Tetesi: Yanayojiri ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)

Tetesi: Yanayojiri ndani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)

Hao wanaotaka abaki ni wale wenye maslahi moja kwa moja na u-RC wake. Ukumbuke hapo kuna wenye tender, zabuni na mazaga zaga kibao na ndio hao wanaojitoa akili kumkingia kifua.
Sasa kwani wewe unakubaliana na hoja ya atoke?
 
Taarifa za ndani za CCM ni kwamba mpaka sasa kumetokea mgawanyiko; wapo wanachama na baadhi ya viongozi wa CCM ambao wameunga mkono madai ya wananchi kuzitaka mamlaka zihakiki tuhuma dhidi ya Kada wa CCM na mkuu wa mkoa wa DSM bwana Paul Makonda almaarufu Daudi Bashite, juu ya vyeti vya kitaaluma. Na kundi lingine ambalo linaamini kwamba hata kama mkuu huyo alifeli darasa la saba au hata awe hakufika darasa la saba Kwa maslahi ya c...hama, akingiwe kifua.

Uongozi wa juu wa chama hicho umewaagiza wanachama kutokukuza madai hayo, na badala yake wajiandae Kwa mkutano mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika mwezi huu wa machi, kama maandalizi ya kubadili katiba ya chama hicho, iendane na matakwa ya mwenyekiti wao Mhe. Magufuli. Wasomi mbalimbali na wachambuzi wa masuala ya kiiasa wamedai kuwa CCM inakoelekea, inarudi zama za 'Kudumisha fikra za mwenyekiti'.

Takribani wiki mbili sasa, mkuu wa mkoa wa DSM amekuwa gumzo kwenye vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na mijadala mbalimbali, juu ya tuhuma dhidi yake, kwamba anatumia vyeti ambavyo sio vyake, mbali na kufeli kabisa mtihani wa kidato cha NNE Kwa kupata alama Sifuri, pia anasemekana alighushi vyeti.

Ndani ya CCM kinachoendelea ni kulazimishana na kuonyana kwamba wamuache Bashite aendelee na ukuu wa mkoa wasihoji taaluma yake na historia yake ya elimu.








Kwani wauza unga wamekuhonga kiasi gani .
 
kwa sasa kuna ccm kanda ya ziwa na ccm inayoguswa muda wowote.mfano kina manji. leo mkuu wa mkoa ana tuhuma za kutumia cheti cha mtu mwingine lakini haguswi.....
 
Nimekuja kuamini huu utajaji majina ilimlenga Mbowe kisha Chadema! Make humu inakuzwa sana chadema ni wauza madawa! Ndo maana wenye ujuvi wa mambo waliona vita ililenga watu ma si vita vya madawa. Baada mission kuwa imetimia, utajaji ukaisha!
Kwa maoni yangu chadema imeumia kwa hili sakata na upande wa pili umeumia pakubwa...sijui kama walitegemea backfire itakuwa kubwa kiasi hiki...sasa hivi hawana nguvu hata kama walikuwa na malengo fulani siku za usoni imekula kwao..hili kombara alilorusha mchungaji..ni kubwa..limeacha majeruhi wengi..watu hawajamini tena...na bunge likianza nategemea msukuma atupe scad nyingine amalize game...
 
nilisikia uvccm wanapanga maandamano ili kuunga mkono serikali KUSITISHA UKAGUZI WA VYETI , kwa madai kwamba unaingilia siri za wahitimu .
 
Imekula kwenu nyumbu nyie aliyepewa na kapewa hata siku moja mwanadamu hawezi kutengua ata kama makonda ataondolewa kwenye urc bado anayo nafasi kubwa ya kuwa kiongozi mkubwa ndani ya taifa hili
 
Hao wanaotaka abaki ni wale wenye maslahi moja kwa moja na u-RC wake. Ukumbuke hapo kuna wenye tender, zabuni na mazaga zaga kibao na ndio hao wanaojitoa akili kumkingia kifua.
Vinginevyo haileti maana kumtetea.
 
Taarifa za ndani za CCM ni kwamba mpaka sasa kumetokea mgawanyiko; wapo wanachama na baadhi ya viongozi wa CCM ambao wameunga mkono madai ya wananchi kuzitaka mamlaka zihakiki tuhuma dhidi ya Kada wa CCM na mkuu wa mkoa wa DSM bwana Paul Makonda almaarufu Daudi Bashite, juu ya vyeti vya kitaaluma. Na kundi lingine ambalo linaamini kwamba hata kama mkuu huyo alifeli darasa la saba au hata awe hakufika darasa la saba Kwa maslahi ya c...hama, akingiwe kifua.

Uongozi wa juu wa chama hicho umewaagiza wanachama kutokukuza madai hayo, na badala yake wajiandae Kwa mkutano mkuu wa CCM unaotarajiwa kufanyika mwezi huu wa machi, kama maandalizi ya kubadili katiba ya chama hicho, iendane na matakwa ya mwenyekiti wao Mhe. Magufuli. Wasomi mbalimbali na wachambuzi wa masuala ya kiiasa wamedai kuwa CCM inakoelekea, inarudi zama za 'Kudumisha fikra za mwenyekiti'.

Takribani wiki mbili sasa, mkuu wa mkoa wa DSM amekuwa gumzo kwenye vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na mijadala mbalimbali, juu ya tuhuma dhidi yake, kwamba anatumia vyeti ambavyo sio vyake, mbali na kufeli kabisa mtihani wa kidato cha NNE Kwa kupata alama Sifuri, pia anasemekana alighushi vyeti.

Ndani ya CCM kinachoendelea ni kulazimishana na kuonyana kwamba wamuache Bashite aendelee na ukuu wa mkoa wasihoji taaluma yake na historia yake ya elimu.
Kilichopo hapa ni kutokana na ukweli kuwa watu wanachanganya mambo mawili, kuna vita ya madawa ya kulevya na kuna tuhuma zimeibuka za vyeti bandia. Ishu ya madawa ya kulevya haina mjadala, ni vita ilikuwepo na kwa bahati nzuri mkuu wa mkoa ametia nguvu vitahivyo baadaye rais ameweka chombo husika cha kushughulikia ambapo sioni tena nafasi ya mtu yeyote kuwaingilia wataalam hao. Kuanzia mwezi wa nane mwaka wa jana serikali ilikuwa na mkakati wa kuhakiki vyeti vya watumishi ambapo tunaambiwa kuna baadhi ya watu wafanyakazi walibainika kuwa na vyeti ambavyo sio vyao, naamnini hatua zimechukuliwa kwa wote waliodakwa. Baraza la mitihani limeshatangaza kuwa mwenye taarifa ya mtu yeyote ambaye anajua mtu mwenye cheti cha bandia atoe taarifa, mimi sioni tatizo kwakuwa nchi hii inajigamba kuwa ni ya ukweli na uwazi na kwakuwa huenda watu wanamsingizia Mkuu wa mkoa, jambo la msingi hapa mkuu ajisafishe kwa kueleza ukweli wa jambo hilo maana mpaka sasa uhakiki wa vyeti bado unaendelea, vinginevyo zoezi hilo litakuwa la kibaguzi.
 
Back
Top Bottom