Pep
JF-Expert Member
- Jul 29, 2015
- 2,338
- 5,488
Dah 🤣🤣🤣Mbona huyu swila sijui swala
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dah 🤣🤣🤣Mbona huyu swila sijui swala
Umeonaeeeeee! Hii ni mojawapo ya ng'ombe. Hivi mtu na akili zako unayefuatilia kesi hii unaona kabisa tangu mwanzo mashahidi muhimu hawagusi ugaidi, halafu anatokea mtu anaandika uharo namna hii!Usijitese kuumiza kichwa chako. Hii nchi ina ng'ombe wengi, ukilinganisha na binadamu wachache wenye akili na utashi wa kufikiri.
Loo! Think tank uharo namna hii?Ndio think tank ya uvccm hiyo, tumuhurumie tu.
LABDA walioteshwa kinabii kuwa huko mbele atakuja informer na taarifa hizo fungueni jalada!Kesi ya kikomedi kweli yan mnafungua kesi wakati informer urio hajaanza kazi ,
endelea kujitoa ufahamu utatuambia alipo ndugailengo la mboe lilikuwa ni kununua mtu yeyote yule ambaye alikuwa tayari kufuata maelekezo yake ambayo ni, kuvuruga amani na utulivu wa nchi.
alikuwa anakusanya vijana wa kihuni na wasaliti na kuwajasirisha kutenda vitendo vya kigaidi/kihalifu dhidi ya nchi yao.
mboe alikuwa na aliunda genge la kigaidi kwa kuwatumia hao makomandoo na wahalifu wengine mbalimbali kama vile, majambazi, wauza madawa ya kulevya, wavuta bangi n.k.
huyo jamaa hakuwa mwanasiasa bali muhalifu mbobezi aliye jificha kwenye uongozi wa chama cha siasa.
ni mtu ambaye hakujali amani na utulivu wa nchi....ni msaliti aliye isaliti nchi yake kwa tamaa na uchu wake wa kijinga.
KimeumanaHabari Wakuu,
Leo 08/ 02/ 2022 shahidi wa 13 anatarajiwa kuendelea kutoa ushahidi wake kwenye kesi inayomkabili Mbowe na wenzake 3.
Kujua Kesi ilipoishia fungua kiungo hiki: Yaliyojiri Mahakamani kesi ya Mbowe na wenzake: Shahidi wa 13, Tumaini Sostenes Swila kuendelea kutoa ushahidi wake Februari 08/2022
Baki nami.
Updates:
Jaji ameingia Mahakamani
Kesi namba 16 ya Mwaka 2021 Jamuhuri Dhidi ya Khalfani Bwire, Adam Kasekwa, Mohammed Ling'wenya na Freeman Mbowe inatajwa hapa Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Ikupendeze Mheshimiwa Jaji naitwa Robert Kidando nipo pamoja na wakili
Mawakili Wa Serikali Waandamizi Na Tulimanywa Majige, Wakili wa Serikali
- Pius Hilla
- Abdallah Chavula
- Jenitreza Kitali
- Nassoro Katuga
- Esther Martin
- Ignasi Mwinuka
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ikupendeza naitwa Peter Kibatala nipo Pamoja na wakili
Wakili Nashon Nkungu amepata Emergency Kidogo yupo karibu sana kufika
- Sisty Aloyce
- Iddi Msawanga
- Maria Mushi
- Kadija Aron
- Lusako Mwaiseke
- Fredrick Kihwelo
Jaji: Kabla hatuja endelea Wasiliana naye tujue yupo Wapi
Wakili Peter Kibatala: Sawa Mheshimiwa Jaji
(Anatoka Nje kwenda Kupiga Simu)
Mahakama itasubiri Kidogo, Ukimya Umetawala Wanaingia
Kwa Pamoja sasa Wakili Dickson Matata na Wakili Nashon Nkungu
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji naomba Sasa nimtambulishe Wakili Nashon Nkungu,
Nashon Nkungu: Samahani sana nimechelewa Sababu ya Usafiri
Jaji anaita Washtakiwa Wote wanne na wote wanaitika wapo Mahakamani
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Shauri limekuja kwa ajili ya Kuendelea Kusikilizwa, Tupo tayari Kuendelea
Wakili Peter Kibatala: Mheshimiwa Jaji nasi pia tupo tayari Kuendelea
Jaji: Shahidi nakukumbusha Ulikuwa chini ya Kiapo na Utaendelea Kuwa Chini ya Kiapo
Jaji: nakualika Wakili Fredrick Kihwelo
Kiwhelo: shahidi Salaam
Shahidi: Salaam
Kiwhelo: Kwa Mujibu Wa Ushahidi Wako Ulisema Ulipeleka simu Nane
Shahidi: Sahihi
Kiwhelo: nakukumbusha Namba za Simu ulizotaja hapa Mahakamani 0719933386 na 0784779944
Shahidi: Sahihi
Kiwhelo: shahidi Ukienda Dukani Kununua Simu, Je ndani Kuna Kuwa na Line
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: kwa hiyo Simu na Line ni Vitu Viwili tofauti
Shahidi: Sahihi
Kiwhelo: Mwambie Jaji ilikiwa Simu 8 ambazo ziliwasilishwa Mahakamani Kama Vielelezo, na Kama line za Simu 8 ziliwasilishwa kama Vielelezo
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Mkumbushe Mheshimiwa Jaji ni Vielelezo namba Ngapi, hizo Line 8
Shahidi: Line Za Simu zipo ndani ya Simu Zenyewe
Kiwhelo: Tumeshakubaliana Kuwa Line na Simu no Vitu Viwili tofauti, Sasa nataka Kujua Line 08 ni Kielelezo namba Ngapi
Shahidi: Hapana ziliwasilishwa Simu tuh, Line zipo ndani
Kiwhelo: Unajua Kuwa IMEI Namba haionyeshi line Bali Umiliki Wa simu
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Unafahamu Kuwa namna pekee ya Kuonyesha Umiliki Wa Line ni Kuleta Namba IMCI
Shahidi: Siyo sahihi
Kiwhelo: Unafahamu Kwamba namba ya IMCI ni tofauti na namba za simu
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: Unaweza Kumwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mmeleta namba za IMCI za line hapa Mahakamani.?
