Yanga, Biashara United uwanjani leo kwa Mkapa, Kocha Nabi atoa kauli kuhusu mchezo huo

Yanga, Biashara United uwanjani leo kwa Mkapa, Kocha Nabi atoa kauli kuhusu mchezo huo

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Wanafainali wa michuano ya Kombe la FA msimu uliopita, Yanga, leo saa moja usiku watakuwa kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam kutafuta nafasi ya kutinga Hatua ya Robo Fainali wakati itakapocheza dhidi ya Biashara United kutoka mkoani Mara.

Kocha wa Yanga, Nasreddine Nabi alinukuliwa hivi karibuni akisema kuwa timu yake inafanya maandalizi ya mchezo huo Pamoja na mwingine wa Ligi Kuu Bara dhidi ya Mtibwa Sugar utakaochezwa Februari 23 kwenye Uwanja wa Manungu, Morogoro.

Biashara imekuwa na mwenendo wa kusuasua katika Ligi Kuu msimu huu.

FLn7kONWYAAhTvi.jpg
 
Asante Kwa Taarifa Mkuu Mabingwa Wa Kihistoria Nchini Leo Wataingia Uwanjani Kumkanyanga Vibaya Mno Biashara United (Wanajeshi Wa Mpakani).
 
Kila la heri Wananchi! Safari hii tunachukua vikombe vyote. Tulianza na Ngao ya Jamii.
 
Back
Top Bottom