Yanga hii ni tofauti na imekamilika kila idara. Haina nia wala sababu ya kufungwa jijini Tunis,Tunisia. Yanga ina kikosi imara na wachezaji wenye ari na wasiotishwa na historia. Yanga hii itaitoa kidedea Tanzania kisoka kimataifa kuanzia mwaka huu.
Leo Yanga imetwaa ubingwa wa VPL kwa mara ya 25. Ubingwa huu utakuwa chachu kwa Yanga kupambana na kujipaisha zaidi. Etoile du Sahel anafungika na hana upekee wowote kisoka ambao Yanga hawezi kuwa nao.
Yanga itawaumbua wakosoaji wake kwenye mechi ya marudiano. Etoile watatoka vichwa chini wasiamini matokeo. Yanga hawajafungwa Taifa na inahitaji sare ya magoli tu kusonga. Yatatokea yaliyotokea kwa Chelsea dhidi ya PSG katika UCL