Cute Wife
JF-Expert Member
- Nov 17, 2023
- 1,906
- 5,000
Wakuu,
Leo mbali na kuwa ni Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA pia wanasherekea Miaka 32 ya CHADEMA kupata Usajili wa Kudumu, ambapo ulipatikana Januari 21, 1993.
Mbivu na mbichi kujulikana leo, tumeona mengi na kusikia mengi kila upande ukitetea kwake. Je, nani ataibuka kidedea? Nani atatolewa kimasomaso na wajumbe?
Katika uchaguzi huu wajumbe watachagua Mwenyekiti Taifa pamoja na Makamu Mwenyekiti kwa Bara na Zanzibar, ambako ushindani mkubwa upo kati ya Mbowe na Lissu kwa nafasi ya Uenyekiti, na Wenje na Heche kwa nafasi ya Umakamu Uenyekiti.
Je, ni Mbowe au Lissu? Ni Heche au Wenje?
Orodha ya Wagombea wote ni;
Mwenyekiti Taifa
Wagombea Wanatoa Salamu kwa Wageni Waalikwa na Wapiga Kura
Tundu Lissu
Lissu amshukuru Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe kwa kufanya nae kazi kwa kipindi cha miaka 20, licha ya kutofautiana kimitazamo lakini amekiri hawajawahi kugombana.
"Nimekaa pembeni ya Mwenyekiti wetu wa Chama mfululizo kwa miaka zaidi ya 20 na katika kipindi chote hicho hatajawahi kugombana, hatujawahi kupigana mimi na yeye binafsi. Ndio tumetofautiana kimsimamo lakini hatujawahi kugombani"
"Vyovyote itakavyokuwa leo, tutakuwa pamoja katika kukijenga chama chetu (Chadema)"
Freeman Mbowe
"Hiki chama tunawajibu wote wa kibinadamu na Wakimungu wakukilinda kwa gharama yoyote ile, na chama hiki hatutakiruhusu kwa gharama yoyote eti kwasababu pengine kura za mbowe hazikutosha au kura za Mhe. Lissu hazikutosha ama za Mhe. Odero yule mzee wetu wa kesho kuna mwanga kwamba kura hazijatosha".
"Uchaguzi huu usiwe vita unapashwa kuwa furaha ya ujenzi wa demokrasia"
"Wako watabiri wengi sana wamesema kuhusu uchaguzi wa CHADEMA, Mhe. Mbowe unaenda kukipasua chama, Mhe. Mbowe inakuaje, hawa ni wanademokrasia, wote kama mnavyowaona. Tofauti zetu kwenye mitazamo hii naamini tunakwenda kuizika mwisho wa kikao hiki tunanelea mbele stronger together"
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, ametoa taarifa kwa ufupi kuhusiana na hali halisi ya Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na Urais wa mwaka 2020.
Mnyika asoma maazimio ya kamati kuu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa (2024), ambapo yatapelekwa Mkutano Mkuu kwaajili ya kupendekezwa kupitishwa kama maadhimio ya mkutano mkuu wa chama.
Mnyika amehitimisha kwa kuwasilisha mapendekezo ya maazimio ya Mkutano Mkuu
Zoezi la uhakiki wa Wajumbe
Shughuli za uhakiki wa wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zinaendelea katika ukumbi wa Mlimani City.
Uhakiki huo unaongozwa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na kukamilika kwake kutaashiria kuanza kwa uchaguzi wa nafasi za uenyekiti na makamu wa chama hicho Taifa.
Wajumbe 996 wathibitishwa ni halali, zoezi la kura kuanza.
Update
Matokeo ya Uchaguzi Mkuu CHADEMA nafasi ya Mwenyekiti Taifa na Makamu Mwenyekiti
Awamu ya 1 nafasi ya Makamu Mweyekiti Zanzibar
Suleiman Issa alipata kura 67 sawa na 7%
Hafidhi Salehe alipata kura 241 sawa na 24%
Said Mzee Said alipata kura 301 sawa 30%
Said Isaa Mohamed alipata kura 388 39%
Wapiga kura waliojisajili 1014
Kura zilizopigwa - 1003
Kura halali 997, Habikika 6
Awamu ya Pili
Wagombea wawili baada ya mmoja kujitoa
Said Mzee Said
Kura zilizopigwa 706
Halali 700
Zilizoharibika 6
Za ndio 625 sawa na 89%
Hapana 75 sawa na 11%
Makamu Mwenyekiti Bara
Wapiga kura 1014
Kura zilizpogwa 1005
Halali 998
Haribika 7
Mathayo Gepgkul
Kura 49 5%
Ezekia Wenje
Kura 372 37%
John Heche
Kura 577 57%
Nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa
Wapiga kura jisajili 1014
Kura zilipigwa 999
Halali 996
Zilizoharibika 3
Odero Odero
Kura 1 0.1%
Freeman Mbowe
Kura 482 48.3%
Tundu Lissu
Kura 513 51.5%
Updates za Matukio
Leo mbali na kuwa ni Uchaguzi Mkuu wa CHADEMA pia wanasherekea Miaka 32 ya CHADEMA kupata Usajili wa Kudumu, ambapo ulipatikana Januari 21, 1993.
Mbivu na mbichi kujulikana leo, tumeona mengi na kusikia mengi kila upande ukitetea kwake. Je, nani ataibuka kidedea? Nani atatolewa kimasomaso na wajumbe?
