Yanayoendelea Wilayani Hai ni mkakati maalum

Yanayoendelea Wilayani Hai ni mkakati maalum

Kasomi

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2014
Posts
11,030
Reaction score
20,391
YANAYOENDELEA WILAYA YA HAI NI MKAKATI MAALUMU UMEPANGWA

Kwanza Niseme Jambo Moja Mliopo Nje Ya Wilaya Ya Hai Hamjui Kinachoendelea Huku Haya Masuala Naomba Mzingumze Kisiasa Sisi Wananchi Tunaoishi Hai Ndio Tunajua Chanzo Ni Nini kuhusu Yanayoendelea Na Nitoe Pongezi Zangu Sana Kwa DC Sabaya Kuisimama Wilaya Hii Kwa Weledi Mkubwa Sana Na Hai Ilivyo Sana Sio Ya Zamani .

Nianze Kwa Kusema Yafuatayo :

Cartbert Swai Mmiliki Wa Weruweru Lodge Mshirika Na Mfuasi Mkubwa Sana Wa Mwenyekiti Wa Chadema Freeman Aikaeli Mbowe Ambapo Ndugu Swai Ana Tuhuma Za Kuwatapeli Watumishi Wake Na Kuwarusha Mishahara Yao , Nimeona Amejirokodi Akiwa Kwenye Shamba Moja Akitoa Tuhuma Dhidi Ya Mkuu Wa Wilaya Ya Hai Ndugu Lengai Ole Sabaya Kwa Kile Kinachodaiwa Kuwa Alimfukuza Mwekezaji Kwenye Shamba Hilo.

Kwanza Naomba Tujiulize Maswali Machache Yenye Tija Na Kufikirisha Kidogo.

• Kwanini Haya Yanatokea Sasa Kuna Mpango Gani Nyuma Ya Pazia?

• Kwanini Viongozi Waandamizi Wa Chadema Akiwemo Godbless Lema , Kumbusho Dowson ( Bavicha ) , Tom Mwaipaja Msemaji Wa Bavicha Ndio Wamekuwa Wanasambaza Hiyo Clip Video Kwenye Mitandao Ya Kijamii Kuna Nini Wanataka Kukilinda Na Kwa Malengo Gani , Je Ishu Ni Cartbert Au Ni Sabaya ?

• Je Kwanini Haya Yanaibuka Wakati Rais Wetu Mama Samia Suluhu Aliposema Anajeukia Mikoa Na Wilaya Kufanya Teuzi Mpya Ndio Kujirekodi Kumetokea Kwa Cartbert Swai Mwanachama Wa Chadema Na Mfanyabiashara Wa Hai ?

• Lema , Cartbert, Tom Mwaipaja Na Kumbusho Dowson Mbona Wakati Dc Sabaya Aliporudisha Kiwanja Chetu Sisi Waislamu Tulichodhulumiwa Sikuona Mmejirokodi Clip Video Angalau Kumpongeza ?

Katika Elimu Yangu Kidogo Katika Masuala Ya Uongozi Na Siasa Nimejifunza Kuhusu Nguvu Ya Baadhi Wafanyabiashara Kutumia Ushawishi ( Power Of Convince ) Kutimiza Malengo Yao Hasi Ili Kudominate Nguvu Ya Watawala Kubow Kwao Ndicho Kinachoendelea Wilaya Ya Hai Kwa DC Sabaya Kusimama Na Wananchi Maskini Na Wanyonge Waliodhulumiwa Mashamba Yao Na Hawa Kina Cartbert Swai Ili Kuendeleza Uharamia Wao Wa Kutokugusika.

Mintarafu Kwa Wale Ambao Hafahamu Sakata Hili Kwa Undani Ni Kwamba Mwenyekiti Wa Chadema Freeman Aikaeli Mbowe Alimuapia Dc Sabaya Atatumia Gharama Yeyote Kuhakikisha Kuwa Hai Haitatawalika Ndani Ya Kipindi Chake Kwahiyo Haya Yanayoendelea Kuibuka Kwa Sasa Ya Mfanyabiashara Ndugu Cartbert Ni Muendelezo Wa Kauli Ya Mbowe Kuwatumia Wafanyabiashara Hawa Kisiasa Ili Kutimiza Malengo Yao Baada Ya Kuona Wilaya Ya Hai Kwasasa Wizi , Ubadhirifu Sacco's Za Wananchi , Ukandamizwaji Wa Haki , Uporaji Wa Mashamba Umedhibitiwa Ndani Ya Hai Sasa Njia Ya Kurejesha Hayo Ni Kumtoa Kafara Dc Sabaya. ( Hizi Mbinu Zinatumika Sana Na Wanasiasa Wengi Wenye Nguvu Kama Mbowe)

Siasa Za Hai Zimetamalaki Na Umafia Mwingi Kwa Pande Zote Mbili Za Baadhi Ya Wafanyabiashara Na Wanasiasa Na Sio Nyepesi Hata Kidogo Na Ikumbukwe Jimbo La Hai Lilikuwa Chini Ya Kiongozi Ambaye Alikuwa Mwamba Wa Siasa Za Kaskazini Na Kiongozi Wa Kambi Rasmi Ya Upinzani Kwa Miaka Mingi Kwa Mantiki Hiyo Haitakuwa Jambo Jepesi Sana Kwa Kijana Mdogo Kama Dc Sabaya Kupambana Hii Vita Dhidi Ya Watu Hawa Hatari Kwenye Nchi Ambao Wapo Kufanya Chochote Ili Kulinda Maslahi Yao Binafsi.

