Yaliyojiri Mikutano ya CCM: Maridhiano ya kitaifa, Mchakato wa Katiba Mpya, Uteuzi, Pongezi kwa Rais Samia na Mwinyi


Habari za CCM hazina mvuto, labda kama zitavutia vyombo vya dola.
 
Kama Mtanzania Mzalendo, naunga mkono azimio namba 1 na 2. Na itapendeza sana kama haya maazimio mawili yatatanguliza maslahi ya Taifa, badala ya maslahi ya watu wachache, au vyama vyao vya kisiasa.
 
Moja ya point muhimu ambazo CCM imechelewa kuzichukua ni point kuhusu ishu ya Katiba mpya. Suala la umuhimu wa katiba mpya ni la wazi mno na hii ajenda ilipaswa ibebwe na CCM toka mwanzo hasa ukizingatia kuwa Mama alikuwa ndio makamu mwenyekiti wa Bunge la Katiba. Hata hivyo hatua iliyofikiwa ni nzuri sana na ya kupongezwa.

Kimsingi sio kila hoja inayoshikiliwa na wapinzani ni mbaya, hoja nyingine ni nzuri tu, na ni muhimu CCM ikawa inazichukua na kuzifanyia kazi hoja za msingi kama inavyofanya awamu ya 6. Kwa kufanya hivyo, inaufilisi upinzani kihoja na wanajikuta hawana hoja yoyote ya msingi. Huko nyuma tuliwahi kuwa na kiongozi mwoga wa hoja, haifahamiki alikuwa anagopa nini maana vyama vya upinzani Tanzania ni wepesi sana.

Ukweli ni kwamba CCM bado ni chama chenye utajiri mkubwa wa rasilimali watu ya kutosha na yenye uwezo mkubwa sana ukilinganisha na vyama mbadala. CCM ina rasilimali vitu na ushawishi vile vile ukilinganisha na vyama mbadala. CCM bado inao uwezo wa kushinda chaguzi vizuri kabisa pamoja na katiba mpya na tume huru ya uchaguzi. Changamoto iliyopo tu ni kwamba baadhi ya wana CCM wanakuwa hawana courage ya kutosha ya kutoa hoja zao na kuzitetea. Hali hiyo hufanya upinzani uonekane kama una hoja fulani hivi, japo kiuhalisia hoja zao ni nyepesi kama unyoya.

Trust me, upinzani wa Tanzania hauna stability yoyote. Hawana hoja za msingi isipokuwa chache tu kama Katiba mpya, Maridhiano na haki ambazo zimeshafanyiwa kazi na awamu ya Sita tena kwa ufanisi mkubwa sana.Uzuri ni kwamba mama hana woga kusimamia mambo ya msingi ambayo yana maslahi kwa Taifa.

CCM tuna uwezo mkuwa sana na nafasi nzuri ya kupambana kwa hoja na tukafanya vizuri sana. By the way sio lazima tuwe tunashinda kwa 99%k wenye chaguzi. Ushindi wa 70% tu unaopatikana kwa haki na kila mtu akiona haki ilivyotendeka inatosha sana. Raha ya mechi ushinde kwenye mchuano mkali na haki iliyo wazi kabisa na kila mtu aone unavyopiga mabao.

CCM tuna uwezo wa kushinda kwa hoja kwa sababu kuna vitu vingi vikubwa vinafanywa na Serikali ya CCM hasa katika kipindi hiki.CCM ina wasomi na rasilimali watu yenye uwezo mkubwa mno. No need to worry on anything.

Kwa sasa mtu anaweza kuitetea CCM kwa confidence kubwa sana na kwa hoja madhubuti kabisa.

Mungu Mbariki Kiongozi wetu umjaze hekima na busara zaidi. Naiona ile tuzo ya Utawala Bora Afrika ambayo imekuwa ikikosa mshindi sasa itakuja Tanzania. Mbele ni kuzuri na matumani kwa watanzania ni makubwa mno kwa sasa.
 
Uwepo wa Katiba mpya utaifanya Zanzibar isinjonywe na Tanganyika.
Maana wazenzi walio wengi hawaupendi huu Muungano ulivyo sasa.

Mama amefanya vizuri kuruhusu huu mchakato ili tufikie muafaka. Maana Marais wote wanaotokea Tanganyika hawakuwa wakiwasikiliza malalamiko ya wazenji.

Mama apewe tu Nishani ya heshima kwa uamuzi huu mzuri.
 
Zanzibar inanufaika zaidi na muungano kuliko hata sisi watu wa bara. Sema tu kuna watu wachache wanaopenda kulalamika, hao ndio wenye shida. Hata hivyo maridhiano ni kitu cha muhimu ili kusiwe na hisia za kwamba kuna mtu au upande hautendewi haki.
 
