Yanga ina matatizo makubwa kimataifa

👆
Comment iyo hapo yenye majibu mubashara kabisa.

Simba na Yanga wanaokota okota wachezaji mwisho wa siku awawezi kukupa kilicho bora.
 
Uzi wako naona unahusu Yanga tu, wakati Simba ina warefu wawili ambao ni Kanoute na Bocco, lakini juzi kuna picha ilitembea mtandaoni wakitembea na jamaa wa Horoya waliyekuwa wanamfikia MABEGANI….!!

Kwahyo, hoja ya VIMO VYA WACHEZAJI, kama ni tatizo basi ijikite kwa timu zote mbili
 
Soma mistari yangu miwili ya mwisho utaona nilichokiandika kuhusu Simba.
 
Shida sio urefu wala ufupi wa mabeki. Tatizo ni kwamba huko kimataifa hakuna Tigopesa wala referee Arajiga. Over
 
SImba juzi ameshinda dhidi ya horoya
 
Yanga wanatakiwa waache bahasha wacheze mpira halisi ili wapate kipimo sahihi

Propaganda za unbeaten za mchongo hazisaidii kwenye mashindano ya Kimataifa

Yule kocha team zote alizofundisha alifukuzwa kwasababu alikuwa hafanyi vizuri kimataifa wazee wa beach kidimbwi wakaona wamepata Guardiola kumbe professor wa mchongo kama babu tale.



Sent from my SM-N950F using JamiiForums mobile app
 
Nabi ana tatizo la "Capacity Limitation" uwezo wake umefikia mwisho na hayuko vizuri kimbinu.

Mfumo wake wa 4-2-3-1 unafaa tu kama una aggressive midfielders ambao kwa bahati mbaya Yanga haina hali ambayo inamfanya mara nyingi Mayele awe joka la kibisa.

Yanga wakiendelea na viungo hao hao na mfumo huohuo basi wakipata hata nafasi ya tatu kwenye kundi lao itakuwa ni mafanikio makubwa sana kwao.

Sioni kama Nabi ana uwezo wa kuipeleka Yanga mbali kwa sababu ya uwezo wake mdogo kimbinu.
 
Acha unafiki
Lipeni mshahara mizuri kwa wazawa wanaojituma

Game ya jana Feisal angepiga yale mashuti yake ya mbali yangeweza kuisaidia timu

Mnamuweka Kisinda mlitegemea nini?

Na jumamosi tunaingia mzigoni tena, sasa rufia makosa yako kama ulivyo fanya juzi, washangilie Raja halafu likukute la kukukuta jumapili yake
 
Nilichogundua wengi wetu sio watu wa mpira ndio maana mnaomgea kile mnachokijua sio mpira ulivyo.
1.Tujifunze kuzipa moyo timu zetu hakuna mtu kutoka nje atakuja kutusaidia ili zifike tunapotaka.
2.Hivi kwa kauli kama hizi unafikiri mfano huyo mwekezaji akijitoa utawaona wapi hao akina mayele,aziz ki ,kisinda,Nabi nk basi wewe njoo uwekeze wewe ili tukusifu...watanzania jifunzenu kusifu cha kwenu acheni ushamba wa kushabia vya wageni...Yanga na Simba hazijacheza vibaya kihivyo hadi kuipondea kiachi hicho ..mchezo wa mpira na magoli na tumefungwa ugenini nao wakija hapa kwa mkapa tutafunga
 
Bado najiuliza ile orodha iliyoiweka ligi ya TZ ya Tano Afrika iliandaliwa wapi!?
 
Nonsense
 
hebu toa takwimu za moloko kwenye hii mechi ya monastir kama wewe ni mkweli
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…