Shahidi: Siwezi kulijibia hilo
Kiwhelo: Kwenye Maelezo Yako Ulisema Mwezi January 2020 Ulipata Uhamishoni Wa Muda Kwenda Makao Makuu Ndogo Dar es Salaam
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Ni sahihi Mwezi August 2021 ulirudi Katika Kituo chako Cha Kazi TEMEKE
Shahidi: sahihi
Kiwhelo: Uhamisho Wako Ulikuwa wa Muda gani
Shahidi: Mwaka Mmoja Kiwhelo: Unaweza Kumwambia Mheshimiwa Jaji Suala la Uhamishoni ni Mchakato au Tukio
Shahidi: Ni taratibu za Kazi
Kiwhelo: Twende Kwenye taratibu za Kazi, Wakati wa Mahojiano Yako Uliaambia Mahakama hii Kuwa Wakati wa Uhamishoni Ulipitia taratibu Mbalimbali
Shahidi: Ndiyo nilieleza
Kiwhelo: Shahidi nitakuwa Sahihi Nikisema Dalili zote zinasema Kwamba Uhamisho wako Ulikuwa wa Kimkakati na Ulihusu Shauri hili
Shahidi: Si Kweli
Kiwhelo: Wakati wa Mahojiano Ulisema Taarifa za Matendo Ya Kihalifu zilipokelewa na DCI ROBERT BOAZ
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Na Vitendo hivyo Vilikuwa vinahusu uchomaji Masoko
Shahidi: Ndiyo na Matukio Mengine
Kiwhelo: Kukata Miti Barabarani?
Shahidi: Ndiyo na Matukio Mengine
Kiwhelo: na Maandamano?
Shahidi: Ndiyo na matukio Mengine
Kiwhelo: Orodha hiyo Kuna Ugaidi Shahidi Ndiyo upo
Kiwhelo: Ulisema Kuna Viongoz walitaka kudhuliwa, Je Unaweza Kumkumbusha Mheshimiwa Jaji Majina ya hao Viongozi
Shahidi: Lengai Ole Sabaya
Kiwhelo: Mtaje Mwingine
Shahidi: Mwingine Simfahamu
Kiwhelo: Kwahiyo Ulikuwa Unaandika Usichokifahamu
Shahidi: Namjua huyo tu
Kiwhelo: Mtuhumiwa Wa Kwanza hadi wa Nne, Waliandaa Vipi Maandamano
Shahidi: Wanajua Watuhumiwa
Kiwhelo: Wewe Unafahamu Vipi Kwamba Walipanga Maandamano
Shahidi: Wanajua Watuhumiwa
Kiwhelo: Kwani Maandamano ni Kosa
Shahidi: Siyo Kosa Kama Ulifuata Sheria
Kiwhelo: Kwani Walikuwa wameshaandamana au Walikuwa wanapanga kuandamana?
Shahidi: Walikuwa wanapanga
Kiwhelo: Ulijuaje Kama hawato omba Kibali
Shahidi: Hilo siwezi kulijibu
Kiwhelo: Ni sahihi Kwamba Tarehe 18 July 2020 ulifungua Jalada la Kesi ya Kula Njama ya Kutenda Matendo Ya Ugaidi
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Ni sahihi Kwamba Maelekezo hayo Ulipewa na ACP KINGAI
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: nitakuwa Sahihi Nikisema Kwamba Mtu Mmoja anaweza Kuamua ufunguliwe Kosa la Namna gani
Shahidi: Siyo Sahihi
Kiwhelo: Wakati una elekezwa na Ramadhan Kingai Kufungua Shauri hili ulikuwa Umepewa Jukumu la kuwa Mshairi Wake
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Kwani alikwambia Fungua Shauri hili au Mlijadiliana Kwamba Kwa Mujibu wa Ushahidi Huu tufungue Shauri hilo
Shahidi: Ailinielekeza
Kiwhelo: Kwani alikwambia amejadiliana na nani Kwamba Wameona inafaa Kosa la Ugaidi lifunguliwe
Shahidi: Hakuniambia
Kiwhelo: Kwa hiyo ni sahihi Kwamba Ramadhan Kingai ndiye aliye taka Shauri hilo lifunguliwe
Shahidi: Siwezi Kujibu hilo
Kiwhelo: Ni sahihi Kwamba wewe ndiyo Ulipokea Simu Kutoka Kwa DC Goodluck zilizo toka Moshi
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Unaweza Kueleza Mahakama Taratibu za Makabidhiano
Shahidi: alini kabidhi zikiwa zimeandikwa PF 145 Nikaenda Kuzi hifadhi katika Kabati la Chuma
Kiwhelo: Ni sahihi pia Kuwa Ramadhan Kingai Alimuamuru DC Goodluck akukabidhi Simu za Khalfani Bwire
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Ni kweli pia Simu za Luten Denis Urio Ulikabidhiwa kwa Hati ya Makabidhiano
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: na Hati ya Makabidhiano hiyo ipo Mahakamani hapa
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Ni sahihi pia unawasilisha Mahakamani Hati ya Makabidhiano ya Simu za Khalfani Bwire
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: kwa Mujibu wa Maelezo Yako, Ulipokea Taarifa za Uchunguzi wa Simu Kutoka Kwa Inspector Innocent Ndowo
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: na Ulipokea Taarifa hiyo kwa Kusaini Kitabu cha Makabidhiano
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Unaweza Kumwambia Mheshimiwa Jaji ikiwa Umekiwasilisha Mahakamani hapa Kitabu hicho
Shahidi: Sijawasilisha
Kiwhelo: Ni sahihi pia Ulipokea Simu Nane Kutoka Kwa Inspector Innocent Ndowo
