Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hili ninalosema ni jambo ambalo wengi hawatataka kukubaliana nalo lakini ntalisema ili kuokoa jahazi katika soka la Tanzania.Mimi binafsi ni mpenzi wa mpira wa miguu na michezo kadhaa toka mwaka 1990. Naufaham mpira wa tz kwa kiasi flan na huwa sipendi kuwa mnafiki kuwa siwezi shabikia mpira wetu nikashabikia wa england, spain n.k though huko pia nina team nazipenda. Ni muda mrefu klabu ya Dar Young African imekuwa ikijitahidi kusajili wachezaji wa kimataifa kwa gharama kubwa magazetin n.k ingawa ukweli pia kuna wachache tunaufaham. Ni jambo jema kuwa na team nzuri na tunaiombea yanga iwe team nzuri. Lakin ninalotaka kusema ni kuwa gharama inazotumia yanga kusajili basi ziwe ni chanzo cha ushindi uwanjani na si tena kutumia pesa nying ili kushinda. Jana kwenye uzi wa live updates nlisema kuwa kuna mdau alinambia Yanga itashinda bao nne. Huyo alikuwa ni mmoja ya wachezaji wa team ya JKT Ruvu aliyesema bila kusita kuwa wanaingia uwanjani tayari wakiwa wanajua kuwa Yanga inatakiwa ishinde nne na kuwa iwe iweje lazima mchezaji flan naye ashinde ili awe na goal nying pia. Mchezaji huyo alinambia kuwa anajua kwa nini yanga itashinda nne na yeye hana namna ya kuzuia kwa kuwa anajua wahusika ni akina nani. Aliomba nisimtaje ila niwaambie wana kandanda kuwa matokeo tayari yanajulikana hivyo wasiwe na mshawasha na pambano hilo. Nliumia sana kwa sababu napenda mpira wa tanzania ukue. Manji anatuharibia soka letu kwa kutafuta utukufu.
Hii mada yako mdau ina tuhuma nzito tatizo ni uthibitisho hakuna! mimi kama mimi niliiangalia ile mechi mwanzo mwisho na kwa uelewa wangu wa mpira, matokeo ya ile mechi hayakupangwa!
Hofu yangu inawezekana huyo mchezaji alikuambia tu kama njia ya kujihami. Golikipa Shaaban Dihile alifanya kazi ya ziada kuokoa magoli mengi ya wazi siku ile na hata wachambuzi wa Azam tv walimsifia kwa hilo!
Achilia hilo, Jkt Ruvu inawezeje kupata ujasiri wa kuuza mechi ilhali iko mkiani mwa msimamo wa ligi na kuna uwezekano wa kushuka daraja! mbaya zaidi ni mwaka wa ngapi huu inafungwa na Yanga? tangu alipokuwepo Minziro taarifa hizi zilisikika kisa Minziro ni Yanga damu!
Tuachane na hilo, tangu msimu wa ligi uanze Jkt Ruvu imefungwa mechi ngapi? hawakufungwa 5-1 na Mgambo? tena uwanja wao wa nyumbani? au nayo waliuza kwa Mgambo fc? walifungwa pia na Simba!
Ambacho tunatakiwa kujifunza ni kwamba Jkt Ruvu ni timu ya jeshi na inapitia michakato mbalimbali mfano wakati flani baadhi ya wachezaji wake kwenda depo katikati ya msimo, na hata wakishuka daraja ni kazi nyepesi tu kwao kupanda tena msimu unaofwata kama ndugu zao Ruvu Shooting hivyo hawana cha kupoteza. Tuamini katika mpira huwa kuna upepo mbaya unaweza kuipitia timu na ikafanya vibaya kama ilivyo kwa Chelsea sasa na Mtibwa fc msimu uliopita.
Nimeona na mimi nitoe maoni yangu kama mdau wa michezo. Hata Yanga kama zilivyo timu nyingine za mpira wa miguu inaweza kushinda, kutoa sare na hata kufungwa na ndio maana ilifungwa 2-0 na coastal union na coast naye akafungwa na ndanda mechi iliyofuata
Cha msingi timu zote za ligi kuu zijipange kwa matokeo mazuri na kuondoa hii dhana kupanga matokeo ingawa siwezi kukataa lolote linaweza kutokea ktk mpira.
watu wanakataa kwa sababu ya ushabiki. ila anayosema sodoku ni kweli na ni kweli ushahidi upo. tunafaham kuna wachezaji wanapewa pesa wapate cards nyekundu au watolewe, tunafaham kuna wachezaji wanapewa pesa wacheze rafu au washike mpira eneo lao la hatari wasababishe faulo. tunafaham mechi ile ya simba na yanga simba ikafungwa mbili kiongozi mmoja wa simba alimhonga mwamuzi ili simba ifungwe apate sababu ya kumfukuza kocha. tunafaham na mwamuzi alionesha ishara mapema kabisa. tunafaham kuwa azam waliipatia pesa nzuri african sports waifunge yanga huko tanga. tunafaham vizuri tu. tunafaham yanga ilifanya nini kuhakikisha inasawazisha huko mbeya kwa prison. simba yanga zina wachezaji wapenzi kwenye team pinzani.zina makocha wapenzi kwenye team pinzani. na ndo maana mwambusi alikuwa nauza kila mechi ya mbeya city kwa yanga ni mpenzi sana wa yanga. tunafaham kuna viongoz wa azam mashabiki wa simba na wa yanga. haya mambo anayozungumza Sodoku ni halisi. mechi zinapangwa ligi kuu na ligi daraja la kwanza.wachezaji,viongozi na makocha wanafanya hii michezo kuhujumu team na kuharibu soka la tanzania. na pia wanahujumiana wenyewe kwa wenyewe. MSIBISHE KAMA HAMJUI NA MSILETE USHABIKI HUMU NDANI. KAMA HAMJUI ULIZENI watu wana matokeo ya mechi mara nyingine kabla hata mechi hazijaanza.