kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Siyo jambo la ajabu kocha kufukuzwa kwenye club timu ikikosa matokeo viwanjani, lakini hii ya Zahera kushindwa kuifunga Pyramids na Ruvu kustahili kufutwa kibarua hainiingii akilini.
Pyramids ina uwezo mkubwa uwanjani na nje ya uwanja kuliko timu yoyote kwenye ukanda wa CECAFA. Yanga ndiyo timu Tanzania ambayo wachezaji na benchi la ufundi wanaidai club hela zao. Yanga ndiyo timu ambayo ina wachezaji ambao pamoja na kuonekana kwenye club ya Yanga, lakini hawaruhusiwi kucheza mashindano ya kimataifa. Yanga ni timu ambayo ina wachezaji muhimu wagonjwa kwa muda mrefu. Yanga ilikuwa na wachezaji muhimu wenye kadi za njano na nyekundu kuelekea mechi ya marudiano na pyramids huko Misri.
Hivyo, hata umlete Zenadine Zidane Yanga lazima Yanga ingefungwa na Pyramids tu. Sawa na Man U na Arsenal kuwafukuza Mourihno na Wenger lakini vipigo vikaendelea kubaki palepale.
Nadhani viongozi wana shida nyingine na Zahera, siyo kufungwa na Pyramids na Ruvu Shooting.
Nadhani tabia ya Zahera ya kupenda kuongea na kuanika ukweli ndani ya club hatujaizoea.
Pyramids ina uwezo mkubwa uwanjani na nje ya uwanja kuliko timu yoyote kwenye ukanda wa CECAFA. Yanga ndiyo timu Tanzania ambayo wachezaji na benchi la ufundi wanaidai club hela zao. Yanga ndiyo timu ambayo ina wachezaji ambao pamoja na kuonekana kwenye club ya Yanga, lakini hawaruhusiwi kucheza mashindano ya kimataifa. Yanga ni timu ambayo ina wachezaji muhimu wagonjwa kwa muda mrefu. Yanga ilikuwa na wachezaji muhimu wenye kadi za njano na nyekundu kuelekea mechi ya marudiano na pyramids huko Misri.
Hivyo, hata umlete Zenadine Zidane Yanga lazima Yanga ingefungwa na Pyramids tu. Sawa na Man U na Arsenal kuwafukuza Mourihno na Wenger lakini vipigo vikaendelea kubaki palepale.
Nadhani viongozi wana shida nyingine na Zahera, siyo kufungwa na Pyramids na Ruvu Shooting.
Nadhani tabia ya Zahera ya kupenda kuongea na kuanika ukweli ndani ya club hatujaizoea.