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Ni kweli pia Unawasilisha Hati ya Makabidhiano Baina yako na Inspector Innocent Ndowo
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: kwa Mujibu Wa Maelezo Yako Unasema Kuwa Mheshimiwa Freeman Mbowe alikuwa akiwawezesha Watuhumiwa Kwa Fedha na Huduma Mbalimbali
Shahidi: Ni sahihi
Kiwhelo: Tuambie Huduma Mbalimbali ni zipi
Shahidi: Mtuhumiwa Freeman Mbowe ndiye aliyekuwa anawasafirisha, Kuwapatia Maradhi, huko walipokuwa Wanafika Moshi
Kiwhelo: Katika Maelezo Yako Unasema Kuwa Uchunguzi wa Cyber Unaonyesha Mheshimiwa Freeman Mbowe alikuwa anawaelekeza Watuhumiwa nini cha Kufanya, Je ni wapi tutaona hayo Maelekezo
Shahidi: Kwenye Maelezo ya Onyo ya Mshitakiwa
Kiwhelo: Ni sahihi Kwamba Jina la Mheshimiwa Mbowe halikuandikwa Katika Jalada la Kesi, Kwa sababu Kama Mngeandika angejua
Shahidi: Ni sahihi Kiwhelo: na Kama angejua angesitisha Mipango hiyo
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Kwani Shahidi Mtu akiwa anataka Kutenda Uhalifu, alafu akasitisha Kuna Tatizo
Shahidi: Hakuna Ila angeweza Kubadili Njia ya Kutenda uhalifu
Kiwhelo: Kwani Mheshimiwa Mbowe ana Mtoto Polisi
Shahidi: Hapana
Kiwhelo: Kwani ana Ndugu Jeshi la Polisi
Shahidi: Sifahamu
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kwa namna gani Taarifa zingemfikia Mheshimiwa Mbowe
Shahidi: Kwa Kubadilishana Taarifa siyo Kwamba watavujisha
Kiwhelo: ni Kawaida Kwa Jeshi la Polisi Kuficha Majina ya Watuhumiwa
Shahidi: Ndiyo ni Kawaida
Kiwhelo: Ni Matukio gani Mengine ambayo Jeshi la Polisi Wanaficha Majina ya Watuhumiwa
Shahidi: Siwezi Kuongelea hapa
Kiwhelo: ila umesema ni Kawaida Yenu Kuficha Majina ya Watuhumiwa
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Ulisema Unafanya kazi Kitengo X
Shahidi: Ndiyo
Kiwhelo: Kwani Shahidi Kuna Makosa Mengine Makubwa ambayo unaona ni Hatarishi Kuya sema hapa
Shahidi: Yapo
Kiwhelo: Tuambie ni Mambo yapi zaidi ya haya Wanayoshtakiwa
Shahidi: Siwezi Kuya sema hapa
Kiwhelo: Mwambie Mheshimiwa Jaji basi Kama hutaki Kutuambia sisi
Shahidi: Siwezi Kusema hapa
Kiwhelo: Ulisema Kwamba Baada ya Kingai Kukupigia Mkutane Polisi Central, Ulisema huluwaona Watuhumiwa ni sahihi
Shahidi: Ni sahihi, ila nilijua Wapo Central
Kiwhelo: Shahidi Katika Jalada ambalo Jina limefichwa, Nani alikuwa Mtuhumiwa
Shahidi: Freeman Aikael Mbowe
Kiwhelo: Jina lake lilikwepo kwenye Jalada?
Shahidi: Hapana, ila Mtuhumiwa ni Mbowe
Kiwhelo: Katika Maelezo Yako Ya Ushahidi Wako, Unasema Watuhumiwa Wamekiri Makosa yao
Shahidi: Ni sahihi, Baada ya Kusoma Maelezo Yao
Kiwhelo: Na Ulipo wapelekea Karatasi Nane, Walikula Talia kuwa ile Michoro na Maandishi siyo Ya kwetu
Shahidi: Ni sahihi Walikataa
Kiwhelo: Mtu aliyekiri anawezaje Kukataa wakati Wa Sampuli
Shahidi: Inategemea
Kiwhelo: Kwahiyo Katika Maandishi Yao Walikiri au Walikataa?
Shahidi: Mshitakiwa Wa kwanza alikataa, lakini baada ya Sampuli zake kwenda Kwa Mchunguzi Majibu ya Kawa ni Yeye
Kiwhelo: Asante Mheshimiwa Jaji, Ya Kwangu ni hayo tuh
Kibatala: Shahidi Tumeshawahi Kukutana Mimi na wewe Kwa Mara ya Kwanza Leo au Tumeshawahi Kufanya kazi pamoja
Shahidi: Sikumbuki Peter
Kibatala: Hakuna zoezi lolote la Kisheria tulifanya na wewe, Siyo Kwenye hii Kesi, Kuhusiana na Uchukuaji wa Vielelezo
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Wacha tuendelee, Shahidi Unakumbuka Wakati unazungumzia Kuhusu Kidaftari nilisimama Kwamba Mnafanya Zoezi siyo la Umuhimu sana, Baadae tukaambiwa tuache Muendelee
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Kwenye Process ya Kuku Sanya Data na Sample, Zilikuwa Processed na Baadae zikaenda kwa Expert
Shahidi: Siyo Mimi, Kidaftari kilikamatwa na Mtu Mwingine
Kibatala: Ni kweli Kwamba Sampuli za Mwandiko ulizo chukua ndiyo zilipelekwa kwa ajili ya Uchunguzi
Shahidi: Ni kweli Mimi ndiye niliye chukua Sampuli
Kibatala: Ulichukua Sampuli Kwa Maelekezo Ya Musa Nankaa au Maelekezo ya Ramadhan Kingai
Shahidi: Kwa Maelekezo ya Ramadhan Kingai
Kibatala: Unafahamu Kazi ya Kuchukua Sampuli ni Kazi ya Kisayansi
Shahidi: Ndiyo nafahamu
Kibatala: Umesomea Mchakato Wa Uchukuaji Sampuli
Shahidi: Nimesomea Kibatala Wapi?
