Yamenikuta, maji yapo shingoni, naomba ushauri wapendwa plse!

Yamenikuta, maji yapo shingoni, naomba ushauri wapendwa plse!

huyo dada kabila gani?? na wewe ni kabila dani dini zenu ni zipi then tunaweza changia zaidi haya mambo yanaendana na udini na ukabila vile vile!
 
mmmh,ndoa ndoana.inashangaza,baada ya ndoa mke kubadilika.kwa kifupi huyo mke hana mapenzi tena na wewe,ila juu ya yote lazima kuna sababu,muulize,ukishindwa mchunguze bila ya yeye kujua ndio utaujua ukweli.hilo suala la mtoto apelekwe kijijini hiyo ni roho mbaya.kwani mtoto ni mtoto.na mtoto hana makosa,huyo mtoto hata ukimuachia hatomlea vizuri
 
Ni hivi Dada Lizzy,

Hayo hayakuwepo hapo mwanzo, imagine hata mtoto wangu aliishi nami pamoja na yeye na kuanza shule hapa mjini hadi darasa la 3 lkn mwaka huu mie narudi field ananiambia mtoto nimempeleka kijijini coz jeuri nataka akajifunze tabia huko rural. Nina mdogo wangu wa mwisho namsomesha na yupo day school, hawaongei hata akimwamkia hajibu hapo mimi nipo je nikiondoka inakuwaje mpendwa? Yaani baada ya ndoa tu tabia imebadilika sana, na sasa ndo ameajiriwa akitoka asubuhi kurudi jioni akifika tu kulala kisa amechoka, mie ndo niingie jikoni au huyo mdogo wangu. Da lizzy nipe ushauri plse

Dah!!Pole yako!

Well kwanza mkalishe chini umuulize nini sababu ya mabadiliko yake.Kwanini sasa hivi ndo aone ndugu zako pamoja na mwanao ni wabaya??Asipokupa majibu ya kueleweka ni bora muachane tu.Inawezekana amepata mtu huko wa kumpa kiburi....usiruhusu mali zikufunge kwenye kifungo cha mateso.Kama ulivyozipata hizo utapata na nyingine.
 
Ni hivi Dada Lizzy,

Hayo hayakuwepo hapo mwanzo, imagine hata mtoto wangu aliishi nami pamoja na yeye na kuanza shule hapa mjini hadi darasa la 3 lkn mwaka huu mie narudi field ananiambia mtoto nimempeleka kijijini coz jeuri nataka akajifunze tabia huko rural. Nina mdogo wangu wa mwisho namsomesha na yupo day school, hawaongei hata akimwamkia hajibu hapo mimi nipo je nikiondoka inakuwaje mpendwa? Yaani baada ya ndoa tu tabia imebadilika sana, na sasa ndo ameajiriwa akitoka asubuhi kurudi jioni akifika tu kulala kisa amechoka, mie ndo niingie jikoni au huyo mdogo wangu. Da lizzy nipe ushauri plse

Sitaki kuwa kwenye hukumu ya kushauri watu kuachana,ila mimi mke kama hawapendi ndugu zangu au wazazi wangu basi hanipendi!
Hey,kwani unadhani una tofauti na ndugu zako?...no,nyie ni damu moja,na hiyo damu haipendi!
Kwanini kuendelea kung'ang'ana nae?

Sasa napata akili kwanini mamangu alinambia nisikimbilie kuoa,...natamani ningekuwa karibu nikupe kalamu uanze kuchana mistari ya talaka fastaaaa!

Unajua ni kiasi gani wazazi wako wanaumia kwa kutokuwa huru kuja kwako lakini eh?
Unafurahia maumivu hayo?

Kama haonekani kupatanishwa achana nae,tupa kule
 
Kama walivyosema wengine hapo juu kwa nini abadilike ghafla inawezekana nduguzo wanamsimanga ukiwa haupo, cha msingi chunguza ujue chanzo ni nini na ukiona ye ndio mwenye makosa mpe muda ajirekebishe kwanza usikurupuke kumuacha na kama hataki kujirekebisha basi chapa lapa kwani mali kitu gani my dear mali zinatafutwa utapata nyingine pengine zaidi ya hizo.

