Kama kawaida yangu kwanzia saa sita kamili siku za jumatatu hadi ijumaa uwa nasikiliza east Africa radio kipindi cha kipinga extra. Pale unakutana na mashabiki mbali mbali wa timu zetu hasa pendwa Simba na Yanga. Jana kulikua na mashabiki wa Yanga wakiongozwa na Jimy kindoki.
Sasa kulikua na mada juu ya mechi kati ya Yanga na Polisi Tanzania.
Kilichonifanya niandike ni vile vilio vya mashabiki wa Yanga juu ya muendelezo wa timu yao pendwa.
Kuna mmoja jina kapuni, Yeye alisema Yanga matokeo wanayopata yanasababishwa na viongozi waliopo , kwa sababu kuna watu ambao ndo wamesajili wachezaji wametengwa na timu. Namnukuu, "Sikiliza Bwana Goza( huyu ndo msimamizi wa kipindi) pale Yanga kuna wanachama ndo waliowasajili wachezaji, mfano yule Papy kasajiliwa na flani( jina kapuni) hata Hata kocha Zahera kaletwa na huyo mtu kipindi tunaangaika hatuna kocha na hatuna hela huyo ndo alimleta akamsajili Zahera.. Hata kuja kwa Haruna moshi msimu uliopita aliletwa na hao watu "
Sasa saizi hao wametengwa na viongozi waliopo.
Mara paa akaingia Jimy kindoki, Yeye ka mjumbe wa kamata ya uamasishaji akaulizwa kuhusu ilo, yeye akasema , yeye kama yeye hailewi ka ilo jambo lipo, akaendelea kusema inawezekana lipo yeye hawezi kujua kwa sababu ni la ndani, ila atalifanyia uchunguzi.
Pia akatoa maoni yake kua yeye anaona timu ya Yanga haifanyi vizr kwa sababu wachezaji wamechezewa( akimanisha wamerogwa) namnukuu " haiwezekani Leo inaibuka mchezaji huyu anafanya vizr Kesho mwingine. Ule Sio uwezo wa wachezaji wetu " akaendelea inawezekana wamechezewa humu humu ndani ( ndani ya Yanga) au ni hao majirani zetu ( akimanisha Simba)
Akaja mwingine yeye akasema toka jana ( ilikua alhamisi) nilisema kama wachezaji wetu wakitambua thamani ya Yanga tunashinda. Lakini angalia timu haimalizi mpira ikiwa Kwenye ile ile peak. Timu inacheza kipindi cha kwanza vzri , cha pili hivyo kabisa.
Kilichosabisha nilete hii mada ni hizi hoja tatu hasa ya kwanza na ya pili.
Moja, je, ndani ya Yanga kuna mgogoro ndo unasabibisha timu isipate matokeo? Afu inakuwaje inakuaje ndani ya timu baadhi ya wachezaji wanamilikiwa na watu flani na si timu hadi kocha wa timu?
Pili, Je wachezaji wa Yanga wamerogwa ka alivyosema Jimy kindoki ndo sababu ya Yanga kutopata matokeo?
Tatu, Je, ni kweli wachezaji wa Yanga hawajui ukubwa wa timu ya Yanga ndo mana hawajitumi dakika zote tisini ?
Nini maoni mwanajamii forum?
Sasa kulikua na mada juu ya mechi kati ya Yanga na Polisi Tanzania.
Kilichonifanya niandike ni vile vilio vya mashabiki wa Yanga juu ya muendelezo wa timu yao pendwa.
Kuna mmoja jina kapuni, Yeye alisema Yanga matokeo wanayopata yanasababishwa na viongozi waliopo , kwa sababu kuna watu ambao ndo wamesajili wachezaji wametengwa na timu. Namnukuu, "Sikiliza Bwana Goza( huyu ndo msimamizi wa kipindi) pale Yanga kuna wanachama ndo waliowasajili wachezaji, mfano yule Papy kasajiliwa na flani( jina kapuni) hata Hata kocha Zahera kaletwa na huyo mtu kipindi tunaangaika hatuna kocha na hatuna hela huyo ndo alimleta akamsajili Zahera.. Hata kuja kwa Haruna moshi msimu uliopita aliletwa na hao watu "
Sasa saizi hao wametengwa na viongozi waliopo.
Mara paa akaingia Jimy kindoki, Yeye ka mjumbe wa kamata ya uamasishaji akaulizwa kuhusu ilo, yeye akasema , yeye kama yeye hailewi ka ilo jambo lipo, akaendelea kusema inawezekana lipo yeye hawezi kujua kwa sababu ni la ndani, ila atalifanyia uchunguzi.
Pia akatoa maoni yake kua yeye anaona timu ya Yanga haifanyi vizr kwa sababu wachezaji wamechezewa( akimanisha wamerogwa) namnukuu " haiwezekani Leo inaibuka mchezaji huyu anafanya vizr Kesho mwingine. Ule Sio uwezo wa wachezaji wetu " akaendelea inawezekana wamechezewa humu humu ndani ( ndani ya Yanga) au ni hao majirani zetu ( akimanisha Simba)
Akaja mwingine yeye akasema toka jana ( ilikua alhamisi) nilisema kama wachezaji wetu wakitambua thamani ya Yanga tunashinda. Lakini angalia timu haimalizi mpira ikiwa Kwenye ile ile peak. Timu inacheza kipindi cha kwanza vzri , cha pili hivyo kabisa.
Kilichosabisha nilete hii mada ni hizi hoja tatu hasa ya kwanza na ya pili.
Moja, je, ndani ya Yanga kuna mgogoro ndo unasabibisha timu isipate matokeo? Afu inakuwaje inakuaje ndani ya timu baadhi ya wachezaji wanamilikiwa na watu flani na si timu hadi kocha wa timu?
Pili, Je wachezaji wa Yanga wamerogwa ka alivyosema Jimy kindoki ndo sababu ya Yanga kutopata matokeo?
Tatu, Je, ni kweli wachezaji wa Yanga hawajui ukubwa wa timu ya Yanga ndo mana hawajitumi dakika zote tisini ?
Nini maoni mwanajamii forum?