Yanga Afrika lazima tukae chini tujitafakali kwa walichokifanya Simba liwe funzo kwetu

UHURU KABANGA

Member
Joined
Jan 1, 2021
Posts
5
Reaction score
15
Kwa hatua iliyofika Simba Sports Club kuingia hatua ya makundi CAF Champions League inatupa changamoto wapinzani na sisi tukae chini.

Tutafakari;Je, siku tukipata nafasi yakuwakilisha nchi je kikosi chetu kinaweza kutufikisha mbali cha msingi tu Yanga wajipange watengeneze kikosi bora chenye uwezo wa kushindana na timu kubwa Afrika kama Mamelod, Kaizer, Orlando, TP Mazembe, Al Ahly.

Kwa mawazo yangu Yanga kuna haja ya kuachana na Maiko Sarpong, Haruna Niyonzima, Carlos Carinho. Wasajili wachezaji wakubwa nawenye uwezo mkubwa kuzidi hao maana naona kama vile hawana mchango kwenye timu.
 
Tatizo linakuja wachezaji wengi wazuri wanataka team zinazoshiriki ligi ya mabingwa tayari na sio kungojea.. cha kufanya watani komaeni mwaka huu mchukue ubingwa hapo mtawapata wachezaji wazuri wazuri. LKN je mtaweza kuchukua ubingwa mbele ya Simba.
 
Mim naupeo mkubbwa wakuchambua soka ukiona naandika kitu si ushabiki nakama kuna media yoyote inataka mchambuz wa soka please contact me au niunganishe
 
Tatizo la Yanga ni Akili Tu, mengineyo ni Nyongeza tu

-Shabiki wa Yanga akikuta Shabiki wa Simba anaamini Simba inaweza kuwa Bingwa Africa anamuambia Wewe ni Kichaa.

-Yanga wakati anashiriki sana Club Bingwa utawasikia wanajitamba Kupanda Ndege wa kimataifa wanaita Simba wa Matopeni, sikuwahi kuona shabiki wa Yanga akizungumzia kuingia Makundi, robo final nk wao wanazungumzia Kupanda Ndege tu.
- Kitendo cha Mashabiki wa Yanga kupokea wapinzani wa Simba na kuwapa msaada ni ushahidi wa matatizo Ya Akili ya Yanga.

Yanga wakijirekebisha kwenye Mentality mengine yote yatakuja na tutaijenga Pamoja Tanzania yetu kisoka kama TP Mazembe na As Vita wanavyoijenga Congo yao kila leo
 
Na Simba waachane na Mugalu maana ni Sarpong mwembamba.
 
Hili la kupokea mashabiki wa timu pinzani inaonekana umeanza ushabiki 2019 Disemba, Yanga wanafanya Simba wanafanya.
 
Hili la kupokea mashabiki wa timu pinzani inaonekana umeanza ushabiki 2019 Disemba, Yanga wanafanya Simba wanafanya.
Tajiri anaweza kuwa anakunywa sana na pombe zisimharibie lakini Maskini pombe inaweza ikawa zinazidi kumuharibia maisha.

Sina hakika kama utaweza kuielewa hiyo sentensi.Sina namna bora ya kukuelewesha
 
Sio hao tu,hata mabeki wenu akina Lamine Moro mtakuwa mnapigwa red card kila mechi na kurudi kulia lia hapa mtandaoni.
Kumbuka kuwa hadi sasa mnabebwa na waamuzi tu maana si kwa mieleka ile uwanjani.
Kwa kikosi chenu cha sasa hamuwezi kucheza timu yoyote ya club bingwa mkashinda.Labda wachezeshe waamuzi wa kibongo
 
Umeongea ujinga na ndo maana mnajiita wekundu wa Msimbazi. Hayo makundi yanaanza Africa Yanga ndio timu ya kwanza kuingia hapa Tanzania.
 
Hata mimi nasubili jibu, labda anaongelea confederation.
Aisee kumbe tunabishana na watoto humu,Yanga anaingia makundi 1998 na ilikuwa robo finali siyo kama Sasa hivi,na kundi lake alikuwa na Raja Casablanca .
 
Tatizo linakuja wachezaji wengi wazuri wanataka team zinazoshiriki ligi ya mabingwa tayari na sio kungojea.. cha kufanya watani komaeni mwaka huu mchukue ubingwa hapo mtawapata wachezaji wazuri wazuri. LKN je mtaweza kuchukua ubingwa mbele ya Simba.
Labda ubingwa wa mapenzi siyo ligi kuu Tanzania bara.
 
Simba siyo timu inayopaswa kuingia hatua za makundi. Basi tu, mpira wetu wa Africa ndiyo ulivyo.
 
Toa sababu, manake ndio imeingia, na kwa taarifa yako tunaenda hadi nusu!! Imani, maandalizi, kupambana, Mungu mbele, ushirikiano na vitu vingine. Hizi ndio bunduki zetu
Simba siyo timu inayopaswa kuingia hatua za makundi. Basi tu, mpira wetu wa Africa ndiyo ulivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…