Kama ukiridhishwa yeye ana makosa halafu hataki kujirekebisha ni pm nikupe mbinu zitakazofanya msigawane mali za uhakika labda kijiko na vigoda tu
 
achana nae huyo m/mke najua unaweza ukawa unampenda sana huyo mchumba wako lakini kwa nn aanze kukuonyesha red light mapema kiasi hiki wakati hata bado hakujapambazuka? Nina mfano wa ndg yangu mmoja alikuwa na kesi kama yako na walipoishia ni jamaa kuacha kila kitu kwa mkewe na akaenda kuanza moja, Bora wewe bado hata hamjafunga ndoa huyo ndg yangu yy alikuwa ameoa ila mkewe alikuja kumfukuza mama mkwe wake wakati jamaa yuko safarini.

Suala la mali sio issue kwanza hamjaoana mtagawana vp mali? nani ana ushahidi kuwa mliishi pamoja, timua huyo mapema au kama vp uza hivyo vitu mtimue halafu nunua vipya. Nakushangaa unashindwa kumtimua kwa kuofia mtagawana mali wakati sio mke wako?

Amka huyo si mke nakwambia na kama ukimuoa utapata laana ya ndugu, marafiki, wazazi na wafanyakazi wenzio hicho ni kimeo MUNGU amekuonyesa tu mapema
 
achana nae huyo m/mke najua unaweza ukawa unampenda sana huyo mchumba wako lakini kwa nn aanze kukuonyesha red light mapema kiasi hiki wakati hata bado hakujapambazuka? Nina mfano wa ndg yangu mmoja alikuwa na kesi kama yako na walipoishia ni jamaa kuacha kila kitu kwa mkewe na akaenda kuanza moja, Bora wewe bado hata hamjafunga ndoa huyo ndg yangu yy alikuwa ameoa ila mkewe alikuja kumfukuza mama mkwe wake wakati jamaa yuko safarini.

Suala la mali sio issue kwanza hamjaoana mtagawana vp mali? nani ana ushahidi kuwa mliishi pamoja, timua huyo mapema au kama vp uza hivyo vitu mtimue halafu nunua vipya. Nakushangaa unashindwa kumtimua kwa kuofia mtagawana mali wakati sio mke wako?

Amka huyo si mke nakwambia na kama ukimuoa utapata laana ya ndugu, marafiki, wazazi na wafanyakazi wenzio hicho ni kimeo MUNGU amekuonyesa tu mapema
Mkuu umepotea sana
 
Kama walivyosema wengine hapo juu kwa nini abadilike ghafla inawezekana nduguzo wanamsimanga ukiwa haupo, cha msingi chunguza ujue chanzo ni nini na ukiona ye ndio mwenye makosa mpe muda ajirekebishe kwanza usikurupuke kumuacha na kama hataki kujirekebisha basi chapa lapa kwani mali kitu gani my dear mali zinatafutwa utapata nyingine pengine zaidi ya hizo.

Kama ukiridhishwa yeye ana makosa halafu hataki kujirekebisha ni pm nikupe mbinu zitakazofanya msigawane mali za uhakika labda kijiko na vigoda tu
L.o.l Maty leo utafanya mkoloni wangu anipe notice kwa ajili ya kucheka
 
Wapendwa wana JF, mie ni mgeni na hii ni post yangu ya kwanza. Naomba msaada wenu wa mawazo ili ni-epuke hii adha ninayoipata.

Ni hivi wapendwa: Nilikuwa na girl friend wangu toka 2007 but tuliishi wote kwa makubaliano bila kufunga ndoa hadi mwaka jana mwezi wa 8, ndipo nikaona ni vema sasa tufunge ndoa. Lakin kilichochelewesha ni kuwa alikuwa anasoma chuo na sasa ni mwalimu wa sekondari.