Shahidi: Chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es Salaam
Kibatala: Kozi inaitwaje
Shahidi: DEVICE ID COURSE
Kibatala: Ilikuwa Module au ilikuwa ni Main Component
Shahidi: Mimi siyo Mchunguzi
Kibatala: Ndiyo Swali langu hapo sasa, Wewe ni Mtaalamu?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Mimi Nimesomea Mambo ya Account for lawyers ila siwezi kujiita Mhasibu, Je Wewe ni Mtaalamu Shahidi: Siyo Mtaalam ila nimesomea
Kibatala: Unajua Maanaa ya Exemplar
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Maana ya Requested writing Sample au Requestes Exaplar
Shahidi: Fafanua hapo
Kibatala: Ni fafanue nini wakati hizo ni Terms za Kisayansi
Shahidi: Sifahamu
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji sisi tunaona ni Haki Shahidi akiomba Ufafanuzi, Shahidi apewe Ufafanuzi, Tunaona ni Haki
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Hakuna shida, Mbeleni akitaka nimfafanulie nitafanya
Kibatala: Wewe Kwa kuwa Unasema Kwamba umefundishwa namna ya Kuchukua Sample, Je unafahamu Kwamba Ikitokea Ubishani Juu ya Saini yangu, Moja ya Njia Moja wapo ni Kuniambia nilete Nyaraka zingine Zenye sahihi yangu hiyo ndiyo inaitwa Requested Exemplar
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Wakati Unachukua Sampuli kwa Khalfani Bwire, Ulikuwa unafahamu hilo
Shahidi: Nilikuwa nafahamu
Kibatala: Lakini nyie Mlichukua Requested Sample
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Kama Ulimwambia Kwamba Pamoja na Sampuli zile Nane Mlichukua Nyaraka zingine za Khalfani Bwire
Shahidi: Nilisema
Kibatala: Mlichukua nini? Kitambulisho
Shahidi: Notebook
Kibatala: Kingai alikuwa anajua Kuhusu hiyo Notebook?
Shahidi: nataka Kufafanua
Kibatala: Sitaki Ufafanuzi, Jibu swali
Shahidi: alikuwa hafahamu
Kibatala: Je unafahamu a kwamba hiyo Notebook ni Mali ya Mtuhumiwa
Shahidi: Siyo Mali ya Mtuhumiwa
Kibatala: Hiyo Notebook alikamatwa nayo Nyumbani au Ulimkuta nayo Kituoni
Shahidi: Ninachofahamu ni kwamba Wali chukua Nyumbani Kwa Khalfani Bwire
Kibatala: Na nani alikukabidhi
Shahidi: Sarjent Johnson
Kibatala: Nikienda Katika Maelezo Ya Sarjent Johnson Nitaona kqambaalikikabi Notebook
Shahidi: Ndiyo Kibatala: Na Mlikabidhiana Kwa Utaratibu Upi
Shahidi: Wa Kipolisi
Kibatala: Na Hiyo Nyaraka ambayo Mlikabidhiana hiyo Diary, Ni Muhimu sana Kama Mtaleta hiyo Nyaraka
Wakili wa Serikali Pius Hilla: Mheshimiwa Jaji, Tutumie Neno Notebook kuepuka Confusion
Kibatala: Sawa, I apologize, Tutumie neno Notebook
Kibatala: Ni Nyaraka gani Ulionyesha Hapa Mahakamani Kwamba Mlikabidhiana
Shahidi: Sijaonyesha Mahakamani
Kibatala: Wakati Unamkabidhi Mtaalamu Wa Maandishi hiyo Notebook Ulimkabidhi kienyeji au Kwa Maandishi ya Kipolisi
Shahidi: Kwa Maandishi
Kibatala: Maandishi yapi, Mwambie Mheshimiwa Jaji
Shahidi: Barua na Dispatch Book
Kibatala: Umetoa hapa Mahakamani hiyo Dispatch
Shahidi: Sijaonyesha
Kibatala: Umetoa Mahakamani hiyo Barua
Shahidi: Sijaonyesha
Kibatala: Turudi tena Katika Sampuli, Je unafahamu a kwamba Unapo chukua Sampuli Unatakiwa uchukue Sampuli katika Mazingira ambayo ni Strictly controlled Environment
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je, hayo Mazingira Uliyo yachukulia hizo Sampuli ni Strictly controlled Environment
https://twitter.com/IAMartin_
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Unafahamu Kwamba ili Ku Create Controlled Environment, ulitakiwa Umpeleke sehemu Nyingine
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Wewe Ulifanya hivyo
Shahidi: Ndiyo nilimuhamisha Kutoka Kituoni Kwemda Jengo la RCO
Kibatala: Majengo ya pale tunayafahamu Wote, Je zinafika Mita 100
Shahidi: Hapana
Kibatala: Unafahamu a kwamba Mwandiko Wa Mtu unaweza Kubadirika Kutiana na Other factors Kama Psychology
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu kwamba Ulichukua Mwandiko wa Mtu ambaye amefiwa na Mzazi unaweza Kuwa tofauti
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Mtu akipigwa na Kufungwa Pingu Mwandiko unakuwa tofauti
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Waandishi Wa Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi
Shahidi: Simfahamu yeyote
Kibatala: Unamfahamu Mwandishi Wa Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi anaitwa Garry Breath
Shahidi: Simfahamu
Kibatala: Garry Breath anashauri Kuwa Unapo chukua Sampuli za Maandishi Za Mtuhumiwa lazima Pawe na Mtu Mwingine Kushuhudia
Shahidi: Ndiyo Lakini siyo lazima
Kibatala: Kwani wewe na Garry Breath nani Mtaalamu Wa Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi
Shahidi: Mimi
Kibatala: Kwani Wewe una Certificate hata ya Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi
Shahidi: Sina
Kibatala: Unafahamu Kwamba Garry Breath ni Daktari Wa Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi anatumia Mpaka na FBI Mbali na Kuandika Vitabu
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wewe Ulichukua Sampuli ngapi Kutoka kwa Bwire
Shahidi: Nane
Kibatala: Unafahamu kwamba inatakiwa uwe na Sampuli siyo Chini ya 15
Shahidi: Siyo Kweli
Kibatala: Kwani wewe Umepata wapi kuwa Sampuli Unatakiwa uchukue nane
Shahidi: Nilifundishwa Chuoni
Kibatala: Unafahamu Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi unashauriwa Uchukue Upper Case na Lower Case
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unatakiwa Uchukue alphabet, Panctuation Mark, na Namba
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Sasa si Ndiyo Upper case na Lower Case
Shahidi: Nilikuwa Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi inaendana na Sayansi ya INC DATING
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Wala Ufahamu Kwamba INC DATING ni Sayansi ya Uchukuaji Wa Maandishi Ilikujia Umri Wa wino tangu Maandishi yaandikwe
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je, unafahamu Kwamba kwetu sisi ni Muhimu Kujua Kama Michoro Khalfani Bwire alichora kabla ya Kukutana na Urio na Mbowe
Shahidi: Kwangu siyo Muhimu Kibatala: Kwani Kama Bwire alichora hiyo Michoro kabla ya Kukutana na Mbowe na Urio Je itahusiana na Kesi hii?
