Yanayofanyika Chato yanafanyika kote Nchini Tanzania

Unalinganisha kijiji cha chatu na miji mikubwa kama Dar, mbeya, Mwanza, Arusha nk, rudi ukafanye homework yako vizuri....
Hivi una ufahamu wa kuweza kutofautisha jiji na kijiji/tarafa?
 
Hivi una ufahamu wa kuweza kutofautisha jiji na kijiji/tarafa?
Hadhi ya chato ilinganishwe na vijiji vingine, siyo miji mikubwa na majiji....ndo maana butiama haijawahi kulinganishwa hadhi hata na Musoma hadi kujengwe makao makuu ya kanda na hospitali ya rufaa.
 
Bado mradi gani mpya ambao unahisi unatakiwa kuwepo Chato?
 
Mkuu,

Umejaribu kuelezea uwiano wa maendeleo vitu nchini Tanzania kwa sasa kwamba kinachofanyika wilayani Chato mkoani Geita ndicho kinachofanyika maeneo mengine Tanzania kwa sawiia lakini maelezo hajathibitisho kwa kuonesha angalu kwa mikoa kumi na tano tu 0ambayo haiko karibu karibu kwamba hicho unachotaka kuaminisha jukwaa hili ni kweli

1. Enzi za Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Burito alipokuwa mapumzikoni Butiama au Msasani mara kadhaa shughuli za serikali alizifanyia ikulu ndogo ya Mwanza (Capri point Mwanza), Musoma mjini na nyumbani kwao Mwitongo, Butiama;
2. Enzi Mwalimu Ali Hassan Mwinyi mapumzikoni alionekana ama Unguja Zanzibar, Jijiji Dar Es Salaam, Mikocheni au Temeke lakini shughuli za serikali alizifanyia ikulu ya Magogoni Dar Es Salaam;
3. Enzi za mwanadiplomasia na mwanahabari Benjamini William Mkapa alipokuwa mapumzikoni alionekana ama Moshi, Lushoto,Tanga na Lupaso, Masasi Mtwara na kufanyia shughuli za serikali ikulu ya Magogoni, Dar Es Salaam;
4. Enzi za Kanali mstaafu na mwanadiplomasia Jakaya Mrisho Halfan Kikwete alionekana ama nchi za nje, Jijijini Dar Es Salaam na Msoga na kufanyia shughuli zake za serikali katika ikulu ya Magogoni Dar Es Salaam au nchi yoyote huko ughaibuni inategemeana na alivyopanga;
5. Enzi za Mwalimu na Mkemia Dk John Pombe Magufuli anapokuwa mapumziko siku zote anaonekana Kijijini Rubambangwe na mjini Chato na kutekeleza majukumu yake ya Urais akiwa hapo Chato;

TANBIHI: Kwa hiyo ikulu sio jengo maalumu la kiofisi kwa utekelezaji wa majukumu ya kiuRas. Mahali Rais alipo hasubiri kurejea kwenye ikulu kuu ya Magogoni au Chamwino kutekeleza majukumu yake ya Urais, mahali popote alipo taasisi zote zinazounda mamlaka ya taswira ya Rais wa nchi zinafanyika kwa ufanisi ule ule.

Hakuna hata mwandishi au mwanasiasa yeyote wa sasa ambaye alishawahi kuelezea kwa kina makazi ya Rais mstaafu Jakaya Kikwete yaliyoko huko Msoga, Chalinze zaidi ya kushiriki hafla mbalimbali ambazo mhusika anapokuwa na nafasi ya kuwashirikisha kuujulisha umma hasa shughuli za kilimo na ufagaji, lakini yeye mwenyewe alishawahi kusikika akisema ni kweli ana makazi huko Msoga lakini hawezi kuishi huko.

Kauli hii ilitakiwa ifuatiliwe na ifafanuliwe vyema kwa manufaa ya jamii. Hospitali iliyopo hapo Msoga enzi akiwa madarakani ilikuwa imechangamka sana na majengo yalikuwa ni angavu lakini kwa sasa tayari yamechakaa na sijui kama kuna mpango wowote wa kuyahuisha kurudi katika ubora.

Hakuna shughuli za kiuchumi zilizowekezwa kuzunguka kijiji hicho ambacho inaonekana kina rutuba na hali ya hewa nzuri kwa kilimo, ufugaji na masoko ya mazao kama Nanasi, Mahindi, Papai, Machungwa na matikiti maji. Kabla hajamaliza muda wa uongozi wake ilipangwa kujengwa bandari ya nchi kavu kati ya Chalinze na Msoga lakini mpaka sasa hakuna chochote.

Kijiji kimezungukwa na misitu yenye uwanda mpana unaoweza kutengwa kwa ajili ya hifadhi na utalii. Lakini pia ndio eneo maarufu kwa sasa ambako ndipo yanapatikana mali asili madini mawe meusi ambayo yanatumika sana kwenye ujenzi wa miundo mbinu imara kama mchanganyiko wa lami, zege kwenye miundo mbinu ya ujenzi wa SGR, Stiglers Gorge dam, barabara, hata kwenye viwanda vya simenti kwa kuwa mawe hayo ni magumu sana.
 
We kweli bwege unalinganisha Dar na huo uchafu Chato?Dar inachangia asilimia 80 ya pato la Taifa,kwa kila shilingi 100 zinazokusanywa Kama mapato na TRA,shilingi 80,zinatoka Dar,hapo ni lazima Dar uipe kipaumbele,hata mtoto wa Darasa la Saba anajua Hili,sasa Chato Kuna nini?

Weka mifano sio kusema jiwe kajenga sehemu nyingi,
 
Huu ni ubinafsi kiwango cha lami haufai kufumbia macho hata kidogo
 
Mtoa mada unayashabikia haya kesho si ajabu akatunga sheria Kama utoki chattling ni marufuku kupata ajira serikalini ndipo utaikana post yako.Central Afrika, Rwanda na Burundi, nigeria yaliyaanza kidogo kidogo Kama haya ukabila,udini,ukanda kustukiza hakuna anaepumua
 
Ili tukuamini unachokisema weka miradi hiyo hapa kwa uwiano wathamani na uwiano wa mgawanyo wa kieneo na kikanda,kushindwa kufanya hivyo ni porojo na uimbaji wa mapambio unaloligharimu taifa hili.Ukweli ,na haki huinua taifa.
 
Kaka nilikua nakuheshimu sana kumbe kichwan bora kibuyu kabisa
Sema tu BAVICHA mna roho za ubinafsi sana, roho zimejikunja. Pingapinga, tu toka Taifa lipataje uhuru nyie ni kupinga pinga,
 
Chato, chato, chato= I am the state
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…