Kifupi sijakaa naye saana coz 2008 nilenda nje ya nchi na nitarudi kusetle home mwakani, tatizo ni kuwa mke wangu hawapendi ndugu zangu hata mmoja,sisi tupo sita na mimi ni wa pili lkn hawapendi ndugu zangu: sio wifi zake wala shemeji zake. Kuhusu wazazi hapo ndo usiseme, nikienda nje ya nchi haendi kusalimia hadi mie nirudi na hata kuwapigia simu. Wazazi wangu kwangu hawafiki hadi mie niwepo bila hivyo hawafiki.

Nilijaribu kuongea naye mara kadhaa amekuwa mkali sana na hata amediriki kunijibu kuwa hanilazimishi kuishi na yeye. Lakini nahis anajibu kwa jeuri coz anajua tukiachana lazima tugawane mali: kama vile nyumba +usafiri n.k lakini hivyo vyote ni jasho langu la kupiga boxi ugaibuni.

Yeye sijazaa naye hata mtoto 1, lkn mie ninae alimkuta but hampendi na hataki nikae naye, mtoto wangu yupo kwa wazazi wangu kijijini. kwa kweli inaniuma saana. Kuhusu kuzaa yeye yaonyesha hadi afanyiwe operation, & it needs some millions of money hapo labda ndo atashika mimba (kulingana na vipimo vya hosp. moja kubwa ya hapa ya wahindi hapa DSM).

NB: 1. Nifanye nini ili mke wangu ajirekebishe tabia yake?
2. Japokuwa nampenda lkn wazazi wangu nao naona ni muhimu ktk maisha yangu,sasa nifanyeje ili naye awapende kama ninavyowapenda wazazi wake na ndugu zake?
3. Nikisema nimuache atataka tugawane MALI, wakati lile ni jasho langu la kupiga boxi, je nifanye nini?

Wapendwa samahani kwa maelezo marefu lakini naomba ushauri wenu na naomba msinitukane wapendwa, maji yamenifika shingoni. Sina nyumba ndogo na wala sina hamu tena ya kuoa, kweli najuta saaana tena saana kuoa!


Hizo red zimefanya nikwambie hivi:
1. Huyo mwanamke kukujibu kuwa hakulazimishi kuishi na wewe ni dalili mbaya sana eidha amekuchoka au kama kuna mtu hapa kasema angalia wasije wakawa wameshamchakachua na kumfundisha ujinga ili aachane na wewe ili mgawane hizo mali.
2. Hiyo ya kugawana mali umenishangaza sana wewe kama umemchoka na humtaki unaogopa nini kumuacha mali zinatafutwa lakini amani haitafutwi kama mali so amua tena ningekuwa mimi sigawani nae chochote namwuachia kila kitu.

Nawasilisha
 
Usikurupuke Bro kumuacha mkeo.

Fanya uchunguzi inawezekana ni hao ndugu zako ndio wana maneno. Ndugu hasa kama tegemezi au hawana cha kufanya kijijini, lazima watajaribu kuingilia ndoa yako ukiwachekea wanahania mjini kabisa na kujaza nyumba milele.

Isitoshe imeandikwa kila mmoja atamuacha baba na mama yake na kuambatana na mkewe, hao wawili watakuwa mwili mmoja. Kama nyie mnaelewana ndugu ndio wawaachanishe?? Labda hilo la mtoto wako kutokuishi na nyie ndio la msingi.

Ndoa changa haipendezi ndugu kuja kuishi na nyie manake mnakosa faragha.
 
Kama walivyosema wachangiaji wengine jua chanzo cha mabadiliko hayo, usipende kusikiliza maneno kutoka kwa ndugu zako inawezekana yanaukweli au uongo
ukishajua ukweli yeye ndio chanzo cha matatizo ni bora kumwacha
 
Dah dunia hii bwana kweli tu wasafiri. Hebu mshirikishe Mungu kwa nia moja hilo tatizo, hebu jaribu kuongea naye kwa lugha ya upendo, mweleze muulize ujue kwa nini anafanya hivo. Hebu tulia ili upate kujua kiini cha matatizo hayo nini? Haiwezekani awachukie wazazi na ndugu zako bila sababu. Na sababa inaweza kutokana na yy mwenyewe, mf. uchoyo nk nk, au ikatokana na hao wazazi/ndugu. Pengine ndugu hao wanamuona kauzibe kwa yale unayo/uliyokuwa unawafanyia na sasa hufanyi au unafanya kidogo.
 