Shahidi: Inategemea
Kibatala: Inategemea nini
Shahidi: Unachokisema
Kibatala: Kama Bwire alichora Michoro kabla ya Kukutana na Mbowe na Urio itahusiana na Kesi hii?
Shahidi: Siwezi Kujibia Kibatala: Unaposema huwezi Kujibia ni Kwamba hutaki au hujui Shahidi: Basi rudia Swali
Kibatala: Kama Bwire alichora hiyo Michoro Tarehe 5 May 2020 Je, Kidaftari hicho kitakuwa na Umuhimu katika hii Kesi Shahidi' Hakitakuwa na Umuhimu
Shahidi: Na Bado Unasisitiza Kwamba Kwako Umuhimu ilikuwa siyo kimechorwa lini au Kimechorwa na nani
Shahidi: Umuhimu ilikuwa Kujua kimechorwa na nani
Kibatala: Je, unafahamu Maana ya Confirmation Bias?
Shahidi: Fafanua
Kibatala: Ni hali ya mtu Kufanya Upelelezi akiwa na Dhana yake Kichwani, Ili Kuthibitisha anachokiwaza yeye
Kibatala: Sasa Unafahamu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: huoni Kwamba Inawezekana Kilichorwa siku za Nyuma
Shahidi: Kama Kingekuwa na Nia Njema asingekataa
Kibatala: Unafahamu Kwenye Sayansi ya Upelelezi Maana ya Tool Elevation
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Ni hali ambayo unachungulia Dirishani au Mlangoni, Kisha Unakuja Kusema Umeona Kuna TV na unaacha Kusema Vingine Ulivyoviona Kama Vile Kabati, Meza na Redio
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Mheshimiwa Jaji, Kama shahidi amesema Kwamba hafahamu Kuhusu Tool Elevation, Sasa ni Vizuri kabla hajauliza swali ahakikishe shahidi Kaelewa
Kibatala: Mheshimiwa Jaji nimepokea Maombi ya Hisani nitafanya
Kibatala: Je, Shahidi Unafahamu Kwamba Katika Sayansi ya Uchunguzi na Upelelezi Wamekatazwa Kufanya Tool Elevation
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Shahidi nimesikia Unasema Kwamba Katika Shauri hili Mlalamikaji ni DCI
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: lakini huyo DCI ni Boss wa
Ramadhan Kingai
Boss wa Inspector Ndowo
Boss wa Inspector Mahita
Boss wa Inspector Swila
Boss wa Jumanne Malangahe
Boss wa DC Goodluck
Boss wa koplo Hafidh
Boss wa Sajenti Nuru
Wote ndiyo wapelelezi na ndiyo mashahidi
Shahidi: Ni sahihi lakini Kuna Vitengo tofauti
Kibatala: Kwani Hao Wa Vitengo Tofauti Hawapo Chini ya DCI
Shahidi: Ni Boss wao
Kibatala: Wakati huo Deputy DCI Alikuwa nani
Shahidi: alikuwa CHARLES KENYELA
Kibatala: DCI kama Yeye alikuwa Ndiye Mlalamikaji, asingemuachia Deputy DCI apeleleze
Shahidi: Si Kweli
Kibatala: Je, RPC akiwa anakutuhumu wewe, Anaruhusiwa Kukupeleleza?
