Mtanzanias
JF-Expert Member
- Jul 30, 2021
- 1,747
- 3,725
Nafikiri ni mda wa wale wanaoendelea kushupaza shingo kukubaliana na ubora wa yanga kwa sasa,,unaweza ukawa na chuki binafsi lakini aziwezi kukusaidia bali zitaendelea kukuumiza moyoni na kukusababishia magonjwa ya moyo, mechi ya leo dhidi ya geita ambayo imekuwa na ubora mkubwa uwanjani yanga kiufundi wamekwenda kucheza mpira wa matokeo objective football kulingana na mazingira ya uwanja, licha ya majeruhi kuwa wengi timu yenye viashiria vya kubeba ubingwa inashinda mechi kwenye mazingira yoyote yale na ndivyo ilivyokuwa leo unamaliza biashara mapema unaangalia mbele ya safari kimipango zaidi, upana wa kikosi ni silaha nyingine inayoibeba yanga msimu huu angalia leo imewakosa wachezaji muhimu kama djuma shaban, kharid aucho,saido ntibanzokiza, lakini back up yao yupo salum abubakari, zawadi mauya, Dickson ambundo, farid musa kwaiyo yanga msimu huu anao uwezo wa kumaliza ligi bila kufungwa aiwezi kuwa ajabu ata kidogo kulingana na takwimu, kabakiza mechi 3 mikoani zilizobaki anacheza dar, pongezi ziende kwa viongozi walioumiza vichwa kufanya usajili wa nguvu na wa malengo👏👏👏👏👏👏