Mkuu pole sana kwa kisa hiki....kifupi ni kwamba huyu sio mtu mwenye upendo na wewe na sio wewe tuu kwa ujumla hana hata chembe ya upendo na familia yako...bora kwa ndugu lakin hata kwa wazazi?...sidhan kama atarekebika huyu...kama hawapendi wazazi wako unadhan hata wewe anakupenda kweli? huyu nadhan yuko na wewe kwa sababu ni mtafutaji na pia hana future nzuri na wewe..mwanamke asietaka ushirikiano familia ya mume ni hatari sana. iko siku atakulazimisha ujikute huna uhusiano mzuri na wazazi na ndugu..watch out bro..mali na nyumba zisikufanye ujutie mashine mwako...zinatafutwa kirahisi ila uhusiano wa ndugu na wazazi ni kovu ambalo halifutiki kirahisi..huna mtoto nae na kuzaa bado ni issue halafu anakuwa na nyodo hivyo..nadhan fikiria kwa undani..usiogope mali kupotea.
Wapendwa wana JF, mie ni mgeni na hii ni post yangu ya kwanza. Naomba msaada wenu wa mawazo ili ni-epuke hii adha ninayoipata.

Ni hivi wapendwa: Nilikuwa na girl friend wangu toka 2007 but tuliishi wote kwa makubaliano bila kufunga ndoa hadi mwaka jana mwezi wa 8, ndipo nikaona ni vema sasa tufunge ndoa. Lakin kilichochelewesha ni kuwa alikuwa anasoma chuo na sasa ni mwalimu wa sekondari.

Kifupi sijakaa naye saana coz 2008 nilenda nje ya nchi na nitarudi kusetle home mwakani, tatizo ni kuwa mke wangu hawapendi ndugu zangu hata mmoja,sisi tupo sita na mimi ni wa pili lkn hawapendi ndugu zangu: sio wifi zake wala shemeji zake. Kuhusu wazazi hapo ndo usiseme, nikienda nje ya nchi haendi kusalimia hadi mie nirudi na hata kuwapigia simu. Wazazi wangu kwangu hawafiki hadi mie niwepo bila hivyo hawafiki.

Nilijaribu kuongea naye mara kadhaa amekuwa mkali sana na hata amediriki kunijibu kuwa hanilazimishi kuishi na yeye. Lakini nahis anajibu kwa jeuri coz anajua tukiachana lazima tugawane mali: kama vile nyumba +usafiri n.k lakini hivyo vyote ni jasho langu la kupiga boxi ugaibuni.

Yeye sijazaa naye hata mtoto 1, lkn mie ninae alimkuta but hampendi na hataki nikae naye, mtoto wangu yupo kwa wazazi wangu kijijini. kwa kweli inaniuma saana. Kuhusu kuzaa yeye yaonyesha hadi afanyiwe operation, & it needs some millions of money hapo labda ndo atashika mimba (kulingana na vipimo vya hosp. moja kubwa ya hapa ya wahindi hapa DSM).

NB: 1. Nifanye nini ili mke wangu ajirekebishe tabia yake?
2. Japokuwa nampenda lkn wazazi wangu nao naona ni muhimu ktk maisha yangu,sasa nifanyeje ili naye awapende kama ninavyowapenda wazazi wake na ndugu zake?
3. Nikisema nimuache atataka tugawane MALI, wakati lile ni jasho langu la kupiga boxi, je nifanye nini?

Wapendwa samahani kwa maelezo marefu lakini naomba ushauri wenu na naomba msinitukane wapendwa, maji yamenifika shingoni. Sina nyumba ndogo na wala sina hamu tena ya kuoa, kweli najuta saaana tena saana kuoa!
 
