Yamenikuta, maji yapo shingoni, naomba ushauri wapendwa plse!

summary
hapendi ndugu
hapendi mtoto
kuzaa mpaka operation
kiburi

ushauri

achana nae ( straight fowad)..huyo atasababisha uzee wako uwe wa manung'uniko.....utazeeka vibaya sana ndugu yangu....kwa kuwa ana matatizo ya uzazi alipaswa kukuheshimu wewe na ndugu zako....huyo hakupendi hata kama anakupikia......lol..halafu kamanda kuna mahali huwa unapuuzia maneno ya ndugu zako...najua wazazi wako wameshakwambia.....lakini leo kwa kuwa umeona maji yako shingoni na hii nadhani ni baada ya wewe kukaa mda mrefu bila kwnda ughaibuni....... angalia maisha yako mkuu na huyo mtoto na hizi mali ndizo zinakufanya uogope kuachana nae, jenga hoja mkuu wangu then mwache aende.....


 
The Following User Say Thank You to Speaker For This Useful Post:

 
Well said man! nadedicate kwako ule wimbo unaosema...mamaaa you are the queen of my heart.....
 
ningekuwa mimi ningemuacha na hizo mali tugawane maanaFuraha yangu ni kuona watu wangu wa karibu wanafurahi.
Mali inatafutwa ila furaha ni wewe mwenyewe kama utaamua kujipa furaha au lah.
 

hebu kasome tena maelezo yake.
 
Vipi huyo mchumba wako ni Yatima au amekulia kwenye mazingira magumu?? Wanawake wenye tabia hizo au mama wakwe huwa wamezaliwa kwenye mazingira magumu sana. Imagine unachukiaje ndugu wa mumeo? Yaani unajua hata huyu shetani nafikiri tunamsingizia mambo mengi sana.

Nakushauri umwache aendelee na majinamizi yake ya kishetani, kuchukia watu bila sababu, kama yuko tayari kubadilika sawa ila kabla ya kumuoa mpe tena miaka 3 uangalie kama amerudisha mapenzi kwa ndugu zako. othewise I advice you to leave her alone, wake wema wako wengi watakaokuja na upendo kwa familia yako na wanaokkuzunguka pia.
 
Huyo mwanamke ni mkorofi inavyoonekana maana angekua na utu na ubinadamu wa kweli angekupenda wewe na familia yako na hata kama ni kutokuelewana na ndugu ingikua kwa baadhi yao tu na si hivyo

CHA KUFANYA
MWACHE AEENDELEE NA MAISHA YAKE KAMA VILE HUJAWAHI KUKUTANA NAE
, MUONDOE NDANI YA MAWAZO YAKO YEYE PAMOJA NA YOTE MLOWAHI KUSAIDIANA YASAHAU
, ANZA UPYA USIMUULIZE CHOCHOTE TAFUTA KILA KITU UPYA maisha ni kitu cha kupita tu haina maana kuishi na mtu anaekutesa MOYO wako mwisho upoteze ndugu, wazazi, mtoto na marafiki hata na uhai wako
 
Maty hapo juu mama mi ninavyodha huyu kaka tayari kashaona ndugu zake ni bora kuliko mke wake, na kashafikia uamuzi wa kumwacha tatizo ni mali zake tu. Kuna kitu nakiona hapo, kuna uhusiano mkubwa kati ya mali zake na wazazi wake pia, sio bure hii spirit ya mali aliyonayo huyu ya kaka yawezekana na hawa ndugu zake wanayo. So wanaona mali kuliko mtu/utu. r
Sijaona sehemu kasema tabia ya huyu dada, naona wazazi na mali. Khaaa sijui lkn kwa vyovyote vile hata mi nikichoka ntasema kama wanichoka...sio bure
 
kwaangw laway!
 
MWANAMKE NI SAWA NA JEZI YA MPIRA UKIUMIA,ANAPEWA MWINGNE AITETEE TIMU,WANAWAKE WENGI WALIOSOMESHWA NA WENZI WAO HUA HAWANA CHA KULIPA ZAID YA MAUMIVU KAMA UYAPATAYO.KUHUSU SWALA LA MKEO INAHITAJIKA UFANYE MAAMUZI MAGUM.MFANO, UTAJISIKIAJE MIAKA IJAYO MWANAO WA KUMZAA AKUTUPIE LAWAMA KUA ULISHINDWA MTUNZA JAPOKUA UNAUWEZO KIFEDHA?↲Pili NI MKE YUPI DUNIANI ANAEKUA NA SIFA NJEMA NA ROHO NZURI KWA KUWACHUKIA NDUGU NA WAZAZI WA MUMEWE?↲MALI NI KITU GAN BILA FURAHA YA NAFSI?CHUKUA MFANO UMETUOMBA USHAURI ILI NAFSI YAKO ITULIE,MBONA HUKUTUOMBA HELA ILI MALI YAKO ISIPUNGUE? WEWE NI M2 WA AINA GANI UNAEKUBALI MWANAO AENDE KIJIJIN ILIHAL WAJUA FIKA NI UGUMU GANI ULIOPO UKO,KAMA NI MSOMI INABDI UPIME KAMA ELIMU YAKO IMEKUSAIDIA AU LA.THENK U.
 