Shahidi: Hairuhusiwi
Kibatala: Kwanini hairuhusiwi
Shahidi: Ni Utaratibu tu wa kazi
Kibatala: Order iliyotoka Kwa DCI unaweza Kui' Challenge
Shahidi: Inategemea
Kibatala: DCI alikupigia Su ufungue Jalada la Ugaidi, Unaweza Kumbishia
Shahidi: kama lipo sahihi nafungua
Kibatala: Kwani Wewe Wakati Unapewa Taarifa Ufungue Jalada la Kesi ya Ugaidi, Ulikuwa na Material gani Mbele yako
Shahidi: Uwepo wa Taarifa
Kibatala: Kwani hiyo Taarifa Ulipokea Wewe
Shahidi: Alipokea Afande Boazi
Kibatala: Mpaka Wakati huo Ulikuwa Umeomgea na Luten Urio au Ilikuwa bado
Shahidi: Ilikuwa bado
Kibatala: kwa hiyo wewe ulifungua sababu ya hear say
Shahidi: Taarifa zilikwepo
Kibatala: Tunataka Kujua Ulipokea Amri au Ulifanya Kazi kama Independent Detective, Je Wakati unafungua Faili ulikuwa Umeshamuhoji na a Kuandika Maelezo ya Afande Boazi
Shahidi: Ilikuwa Bado
Kibatala: Tunakubaliana Wakati wanaongea Urio na Mlalamikaji Afande Boazi wewe hukuwepo
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Na wewe bado Unasisitiza Kwamba Ulikuwa na Material Wakati unafungua Jalada la Kesi
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Unafahamu a Maana ya Hear say
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Ni sahihi Kwamba wewe Ulifanyia Kazi Hear Say
Shahidi: Ni Hear Say
Shahidi: Mheshimiwa jaji naomba niende washroom (chooni)
Shahidi amerejea
Kibatala: Shahidi tuliishia pale kwamba Yale uliyofungulia Kesi ni hear say
Kibatala: Je aliyekuwa Incharge Wa Upelelezi Wa Kesi hii yote alikuwa huyo huyo ROBERT BOAZ
Kibatala: Je Maelekezo na Taarifa zote Kuhusu Upelelezi Yalikuwa Yanatoka Kwa Robert Boaz
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Je Mtu huyo hana Maswahi Binafsi
Shahidi: Hana Maslahi Binafsi
Kibatala: Unafahamu Maslahi Binafsi na Viashiria Vyake
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Na hapa huvioni
Shahidi: Sivioni
Kibatala: Pride, Intergrity, Dignity ya DCI inajadiliwa katika kesi hii
Shahidi: Kinachojadiliwa hapa ni Kesi
Kibatala: Kwani nani alipokea Taarifa akaona Kwamba hapa Kuna Kosa la Ugaidi
Shahidi: DCI Robert Boaz
Kibatala: Unaona Hakuna Maslahi Binafsi
Shahidi: Hakuna
Kibatala: Wewe ulifungua Jalada Siku ya Tarehe 18 July 2020
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Ni kweli Kwamba ulifungua Jalada bila kuwa na Maelezo ya Robert Boaz
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Uliona Maelezo ya Robert Boaz Tarehe 13 August 2020 kuwa ameandika Chini ya Kifungu cha 3(3) cha Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai
Shahidi: Naomba Kuona (Ndiyo)
Kibatala: Unafahamu kwa Mujibu Wa Sheria, Askari anayepokea Taarifa Kwa Mdomo au Kwa Maandishi anatakiwa arekodi kwa Maandishi haraka sana
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Je unataka Kuniambia Kuwa Unaweza Kupokea Taarifa Kwa Mtoa Taarifa, Unaweza Kufungua Faili la Kesi bila Kuwa na Maelezo ya Mlalamikaji
Shahidi: Kama anaye Fungua Kesi ni Raia lazima Uchukue Maelezo, ila Kama Kwa Polisi Maelezo siyo lazima
Shahidi kapewa PGO
Kibatala: Tafuta sehemu inayosema Kwamba Taarifa Hii urekodi Mapema Sana na Taarifa Fulani siyo lazima
Shahidi: Nimekwambia Sikumbuki
Kibatala: Take your time (chukua muda wako) nimekuombea PGO hapo
Shahidi ANAPEKUA PGO
Shahidi: Kwenye PGO sioni mimi
Kibatala: Sasa nakuonyesha Kile Kifungu cha 10 (3) cha Sheria ya Mwenendo Wa Makosa ya Jinai Shahidi amesogezewa Laptop baada ya Mawakili wa Serikali kuihakiki laptop
Shahidi ANASOMA
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Unafahamu Maana hicho Kifungu
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji Sasa Maana yake
Shahidi: Kwamba Askari Polisi ambaye anapokea Taarifa, ataandika Maelezo ya Mtoa Taarifa yoyote
Kibatala: Sheria imeweka Utofauti?
Shahidi: Haijaweka
Kibatala: Haya taja Sasa Mwongozo ambao unakuruhusu Kutoandika Maelezo Ya Mlalamikaji kama Polisi
Shahidi: Sikumbuki
Kibatala: Sasa Mbona Ulisema Kuna Mwongozo, Lengo lako lilikuwa nini
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Haya nisionekane na Kuharass, Je Maelezo Ya Robert Boaz Uliandika lini
Shahidi: Tarehe 13 October 2020
Kibatala: Ni baada ya Miezi Mingapi
Shahidi: Miezi Mitatu
Kibatala: Bado Mnataka tusione Kuwa Kesi ni ya Kutunga
Kibatala: Haya Maelezo Ya Mtoa Taarifa umeandika lini
Shahidi: Tarehe 11 August 2020
Kibatala: Muda gani Umepita
Shahidi: Wiki Mbili
Kibatala: Kutoka Tarehe 18 July 2020 Mpaka 11 August 2020 ni Wiki Mbili
Shahidi: Ni Wiki 3
Kibatala: kwa hiyo tangu ufungue Faili hata Maelezo Ya Mtoa Taarifa ulichukua baada ya Wiki Tatu, kwanini tusiamini Mlimkamata Luten Denis Urio Mkampiga baada ya kutajwa na Adamoo kisha Mkampa Dili la kuwa Shahidi