Hapo hakuna kitu Mangi,ishi kwa amani.wasiwasi wako ni mali.mimi wa kwangu nimemuachia kila kitu,nilitoka na nguo zangu na vitabu tu.mali utatafuta tu man.

hahahahaha nimecheka mpaka mbavu zinauma lol, we kweli ulimchoka
 
Sitaki kuwa kwenye hukumu ya kushauri watu kuachana,ila mimi mke kama hawapendi ndugu zangu au wazazi wangu basi hanipendi!
Hey,kwani unadhani una tofauti na ndugu zako?...no,nyie ni damu moja,na hiyo damu haipendi!
Kwanini kuendelea kung'ang'ana nae?

Sasa napata akili kwanini mamangu alinambia nisikimbilie kuoa,...natamani ningekuwa karibu nikupe kalamu uanze kuchana mistari ya talaka fastaaaa!

Unajua ni kiasi gani wazazi wako wanaumia kwa kutokuwa huru kuja kwako lakini eh?
Unafurahia maumivu hayo?

Kama haonekani kupatanishwa achana nae,tupa kule


Aisee kuna ndugu wana midomo na wanataka maamuzi yote muhimu kati ya wanandoa wahusishwe. Pia kuna wakwe ukiwachekea kutwa wanashinda hapo kwenu ilhali watu ndio kwanza mmeoana mnataka privacy.

Mara nyingi ndugu wa upande wa mume wanachangia sana ndoa za watoto wao kuvunjika. Wanaume tuamke na kukataa kutawaliwa na wazazi wetu hata kama wametuzaa. Familia yako ya zamani (wazazi) na ndoa yako ni vitu viwili tofauti, ukijaribu kuvichanganya una haribu. Haiwezekani mkeo awachukie ndugu zako bila sababu. Huyu bibie lazima hawa ndugu wa mume walisha mletea za kuleta ndo maana kawadelete.
 
Mkuu, kwa maelezo yako unaonesha kuangalia consequences za kuachana ...

the fact kwamba unafikiria ivo ni kwamba tayari ameshakutoka, hili la kusema bado unampenda siliamini sana maana hata mimi ningempendaje mtu hapendi ndugu zangu, hapendi mtoto wangu nk? Huenda ana act ivo sababu anajua anaweza asipate mtoto maishani but she could do better

kama yeye anaona pia kuachana na wewe sio issue, manake pia hakupendi kivile.....sasa angalia maisha yako yanaenda pande gani kama vipi tafuta mpango wa kando utulie zako kimyaaaa....:A S-key:
 
L.o.l Maty leo utafanya mkoloni wangu anipe notice kwa ajili ya kucheka

Mbona hicho kitu kidogo tu kama analeta jeuri, mnagawana na yule mliezaa nae for the sake of your child/children au yule ambae wewe baba umeamua kumuacha bila sababu so umempotezea muda wake. Lakini ambae analeta dharau, unamuomba abadilike hataki dawa yake ndogo sana

Kaka yangu yoyote humu akipata tatizo kama hili usisite kunitafuta utafurahi na roho yako, tena free of charge, ila uwe na uhakika wewe huna makosa hata chembe maana nikizungumza tu na wewe tajua kama u mkweli au unaleta usanii
 
Aisee kuna ndugu wana midomo na wanataka maamuzi yote muhimu kati ya wanandoa wahusishwe. Pia kuna wakwe ukiwachekea kutwa wanashinda hapo kwenu ilhali watu ndio kwanza mmeoana mnataka privacy.

Mara nyingi ndugu wa upande wa mume wanachangia sana ndoa za watoto wao kuvunjika. Wanaume tuamke na kukataa kutawaliwa na wazazi wetu hata kama wametuzaa. Familia yako ya zamani (wazazi) na ndoa yako ni vitu viwili tofauti, ukijaribu kuvichanganya una haribu. Haiwezekani mkeo awachukie ndugu zako bila sababu. Huyu bibie lazima hawa ndugu wa mume walisha mletea za kuleta ndo maana kawadelete.

Ndio inabidi kabla ya kuchukua maamuzi achunguze kwa umakini kabisa nini chanzo
 
Back
Top Bottom