Katika uchaguzi huu wajumbe watachagua Mwenyekiti Taifa pamoja na Makamu Mwenyekiti kwa Bara na Zanzibar, ambako ushindani mkubwa upo kati ya Mbowe na Lissu kwa nafasi ya Uenyekiti, na Wenje na Heche kwa nafasi ya Umakamu Uenyekiti.
Je, ni Mbowe au Lissu? Ni Heche au Wenje?
Orodha ya Wagombea wote ni;
Mwenyekiti Taifa
- Freeman Mbowe
- Odero Odero
- Tundu Lissu
- Ezekia Wenye
- John Heche
- Mathayo Gekul
- Hafidh Saleh
- Said Issa Mohammed
- Said Mzee Said
- Suleiman Makame Issa
Wagombea Wanatoa Salamu kwa Wageni Waalikwa na Wapiga Kura
Tundu Lissu
Lissu amshukuru Mwenyekiti wa Chama, Freeman Mbowe kwa kufanya nae kazi kwa kipindi cha miaka 20, licha ya kutofautiana kimitazamo lakini amekiri hawajawahi kugombana.
"Nimekaa pembeni ya Mwenyekiti wetu wa Chama mfululizo kwa miaka zaidi ya 20 na katika kipindi chote hicho hatajawahi kugombana, hatujawahi kupigana mimi na yeye binafsi. Ndio tumetofautiana kimsimamo lakini hatujawahi kugombani"
"Vyovyote itakavyokuwa leo, tutakuwa pamoja katika kukijenga chama chetu (Chadema)"
Freeman Mbowe
"Hiki chama tunawajibu wote wa kibinadamu na Wakimungu wakukilinda kwa gharama yoyote ile, na chama hiki hatutakiruhusu kwa gharama yoyote eti kwasababu pengine kura za mbowe hazikutosha au kura za Mhe. Lissu hazikutosha ama za Mhe. Odero yule mzee wetu wa kesho kuna mwanga kwamba kura hazijatosha".
"Uchaguzi huu usiwe vita unapashwa kuwa furaha ya ujenzi wa demokrasia"
"Wako watabiri wengi sana wamesema kuhusu uchaguzi wa CHADEMA, Mhe. Mbowe unaenda kukipasua chama, Mhe. Mbowe inakuaje, hawa ni wanademokrasia, wote kama mnavyowaona. Tofauti zetu kwenye mitazamo hii naamini tunakwenda kuizika mwisho wa kikao hiki tunanelea mbele stronger together"
Katibu Mkuu wa CHADEMA, John Mnyika, ametoa taarifa kwa ufupi kuhusiana na hali halisi ya Uchaguzi Mkuu wa Wabunge na Urais wa mwaka 2020.
Mnyika asoma maazimio ya kamati kuu kuhusu uchaguzi wa serikali za mitaa (2024), ambapo yatapelekwa Mkutano Mkuu kwaajili ya kupendekezwa kupitishwa kama maadhimio ya mkutano mkuu wa chama.
Mnyika amehitimisha kwa kuwasilisha mapendekezo ya maazimio ya Mkutano Mkuu
Zoezi la uhakiki wa Wajumbe
Shughuli za uhakiki wa wajumbe wa mkutano mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) zinaendelea katika ukumbi wa Mlimani City.
Uhakiki huo unaongozwa na Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika na kukamilika kwake kutaashiria kuanza kwa uchaguzi wa nafasi za uenyekiti na makamu wa chama hicho Taifa.
Wajumbe 996 wathibitishwa ni halali, zoezi la kura kuanza.
Update
Matokeo ya Uchaguzi Mkuu CHADEMA nafasi ya Mwenyekiti Taifa na Makamu Mwenyekiti
Awamu ya 1 nafasi ya Makamu Mweyekiti Zanzibar
Suleiman Issa alipata kura 67 sawa na 7%
Hafidhi Salehe alipata kura 241 sawa na 24%
Said Mzee Said alipata kura 301 sawa 30%
Said Isaa Mohamed alipata kura 388 39%
Wapiga kura waliojisajili 1014
Kura zilizopigwa - 1003
Kura halali 997, Habikika 6
Awamu ya Pili
Wagombea wawili baada ya mmoja kujitoa
Said Mzee Said
Kura zilizopigwa 706
Halali 700
Zilizoharibika 6
Za ndio 625 sawa na 89%
Hapana 75 sawa na 11%
Makamu Mwenyekiti Bara
Wapiga kura 1014
Kura zilizpogwa 1005
Halali 998
Haribika 7
Mathayo Gepgkul
Kura 49 5%
Ezekia Wenje
Kura 372 37%
John Heche
Kura 577 57%
Nafasi ya Mwenyekiti CHADEMA Taifa
Wapiga kura jisajili 1014
Kura zilipigwa 999
Halali 996
Zilizoharibika 3
Odero Odero
Kura 1 0.1%
Freeman Mbowe
Kura 482 48.3%
Tundu Lissu
Kura 513 51.5%
Updates za Matukio
- Mwamakula: Wajumbe wameambiwa kuipiga picha au kuweke alama karatasi ya kura kama ushahidi wa kuongezewa pesa baadaye
- Jumla ya wajumbe wanaoenda kupiga kura ni 996, zoezi la kupiga kura linaanza muda wowote kuanzia sasa
- Frank Mwakajoka kachaguliwa kuwa mwenyekiti wa uchaguzi
- Mgombea Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Zanzibar: Vijana walipewa nafasi ya kukiongoza chama hawakufanya kit