Kuzaliwa Kwa KATIBA mpya kutatimiza Unabii wa KIFO Cha KINYONGA wa KIJANI na MANJANO.

Kifo Cha KINYONGA huyo kitasababisha KUZALIWA Kwa Chama kingine Kutoka ndani ya Kinyonga.

Na CHAMA hicho kipya kitakuwa ni Kwa maslah mapana ya nchi. Amen
 
Kuzaliwa Kwa KATIBA mpya kutatimiza Unabii wa KIFO Cha KINYONGA wa KIJANI na MANJANO.

Kifo Cha KINYONGA huyo kitasababisha KUZALIWA Kwa Chama kingine Kutoka ndani ya Kinyonga.

Na CHAMA hicho kipya kitakuwa ni Kwa maslah mapana ya nchi. Amen
Ninyi ni watu wa ajabu sana. Watu ambao msichopenda kufanyiwa ndicho mnachopenda kuwafanyia wenzenu. Mfano hamtaki kutukanwa ila mnatukana wenzenu, Hamtaki udikteta, ninyi wenyewe hamna uvumilivu kabisa na mtu mwenye mawazo tofauti na yenu.

Ndio maana tunasema upinzani wa Tanzania sio wakuaminika kabisa maana waliopo humo hawana moral standards, ni wapiga kelele tu.
 
Habari za CCM hazina mvuto, labda kama zitavutia vyombo vya dola.
Hivi mkuu unajua unachotafuta kwa maslahi ya taifa?
Inaonyesha pengine hujui unachotafuta , na hivyo utajikuta unapinga hadi mambo ya maana yenye maslahi ya taifa
 
Ni jukumu sasa wadau wote wajue kwamba awamu ya 6 ipo kwa ajili ya ustawi wa taifa katika mapana yake na yanapokuja mambo serious ni muhimu kutanguliza maslahi ya taifa mbele, vinginevyo tutakwama tena mahali halafu tutaanza kulaumiana kumbe tunajikwamisha wenyewe kwa sababu ya ushabiki wa kitoto tu.
 

..mchukue na hoja ya muungano wa serikali 3.

..kuondoa madaraka ya ki-mungu-mtu ya raisi.

..ugatuzi wa madaraka. Ama kuanzisha mfumo wa serikali za majimbo.

..kuanzishwa kwa tume huru ya uchaguzi.


..na kuundwa kwa Tume ya ukweli na maridhiano.
 
Mimi ni MTANZANIA, nafuatilia siasa bt Sina Chama chochote.

Niko NEUTRAL, CCM Leo imenifurahisha kuridhia mchakato wa KATIBA mpya uanze.

Bt CCM ikikosea nairudisha Kwa mstari, CDM vile vile.

Msisahau kuwa Vyama vyote Kwa ujumla havifikishi wanachama mil 10 bt TANZANIA tupo zaidi ya Mil 60.

Lipo kundi kubwa sana msisahau ni Watanzania, wanashiriki siasa bila kuwa na vyama. Amen
 
Katika Hali ambayo haikutarajiwa hasa na CCM wenyewe, Katibu wao mwenezi amejitokeza na kutangaza hadharani kuwa CCM wako tayari kendeleza mchakato wa Katiba Mpya.

Katika hafla Ile wengi walionekana kupigwa butwaa huku wakishangilia kwa shangilio feki.
 
Pongezi kwa wote waliopiga kelele mpaka kelele zao zikasikika.
hii imenikumbusha migomo ya vyuoni kudai bumu litoke,Unashangaa kabla ya watu kugoma bumu lilikuwa
halitoki,wakigoma linatoka mpaka unajiuliza,kama tatizo lilikuwa ni ukosefu wa fedha
sasa fedha imetoka wapi baada ya wanachuo kugoma?

All in all nawapongeza halmashauri ya chama cha mapinduzi,kwa kuona nguvu ya hoja ya katiba mpya
 
Safi sana..haya ndio masuala ya kinchi..katiba mpya ni hitaji la wananchi.

Wapeni mwanachi katiba mpya...hizi kelele ziishe mbona simpo tu.

#MaendeleoHayanaChama
 
Hivi mkuu unajua unachotafuta kwa maslahi ya taifa?
Inaonyesha pengine hujui unachotafuta , na hivyo utajikuta unapinga hadi mambo ya maana yenye maslahi ya taifa

Mambo gani yenye maslahi ya taifa? Au huko kuingizana mjini ndio maslahi ya taifa?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…