hii, mkuu wa jopo la mawakili wa utetezi ni Peter Kibatala na si kosa barua hiyo kusainiwa na yeye..
3. By the way, wameombwa sheria inayokataza hilo, wameshindwa kuitoa ama japo kunukuu kifungu cha sheria..
Maana nikijaribu angalia mawakili wa serikali wanakomaa na hii issue!
Ofcoz, ni lazima wakomae na hilo kwa sababu kama nilivyosema mwanzo, that, THEY WERE CAUGHT BY SURPRISE....
Hawakutegemea "counter attack" hatari na matata kwao kama hii ambayo inaweza kugeuza mambo mengi kuwa against them...!
And you know what?
Hiyo barua ikikubaliwa na kupokelewa tu kuwa kielelezo cha ushahidi upande wa utetezi, tutashuhudia bonge la U - TURN ktk kesi hii...!
Nadhani maelezo hayo juu, yanaweza kukupa ufahamu kiasi fulani...
NB: naona leo mawakili wa serikali walikua wanatumia kila ku provoke mawakili wa utetezi kisaikolojia...
Yes, na provocation dhidi ya wenzao ni kwa sababu hizi;
1. Just, ku - panic kwa sababu hatua waliyoichukua upande wa utetezi kupitia kwa mshitakiwa wa pili Mohamedi Abdilah Ling'wenya baada ya kupendelewa ktk mapingamizi yaliyokwisha kutolewa maamuzi, hawakuitegemea na ina threaten kuwatupa nje na kudhihirisha hila na uongo wa ushahidi wao na mashitaka kwa ujumla...
2. "Umafia" wanaoutumia kujipatia nyaraka fulani fulani bila kufuata sheria tena zingine mahakama ikiwa ndiyo custodian wake, imewashitua na kuwashangaza na kuleta panic upande wa Jamhuri hata kujiuliza wamewezaje kupata akili hii...
Hili hata Judge linampa wakati mgumu. Ameingia ktk mtego ambao ili ajinasue ni lazima ajichanganye tu. Na akijichanganya tu atawapa upenyo upande Wa utetezi kupiga nyundo....!!!
3. Wala usiwe na shaka, mtu yeyote anayeshindwa kutetea hoja na akaanza kum - provoke mwenzake, basi tambua kuwa ameshashindwa...
Hawa Jamhuri na Polisi wao, UONGO wao utawekwa wazi zaidi na zaidi very soon...