Shahidi: Si kweli
Kibatala: Ulisema Kwamba ulifungua P. E file
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je, Faili la P.E ulilipa Kosa gani
Shahidi: Lile Jalada ni Jalada la Uchunguzi
(Shahidi anaongea)
Kibatala: Ukimaliza Kuongea Mambo yako Jibu swali Langu Jalada la P.E Uliandika Kosa au halikuwa na Kosa
Shahidi: Jalada la P. E halikuwa limeandikwa Kosa
Kibatala: Wewe Tarehe 14 Kwamba Robert Boaz amekutana na Denis Urio umeitoa Wapi
Shahidi: Nilipata Kwenye Kikaratasi alichonipa Kingai
Kibatala: Kwahiyo Kingai ndiye Kakwambia? Maana Kingai alikuwa katika Kikao cha Robert Boaz na Urio
Shahidi: Sahihi
Kibatala: Kwanini sasa Robert Boaz katika Maelezo Yake Hakuna Sehemu aliyoitaja Tarehe 14, angalia Maelezo hayo hapo
Shahidi: Hakutaja
Kibatala: Tafuta kwa Kingai Kama alitaja hiyo Tarehe 14
Shahidi: Hajataja
Kibatala: Kingai aliandika lini Maelezo Yake
Shahidi: Tarehe 28 June 2021 Kibatala: Nikisema hiyo Tarehe 14 mmebuni baada ya Sisi Kumuhoji Luteni Denis Urio
Shahidi: Si Kweli, Mimi Ndiye nilifungua faili
Kibatala: Kipi Ulicho Kifanya wewe Kama Mpelelezi Mpaka Tarehe 18 July 2020 Mpaka Ukapandisha Status ya Faili
Shahidi: Kingai alinielekeza nifanye hivyo
Kibatala: kwa hiyo Hakuna Ulicho fanya wewe cha Kupandisha Kupandisha Status ya Faili, zaidi ya Kingai
Shahidi: Ndiyo ilikuwa ni Maelezo ya Kingai
Kibatala: Kwa hiyo Mpaka Unapandisha Status ya Faili Kitoka Kwa Kingai ulikuwa Unawa Jua hao Wakina Khalfani Bwire
Shahidi: Hapana nilikuwa siwafahamu
Kibatala: Je, unafahamu Kwamba Urio na wenzake Kwa Mara ya Kwanza Walikutana Tarehe 20 July 2020
Shahidi: Ndiyo nafahamu lakini palikuwa na Mawasiliano
Kibatala: Ilikuwa ni Personal Knowledge au Mambo ya Hear say
Shahidi: Ilikuwa ni Hearsay
Kibatala: Na kama siyo hear Say tuambie hapa Denis Urio aliongea kwa mara ya Kwanza na Bwire au Lijenje
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Umeshawahi Kuona Mawasiliano ya Khalfani Bwire na Moses Lijenje
Shahidi: Kupitia Maelezo ya Onyo
Kibatala: Kwa Maana hiyo unamwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Mawasiliano ya Urio, Bwire na Lijenje ni Maelezo ya Onyo
Shahidi: Hapana
Kibatala: Nini kilisababisha ukapandisha hadhi ya Faili
Shahidi: Niliambiwa na Kingai nifanye hivyo
Kibatala: Ulisema Kwamba Moja wapo ya sababu ya Kuto weka Jina la Mbowe Mlikuwa mnaogopa Leakage, Je Wakati Mnafungua Faili Kingai aliwaambia Kuwa Kuna tuhuma Za Ugaidi
Shahidi: Hapana
Kibatala: Nani kati yenu aliye amua kuwa kuna tuhuma Za Ugaidi, Ni wewe au Kingai
Shahidi: Siyo Mimi
Kibatala: Ni lini baada ya Kufungua, Uliform Professional Opinion zako Ukaona Kwamba hapa Kuna tuhuma Za Ugaidi
Shahidi: Baada ya Kumuhoji Luten Denis Urio
Kibatala: Unasema Kwamba wewe ulikuwa Katika Kitengo X. Je, Ulimwambia Jaji Kwamba Wewe na Kingai Mlikaa Ofisi gani
Shahidi: Sikumbuki Kibatala Mimi nikisema hukusema Je utakataa
Shahidi: Sikumbuki
Shahidi: Tarehe 27 July 2020 Nilipokea Faili kutoka kwa DCI Nikampigia Simu Kwamba Jalada hili Mimi na wewe tumepangiwa, na Mimi Ni Msaidizi wako
Kibatala: Je ni Protocol ya Kawaida Faili Kutoka kwa Junior Officer Kwenda Kwa Superior Wako
Shahidi: Ni Jambo la Kawaida
Kibatala: Tarehe ngapi mliamua Kuwa Msiweke Jina la Freeman Mbowe Katika faili
Shahidi: Tarehe 18/7 Kibatala: kwenye Jalada la P. E Jina la Mbowe lilikuwepo
Shahidi: Lilikuwepo
Kibatala: Wakati huo Denis Urio alikuwa anafahamu tayari Kwamba Mbowe ni Mtuhumiwa
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Je unafahamu Kwamba Denis Urio alikuwa anaishi Wapi Wakati huo
Shahidi: Morogoro
Kibatala: Je, Denis Urio anakiapo cha Jeshi la Polisi
Shahidi: Hapana lakini ni Askari Wa JWTZ
Kibatala: Je, Denis Urio Mlimuapisha asitoe siri
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Denis Urio alikutana na Moses Lijenje na Khalfani Bwire kawaambia Mnaenda kwa Freeman Mbowe akiwashawishi Mambo ya Uhalifu Mniambie
Shahidi: Mimi sikuupata nafasi Kuongea naye
Kibatala: Je unaona Dhana yako ya Usiri bado upo Wakati Kingai tayari ameshaongea na Watu zaidi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je, unafahamu Kwamba Katika Kikosi cha Ramadhan Kingai, Gari yao Ilikuwa na Dereva wa Cheo Cha Chini anaitwa Azizi
Shahidi: Sifahamu
Kibatala: Je, unafahamu Kwamba Watuhumiwa Walikamatwa na Kupelekwa Kituo cha Polisi Moshi
Shahidi: Nafahamu
Kibatala: Unafahamu Kwamba Watuhumiwa Walienda Kituo cha Polisi Mbweni, Je bado Kuna sababu ya Usiri
Shahidi: Watuhumiwa walikuwa wameshakamatwa