Aghalabu Katika Taaluma Ya Uongozi Kuna Kitu Kinaitwa Good - Interest Na Selfishness Katika Kile Kinachofanywa Na Mfanyabiashara Huyu Na Mwanachama Wa Chadema Ndugu Cartbert Swai Hana Good Interest Na Maisha Ya Wananchi Maskini Na Wanyonge Wa Hai Bali Ana Selfishness ( Which is Moral Cancer ) Ya Kutaka Lengo Lake La Kuendelea Kujimilikisha Mashamba Ya Wananchi Wanyonge Kama Alivyomfanyia Mama Mjane Kwa Kumpora Kwa Kisingizio Kuwa Ana Mkakati Wa Kibiashara ( Business Plan ) Hili Ni La Kukemewa Na Wananchi Wote Kwa Nguvu Zote Ndio Kaliba Ya Baadhi Ya Wafanyabiashara Wasio Waaminifu Walikuwa Na Kauli " Serikali Nimeiweka Mfukoni" Hili Halimuitaji Dc Sabaya Peke Yake Linatuhitaji Sote Kama Wananchi Wenye Mapenzi Mema Na Nchi Yetu Ili Kumsaidia Pia Mama Yetu Rais Samia Suluhu Hassan.

Mosi Ndugu Cartbert Swai Nikushauri Kuwa Uongozi Wa Awamu Hii Sita Ya Sasa Sio Uongozi Wa Fitna , Majungu , Uzandiki Na Siasa Chafu (Dirty Politics) Ili Kufanya Defamation Ya Mtu Mwingine Ili Kujijenga Wewe Kibiashara Kwa Njia Zisizo Halali Bali Ni Uongozi Uoendeshwa Kwa Misingi Ya Haki , Ustawi , Demokrasia Ya Kweli Pasipo Kumuonea Mtu Yeyote Kwa Maslahi Mapana Ya Wananchi Na Taifa Letu Hivyo Kama Wewe , Godbless Lema, Kumbusho Dowson , Tom Mwaipaja Msemaji Wenu Wa Bavicha Mmetumia Mbinu Hizi Kuchafua Viongozi Wa Serikali Ili Kumpambania Mwenyekiti Wenu Freeman Aikaeli Mbowe Kwenye Nafasi Yake Ya Kisiasa Jimbo La Hai Hii Umefeli Brother Tafuta Njia Bora Ya Kushughulika Na Changamoto Zinapotokea Ili Kutafuta Njia Nzuri Na Bora Kufikia Maelewano Ya Pamoja { Memorandum Of Understanding)

Nihitimishe Kwa Kusema Wazi Wilaya Ya Hai Kulikuwa Na Umafia Mwingi Sana Ulifanyika Kwa Miaka Mingi Kwa Baadhi Ya Wafanyabiashara Sampuli Ya Cartbert Swai Ambaye Pia Miaka Karibuni Alikopa Kiasi Kikubwa Sana Cha Mkopo Toka Benk Ya CRDB Na Kushindwa Kulipa Na Ilipelekea Nyumba Yake Kupigwa Mnada Hadharani Kufidia Deni Hilo, Je Nikuulize Na Haya Dc Sabaya Anahusika? Ifike Mahali Siasa Na Biashara Tusichanganye Na Kuharibu Taswira Ya Viongozi Kwa Maslahi Yetu Binafsi .

Kazi Iendelee...

Wasaalamu:

Raia Mwema Toka Hai
 
Ndio maana tumesema Ole ajitokeze kuongelea hizi tuhuma ili kama anachafuliwa hatua za kisheria zichukuliwe kwa mchafuaji

Kama sivyo awajibikie tuhuma zake

Tanzania ni yetu sote maendeleo hayana vyama
 
Mwambie alikutuma sisi sio wajinga. Sabaya ni kama Bashite tu madudu yao yako wazi wazi sana na sio kosa moja ana makosa ya jinai mengi sana wala sio mtu anaestahili kuwa uraiani achilia mbali kuwa na nafasi katika serikali alitakiwa kuwa jela yule ni mhalifu, jambazi, muuaji, mwizi, mhuni.

Nasema Sabaya sehemu anayostahili kuwepo ni gerezani tena maximum security prison.
 
Tuambie ni mambo gani ya neema yameanzishwa Hai toka huyo DC wako afike? Zaidi ya kutisha wawekezaji, kuvuruga mashamba, kufunga wafanyabiashara nk.

Kina mtatiro kule ruvuma wanakuza korosho, michezo, biashara, kilimo kingine, huduma za jamii etc Huyo wa moshi ni kujidai jasusi kila wakati...

Je, alitumwa kuiporomosha hai au kuiinua? Tunajua kaskazini ilichukuliwaje na jiwe!! Hata ukuta tunahisi ilikuwa kuzuia matajiri wa madini kaskazini, mbona ukuta haukujengwa kwake kuzuia dhahabu iliyo ghali kuliko tanzanite? Vikao vyote vikatolewa Ile Genova ya Afrika vikakimbiziwa kuleeee...

Mjini tunaishi kwa akili huyo DC kama ni bora sana ahamishiwe chato ili iwe mkoa haraka!

Hila zinamwishooo
 
Ndio maana tumesema Ole ajitokeze kuongelea hizi tuhuma ili kama anachafuliwa hatua za kisheria zichukuliwe kwa mchafuaji

Kama sivyo awajibikie tuhuma zake

Tanzania ni yetu sote maendeleo hayana vyama
Haya maisha mtu unatumia akili nguvu kutafuta angalau maisha bora anakuja stranglers anakufanya uishi kama panya mbaya sana haikubaliki aisee 🤔
 
Back
Top Bottom