Yanga fanyeni haraka mumrudishe J.Abdul

Yanga fanyeni haraka mumrudishe J.Abdul

Abby Newton

JF-Expert Member
Joined
Nov 12, 2017
Posts
1,252
Reaction score
2,253
Kwa namna nikivyoiona Simba ikicheza jana, kwa ile speed na ujanja ujanja wa akina Morrison, Micksone, Bwallya na wengineo ni dhahiri yule dogo aliyetoka Mtibwa A.Shomari hatoweza kupambana nao. Uzoefu ni kitu cha muhimu.

Nawashauri viongozi wa Yanga aka Uto.watafakari tena na ikibidi wamrudishe haraka J.Abdul haraka kundini,la sivyo kuna balaa linaweza kuwakuta tar.18.10.2020. Abdul bado ni mchezaji mzuri hasa akikutana na wachezaji wazuri maana ye ni mtaalamu wa kumwaga maji.
 
Yanga sijui tu wamelogwa na nani.wameacha wachezaji wazuri sana kama J.Abduli,Ngasa.hata Papaa Molinga na Yondani ni wachezaji wazuri tu.
Yanga mchezaji akidai stahiki zake anakuwa mbaya hana nidhamu.mpira ni pesa sio ujanjaujanja.
 
Huyu Micksone ni mchezaji wa timu gani?
 
Daah kweli aisee hii Simba kwa jinsi nilivyoiona jana wanaweza kuja kutupiga 5 kama kipindi kile, jamaa kikosi chao kinatisha.
Timu yangu Yanga tufanye kweli kuepuka aibu za kujitakia.
 
Acha akili za kukalili kaondoka CR7 madrdid ijekuwa yondani au juma?? Kama unaweza wasajili wewe
 
Daah kweli aisee hii Simba kwa jinsi nilivyoiona jana wanaweza kuja kutupiga 5 kama kipindi kile, jamaa kikosi chao kinatisha.
Timu yangu Yanga tufanye kweli kuepuka aibu za kujitakia.
Kabisa,km Juma Abdul akiongezwa walau kikosi kitabalance kimtindo. Yanga bado inatia shaka sana sehemu ya ulinzi kulia na kushoto.
 
Yanga sijui tu wamelogwa na nani.wameacha wachezaji wazuri sana kama J.Abduli,Ngasa.hata Papaa Molinga na Yondani ni wachezaji wazuri tu.
Yanga mchezaji akidai stahiki zake anakuwa mbaya hana nidhamu.mpira ni pesa sio ujanjaujanja.

Hao wote ulio waacha wameondoka pale Utopoloni FC sio kwa sababu za kuachwa na timu, Bali ni kwasababu za kushindwana katika maslahi ya malipo.

Nadhani ni kheri wameona waachane nao ili kuepuka mambo ya kugoma na kudaiana mishahara huko mbeleni pale ambapo klabu itakwama kifedha kuweza kuwalipa mishahara.

Halafu sidhani kama ndio wamekwisha maliza suala la usajili, kwa taarifa zilizopo za ndani inaonyesha bado hawajakamilisha zoezi.
 
Acha akili za kukalili kaondoka CR7 madrdid ijekuwa yondani au juma?? Kama unaweza wasajili wewe
Nadhani ndio wale wale waliokuwa wakiamini kuwa kuondoka kwa Emmanuel OKWI kungeleta mtikisiko mkubwa sana klabuni Simba.
 
Kwa namna nikivyoiona Simba ikicheza jana,kwa ile speed na ujanja ujanja wa akina Morrison,Micksone,Bwallya,na wengineo ni dhahiri yule dogo aliyetoka Mtibwa A.Shomari hatoweza kupambana nao. Uzoefu ni kitu cha muhimu.

Nawashauri viongozi wa Yanga aka Uto.watafakari tena na ikibidi wamrudishe haraka J.Abdul haraka kundini,la sivyo kuna balaa linaweza kuwakuta tar.18.10.2020. Abdul bado ni mchezaji mzuri hasa akikutana na wachezaji wazuri maana ye ni mtaalamu wa kumwaga maji.
Kweli kabisa, pia Jaffary na Yondani.
 
Kwa namna nikivyoiona Simba ikicheza jana,kwa ile speed na ujanja ujanja wa akina Morrison,Micksone,Bwallya,na wengineo ni dhahiri yule dogo aliyetoka Mtibwa A.Shomari hatoweza kupambana nao. Uzoefu ni kitu cha muhimu.

Nawashauri viongozi wa Yanga aka Uto.watafakari tena na ikibidi wamrudishe haraka J.Abdul haraka kundini,la sivyo kuna balaa linaweza kuwakuta tar.18.10.2020. Abdul bado ni mchezaji mzuri hasa akikutana na wachezaji wazuri maana ye ni mtaalamu wa kumwaga maji.
We kumbuka yanga wana no 2 boxer,hawana shida ya juma abdul
 
We kumbuka yanga wana no 2 boxer,hawana shida ya juma abdul
Boxer sio mzuri kwenye kushambulia. Mpira wa kisasa beki wa pembeni ndio msingi wa kutengeneza mashambulizi. Lazma beki awe na speed,uwezo wa kupiga chenga,kupiga basi za haraka na kupiga cross mujarabu. Mwangalie Kapombe,Shabalala au Kangwa wa Azam. Nazani umenielewa
 
Boxer sio mzuri kwenye kushambulia. Mpira wa kisasa beki wa pembeni ndio msingi wa kutengeneza mashambulizi. Lazma beki awe na speed,uwezo wa kupiga chenga,kupiga basi za haraka na kupiga cross mujarabu. Mwangalie Kapombe,Shabalala au Kangwa wa Azam. Nazani umenielewa
Uliwahi kumuona dogo akiwa anacheza kabla hajapata majeruhi mwaka jana? Unajua ni kwanini ilibidi Juma abdul asubiri benchi mechi mfululizo!? Unakumbuka kazi iliyokua anaipiga kwenye kikosi cha kili stars CHAN!?

Sema haijulikani kama atarudi na moto uleule. Ila yule dogo ni zaid ya J abdul.
 
Yanga sijui tu wamelogwa na nani.wameacha wachezaji wazuri sana kama J.Abduli,Ngasa.hata Papaa Molinga na Yondani ni wachezaji wazuri tu.
Yanga mchezaji akidai stahiki zake anakuwa mbaya hana nidhamu.mpira ni pesa sio ujanjaujanja.
Ukitaka uonekane mbaya dai chako. Utopolo wana laana ya kuwadhulumu wachezaji wao na watapata tabu sana miaka kadhaa ijayo. Tutawakera sana
 
  • Thanks
Reactions: Tui
Back
Top Bottom