Kibatala: Freeman Mbowe alikuwa amekamatwa?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Sasa ni Freeman Mbowe Mpumbavu kiasi gani kiasi Magaidi wake Wamekamatwa halafu yeye awe Mtaani
Shahidi: Jukumu letu lilikuwa Kuzuia Uhalifu usitendeke
Kibatala: Unafahamu tofauti ya Kulipua Vituo Vya Mafuta na Kuchoma Kituo cha Mafuta
Shahidi: Ni Mambo Mawili Tofauti
Kibatala: Wewe Ulikuwa na Maelezo ya Mashahidi ya Washitakiwa, Kwamba Kosa lilikuwa ni Kulipua Vituo Vya Mafuta na Kuchoma Masoko
Shahidi: Ni sahihi
Kibatala: Lakini Robert Boaz anasema Kwamba Ilikuwa ni Kuchoma Vituo Vya Mafuta
Shahidi: Lakini haibadilishi Kitu
Kibatala: Haibadilishi Kitu wakati umeshasema ni Mambo Mawili tofauti
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Na Kingai na Denis Urio Wanasema Kulipua Vituo Vya Mafuta, Je Mpaka hapo Kuna Sehemu Mtu kazumgumzi Kuchoma Moto Masoko
Shahidi: Hakuna sehemu ambayo wamesema Watachoma Masoko
Kibatala: Sasa Wewe Taarifa ya Kuchoma Moto Masoko ulitoa Wapi
Shahidi: Ni Terminology tuh
Kibatala: Mwanzoni si umesema Kwamba ni Tofauti, Ila sasa hivi no Terminology tu
Shahidi: (Kimya)
Kibatala: Haya Kwa Jumanne Malangahe anasema Kuchoma Moto Vituo Vya Mafuta na Kulipua Mikusanyiko ya watu
Shahidi: Tuone
Kibatala: SOMA HAPA
Shahidi ANASOMA "Kuchoma Vituo Vya Kuuzia Mafuta na a Kulipua Mikusanyiko ya watu"
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama Jumanne anasema Kulipua Masoko
Shahidi: Hakuna sehemu Imeandikwa Kulipua Masoko
Kibatala: Katika Ushahidi Wako Unasema Moja ya Source zako
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji Tulikuwa tunajadiliana na Wenzangu hapa, lakini Kuanzia pale alipoenda Kwa Boaz, URIO na Sasa Kwa Shahidi Mwenyewe Sisi Kwa Shahidi Mwenyewe hatuna Tatizo,Mahakama Inakuwa sehemu Ngumu sababu Wale wengine Wameshatoa Ushahidi Wao, Kama wanataka Kuingiza Maelezo Yale, Ilitakiwa Iwe Kwa Wale Mashahidi Kwa Mujibu wa Kifungu 164 cha Sheria ya Ushahidi limeweka Masharti
Sisi tunaona Kwamba Kile Kinachoingia katika Ushahidi, kinaingia Kinyume na Utaratibu
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Kwa Heshima na Tahadhima, Wao Wenyewe walikuwa wanazungumzia Kidaftari ambacho Hakipo Mahakamani, Kuwa na Usawa Pili kamw hakusimama wakati huo, Basi Kuna Estoppel Hawezi Kuja sasa Kuomba Mahakama Ifute Ushahidi Kwa kazi ambayo hatujaisaidia
Tatu ni kwamba nauliza Kutokana na Majibu wa shahidi Mwenyewe Labda Kama Nita uliza Maswali ambayo hayapo, Hii ni Cross examination Mheshimiwa Jaji ni hayo tu.
Jaji: Wakati Wakili anauliza Maswali Kuhusu eneo hilo shahidi aliomba Ruhusiwe Kurejea, ili aweze Kujibu Kwa namna ambavyo ameuliza ameuliza akiwa anarejea, na Shahidi amejibu Maswali hayo kwa namna ambavyo alikuwa anarejeshwa na Upande wa Utetezi
Kwa namna ambavyo ameuliza ameuliza akiwa anarejea, na Shahidi amejibu Maswali hayo kwa namna ambavyo alikuwa anarejeshwa na Upande wa Utetezi Ni kweli Nyaraka hazipo Katika Kumbukumbu za Mahakama
Katika Mazingira hayo Mahakama Inaona Kwa nma hiyo Maswali ambayo yameulizwa na Kujibia hayawezi Kuondolewa
Jaji: Mahakama Inaelekeza Wakili wa utetezi (Peter Kibatala) aendelee Kuuliza Maswali.. NATOA AMRI
Mawakili wa pande zote mbili wanakubaliana na Uamuzi Jaji kwa Kusimama na Kumuinamia Kidogo
Kibatala: Katika Maelezo Yako umeona kuwa Hakuna Kulipua Mikusanyiko ya watu
Shahidi: Ni sahihi, Kwenye Maelezo siwezi Kuandika Kila Kitu
Kibatala: Ulimwambia Mheshimiwa Jaji Kwamba Kwenye Maelezo uwezi Kuandika Kila Kitu
Shahidi: Hapana
Kibatala: Katika Maelezo Yako Hakuna Tarehe 14 July 2020 Kama sehemu ya Kufanya Majukumu yako
Shahidi: Ni kweli Hakuna
Kibatala: Ni kweli Shahidi Statement Yako Umerekodi wa Mapema Sana Kuliko Ushahidi Wa Leo hapo Kizimbani
Shahidi: Ni kweli
Kibatala: Mheshimiwa Jaji Ni Saa Saba na Dakika 5 naomba Kutoa Hoja tuairishe, nikirudi tuweze Kuendelea na Maswali ya Shahidi
Wakili wa Serikali Robert Kidando: Mheshimiwa Jaji hatuna Pingamizi
Jaji: natoa airisho Mpaka Saa 7 na Dakika 45
Jaji anatoka (1:06 PM)
Hawaoni hata aibuHivi hii mijamaa haioni aibu kutoa ushahidi wa kijinga kiasi hiki....!!?
MchongoDuh! Huu cross examination ya Kibatala imemfanya shahidi kuonekana ni takataka. Kichwani hakuna kitu. Weledi ni zero. IQ ni minimum.
Hata kama ana nia ovu, kama angekuwa na hata average IQ, angeuweka huo uovu wake kwa akili kidogo kuliko alivyouweka kiasi cha kumfanya aonekane ni brainless.
📌📌📌📌📌Kadiri hii kesi inavyoendelea ndivyo inavyozidi kuipata serikali matope na kutengeneza ushahidi usiopingika wahanga watakapoamua kukata rufaa ama kufungua kesi ya fidia