Dah pole mama Sabrina!! Nina mkasa unaofanana na wako kidogo,kuna siku panya walikua wanasumbua sana kwenye store ya kihifadhia pumba ya kulisha nguruwe!! Siku moja niko free nikasema ngoja niwakomeshe maana nilikua hata nikiwawekea sumu hawali,.
Nikatoa magunia yote ya pumba nikacha moja tu ambalo kwa chini nilikua na mbao ambazo wamejificha humo.
Nikachukua mpini wa jembe nikawasha na taa yenye mwanga mkali nikabamiza mlango paaaah! Ili nikitembeza rungu wasitoke!! Niuwe wote
Nikatoa lile gunia ambalo kwa chini panya wengi wamejificha kwenye zile mbao,walitoka panya wengi wakirandaranda wasione pakutokea!.
Mi nikaanza kutembeza rungu nikaua wote pamoja na vitoto(sikumbuki idadi)
Nakuja kufungua mlango niwatoe nifanye usafi mlango haufunguki!! Vuta wapi kitasa kimejiloku afu home nipo alone simu ipo chaji geto
Nakumbuka nilikaa mle store kuanzia sasa 11 jioni mpaka kesho yake saa 2 asubuhi ambapo nilipata wazo la kutoboa ceiling board nikapita daarini mpaka kutobozea kwenye korido ya geto