Yanga amkeni, Mchuzi wa Mbwa hunywewa ukiwa bado Wamoto

Yanga amkeni, Mchuzi wa Mbwa hunywewa ukiwa bado Wamoto

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Wafilipi 2:9

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Wafilipi 2:10

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Wafilipi 2:11
 
Kama ambavyo tayari imeshajulikana kwamba mwaka huu tuzo nyingi zitaenda Yanga (winner takes all)
Viongozi, mashabiki na wapenzi wa Yanga Afrika kataeni huu uhuni unaotaka kufanywa na Tff kwani waathirika wakubwa wa kusogezwa mbele kwa izo tuzo ni nyie..

Hebu jaribuni kuwaza nje ya box, wakati wa izo mechi za ufunguzi wa ligi ( ngao ya jamii) mkipoteza mechi iyo ya ufunguzi labda dhidi ya mtani wenu Simba na yeye ndio akabeba iyo ngao ya ufunguzi wa ligi, hizo tuzo zenu zitakuwa na maana gani?

Yaani mtapata wapi ujasiri wakushangilia tuzo za msimu ulioisha wakati wenzenu tayari wameanza kuvaa medali za ushindi wa msimu mpya ulioanza?

Pia endapo Aziz Ki atakuwa ameondoka Yanga na kusajiliwa na timu nyingine, je mtaweza kuhoji maamuzi ya Tff kumpa u MVP mchezaji mwingine tofauti na Aziz Ki? Kwa maana wakati huo mtakuwa mnamtetea mchezaji asiye mchezaji wenu?

TFF sio wapumbavu kupeleka mbele utoaji wa tuzo, wana agenda ya siri...

Suspending their individual reasoning because of group objectives Shauri yenu, babu onyango ndio nimeshawasanua hivyo
Siyo hivyo tu MVP Ina muongezea CV mchezaji huko anakokwenda, TFF wamelenga kuinyanyasa yanga na siyo vinginevyo Hawa TFF wanaahirisha kufikiri kwa nafsi kwaajili ya masilahi yao binafsi,ama kutumikia kundi Fulani, (suspending their individual reasoning because of group objectives),thus conflict of interest
 
Kwa nini imekuwa ghafla hivi? Kuna mtu nimesoma comment yake anasema mbona fainali zimehamishwa kutoka Babati kwenda Zanzibar na watu wamefurahi. TFF wanafanya makosa mengi ya kimsingi katika mpira wa Tanzania ila bahati nzuri wanabebwa na uwepo wa Simba na Yanga. Suala la tuzo siyo dharula mpaka ipelekee kukiuka kanuni walizo jiwekea.
 
ila GONGOWAZI sijui huwa mnawaza nini? Majuzi tu TFF wamebatilisha mechi ya fainali ya Kombe la Shirikisho la CRDB badala ya kuchezwa Manyara kama ilivyokuwa imepangwa awali sasa itachezwa Zanzibar. Sijasikia mkijilizaliza na wengi wenu mmefurahia maamuzi hayo. Ila hili la tuzo kusogezwa mbele hamlitaki mchana kutwa usiku kucha kujilizaliza.
Watu wa jukwaa la mapenzi mkija huku hua mnakua wapuuzi sana..Zipo nyuz lukuki humu kulalamika swala la Fainali kupelekwa zanzibar usikurupuke rudi huko Jukwaa lenu la kula Tunda kimasihara.
 
Back
Top Bottom