Mkuu, pole sana na hizo changamoto.
Najua wengi wameshauri kwa kadiri ya uwezo wao, lakini kwa upande wangu ningeshauri wazo la 'KUVUNJA NDOA' ondoa kabisa.
Hebu fuata ushauri uliotelewa na wadau hawa









Siku zote lazima tujifunze kutatua na sio kukimbia matatizo. Kama ndoa yako ni ya KIKRISTO, basi imekatazwa kabisa kwa wanandoa kuachana isipokuwa kwa sababu ya uzinzi.
Kwa vile tatizo lako linaweza lisihusiane na uzinzi hivyo basi, yakupasa kutatua tatizo, labda ukirudi kutoka kubeba box.
Kaa na watu wenye busara, watu wa kanisa kama wachungaji jaribu kupata ushauri wao. Pia jaribu kutafuta nafasi nzuri ya faragha kuzungumza na mwenzio. Hayo matatizo yote yanasuluhisho... Hebu weka moyo wako na uamini kuwa utayapatia ufumbuzi matatizo yako na sio kuyakimbia, kwa sababu huna hakika utakutana na mtu wa namna gani.
Kama mliweza kupanga na kufunga ndoa pamoja na changamoto zote zile huoni kuwa unaweza kupata suluhisho??
Ndoa yako ni changa sana, haina hata mwaka,hivyo nafasi ya kupata solution ni kubwa sana. Mkae chini mzungumze
Labda angalizo kwa wasomaji wengine, mojawapo ya vitu vilavyoleta matatizo katika ndoa ni WATOTO wa nje kuletwa ndani ya ndoa. ni wanawake wachache sana wanaweza kuvumilia kwa moyo mmoja, lakini kama ikiwezekana watoto wa nje uwahudumie kivyao vyao..

Asante
 
We mamayo c ajapata bahati ya kudharauliwa na mke wa mtoto wake,kwanza mtoa mada anajua tatizo ni mkewe,na anahofia sana mali zake kuliko ki2 kingne.
 
freema: nawasiwasi na wewe mbona kama unamtetea sana au na wewe ndio tabia zako??

Kama wasiwasi wako ni kutetea, basi hata mim nakuwa na wasiwasi na wewe, umeshaacha mke kwa sababu kama hii?

Ukifanya kazi ya ushauri, matatizo haya hasa kwenye extended families kama za Kitanzania, ni mengi mno. Asilimia kubwa ya matatizo ya ndoa yanachangiwa na ndugu wa mume/mke kuingilia wana-ndoa. Hii humfanya mmoja wao ajione out of place.....ndipo vurugu zinapoanza.

Fikiria unaishi na shemeji yako, halafu anaanza kupeleka salamu za lawama kijiji, shemeji hanipikii, shemeji ananituma sana nakosa muda wa kujisomea, shemeji ananiangalia wakati nakula, shemeji haninunulii nguo, shemeji ananipa pocket money kidogo, shemeji anamchapa mtoto, hampi chakula, anamfokea....etc. Kinachofuatia ni ndugu wote kumwona huyo mwanamke mbaya, ana roho mbaya bila kuuliza chanzo cha yote. Tena ukute shemeji alikuwa anaishi na brother kabla hajaoa, ndio kabisa kwa sababu akija mwanamke ataleta sheria mpya. Shemeji anaona tabu. Kaka anapigiwa simu huko majuu, mkeo hivi, mkeo vile. Mambo yanaenda yakikua, mwisho wa siku yanafikia hapo yalipofikia.

Sisemi mwanamke yuko right, ila na ndugu wa wanaume, hasa wanapokuwa tegemezi kwa kijana wao, huleta vurugu na kashikashi kwenye ndoa, hasa changa na isiyo na mtoto.
 

Okey,siwezi kukulaumu sana!
Inategemea ulikuwa na uhusiano gani na wazazi wako wakati unakua,....
Kwenye amri za Mungu nizijuazo,...hakuna amri yoyote inayo ongelea mke (simaanishi kumdharau)!
Ila kuna amri inayo ongelea wazazi na ndiyo amri pekee yenye ahadi!,...utazidishiwa siku za kuishi.
Kwenye kitabu kitakatifu kuna sehem unaambiwa ikilazimika basi utaachana na mkeo,lakini hakuna sehemu inasema kwa namna yoyote ile umuudhi au kumsahau mzazi wako.

Simaanishi usimpende mkeo,..(imeamriwa umpende),..na tusitumie kigezo cha mme kuachana na wazazi wake kwenda kuwa mwili mmoja na mke wake kama sababu ya kuwasahau wazazi,...NI LAANA

Lakini mke anapokuwa sababu ya wewe kuvunja amri ya Mungu,..(waheshimu baba na mama upate heri na miaka mingi duniani),...huyo mke ana faida gani?
 
umezungumza uzuri,ila katka familia wote hamuwez kua na uwezo sawa,sasa m2 akisaidia ndugu mkewe alete mgogoro then uyo ni mke ambaye anafundsha sekondari na ni m2 mwenye elimu ya chuo,sasa anawafundisha nini wanafunzi huko shuleni? Mana kama wasifu wake wa ndani ndo huo,je unataka kusema utatofautiana na wasifu wake wa nje kiutendaji?
 
Huyo dada asiye na mzuka wa kumpikia mume wake kwa sababu ya 'kuchoka' amezidi. Hata kama ingekuwa ndugu zako ndo wabaya asingefikia hatua hiyo. Ukiwa nje unamiss misosi ya home vibaya, umerudi hakuna mapishi ya mkeo... dah! hiyo michosho si kawaida.
 
...natamani nikujibu kwa experience yangu, lakini sdidhani ni busara.

Fuata moyo wako, usifuate akili yako. Sikiliza kwa makini nini moyo wako unakushauri.
Ukiwa tayari, fanya maamuzi magumu na uyasimamie mpaka mwisho wa maisha yako.


Kila la heri.
 

Vunja ukimya ongea na mwenzako!
 
hii inawezeka kabisa, lkn ndio hata mtoto aliyemkuta hapo kamfanyia visa!!??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…