Mario Kejob
JF-Expert Member
- Apr 14, 2020
- 441
- 536
Maamuzi waliyochukua Yanga yatakuja kuwagharimu siku za usoni ya kuwataka TFF kufuata kanuni kwa asilimia mia moja. Ipo siku Yanga watakuwa na dharura ya kweli kwa mfano kupata puncture au flat tire wakati wanakwenda uwanjani na hivyo kuwapigia simu TFF kusogeza mchezo mbele kutokana na dharura hiyo, hapo ndipo Yanga watajua what goes around comes around.
Maamuzi haya yatakuwa kama boomerang na kuwapiga wao wenyewe pale TFF itakapo wajibu kwamba kanuni hairuhusu na wanahitaji masaa 24 kufanya hivyo.
Delay na postponement ni vitu viwili tofauti. Si amini kuwa delay ya game inahitaji notice ya masaa 24 ila postponement ndiyo inahitaji. Je? Mchezaji wa Yanga akipata ajali na kufariki siku ya mechi, Yanga watawajibika kucheza mechi siku hiyo? Si wataomba mchezo uahirishwe!
Hapo masaa 24 watayatoa wapi? Na hiyo timu pinzani ikifanya kama walivyofanywa Yanga, si tutakuwa tunaliua soka letu! Na kwa mantiko hiyo basi; Yanga hawakutaka TFF itii agizo la serikali ili mchezo uendelee katika muda awali?
Masikini washabiki na wapenda soka wa nchi hii waliojazana uwanjani kwa maelfu, gharama zao na muda wao nani atawalipa?
Upo uwezekano wa CAF na FIFA kuingilia kati suala hili, nani atajibu hoja zao? Na kama kutakuwa na penalties, nani atalipa?
Jamani tuwe tunachukua maamuzi ya busara kwa faida ya maendeleo ya soka letu na nchi yetu kwa ujumla.
Kama kichwa cha habari kinavyosema hapo juu, hili litakuwa ni " tukio rejea" la matukio kama haya yakayofuata siku za usoni. Hivyo, maamuzi yoyote yatakayotolewa yazingatie haki, sheria na kanuni ili tusije ku-set a bad precedent kwa timu nyingine kufanya hivyo baadae ikizingatiwa kuwa timu zote zina haki sawa.
Maamuzi haya yatakuwa kama boomerang na kuwapiga wao wenyewe pale TFF itakapo wajibu kwamba kanuni hairuhusu na wanahitaji masaa 24 kufanya hivyo.
Delay na postponement ni vitu viwili tofauti. Si amini kuwa delay ya game inahitaji notice ya masaa 24 ila postponement ndiyo inahitaji. Je? Mchezaji wa Yanga akipata ajali na kufariki siku ya mechi, Yanga watawajibika kucheza mechi siku hiyo? Si wataomba mchezo uahirishwe!
Hapo masaa 24 watayatoa wapi? Na hiyo timu pinzani ikifanya kama walivyofanywa Yanga, si tutakuwa tunaliua soka letu! Na kwa mantiko hiyo basi; Yanga hawakutaka TFF itii agizo la serikali ili mchezo uendelee katika muda awali?
Masikini washabiki na wapenda soka wa nchi hii waliojazana uwanjani kwa maelfu, gharama zao na muda wao nani atawalipa?
Upo uwezekano wa CAF na FIFA kuingilia kati suala hili, nani atajibu hoja zao? Na kama kutakuwa na penalties, nani atalipa?
Jamani tuwe tunachukua maamuzi ya busara kwa faida ya maendeleo ya soka letu na nchi yetu kwa ujumla.
Kama kichwa cha habari kinavyosema hapo juu, hili litakuwa ni " tukio rejea" la matukio kama haya yakayofuata siku za usoni. Hivyo, maamuzi yoyote yatakayotolewa yazingatie haki, sheria na kanuni ili tusije ku-set a bad precedent kwa timu nyingine kufanya hivyo baadae ikizingatiwa kuwa timu zote zina haki sawa.