Yanga kama Mwadui hucheza kumkamia Simba

Yanga kama Mwadui hucheza kumkamia Simba

kibaravumba

JF-Expert Member
Joined
Dec 21, 2012
Posts
6,634
Reaction score
7,015
Mimi nikiwa mwana Simba napenda kuwapongeza wachezaji wetu kwani walijitahidi kutengeneza nafasi sana hasa kipindi cha pili lakini bahati haikuwa yetu.

Yanga kama akina Mwadui,Prison,na wengineo kama hawa,hupata faraja sana kuifunga Simba kwani wanajua ukubwa wake.
Wao huikamia sana na wakipata goli moja hutumia nguvu zote kulilinda.

Hawa hawa yanga wamepata nafasi nyingi sana kucheza kimataifa kuliko Simba lakini Simba ndiye anabaki kuwa timu yenye mafanikio zaidi kuliko timu yoyote hapa nchini kimataifa.Hapa ndio tunapima ubora wa timu na si mechi ya derby.

Yote kwa yote niwapongeze watani kwa kufanikiwa kuikamia mechi na kufunga goli moja.
 
Inaonesha hujui maana ya Derby.. Dabi haiwezi kuwa lelemama hata kama timu Fulani iko mkiani mwa ligi.. Yanga imecheza ikijua wako kwenye dabi na Si mazoezi..
Nijijibu kulingana na heading yako.. Huo utopolo wako wa chini sijasoma niwie radhi kwa hilo
 
Hawa ndio wale walimuamini zeruzeru eti watashinda ili wabaki uwanjani dakika tano za kushangilia. Yule zeruzeru amewaponza [emoji169][emoji172][emoji169][emoji172]
Duh!Kuna watu mnajiamini sana na maumbile yenu.Ni kama mlijadiliana na Mungu muwe hivyo mlivyo.

Hata hivyo hapa naongelea kweli( facts) hivyo usiumie sana.Yanga wamepata nafasi nyingi sana kimataifa kuliko Simba, lakini takwimu zinaonesha Simba ni bora kimataifa kuliko timu yoyote hapa nchini
 
Nalazimika kukubali yanga wanewekeza zaidi kwenye kamati ya ufundi kuliko benchi la ufundi.

Ndiyo maana imejaa wazee vigagula tupu wakati Simba imejaa wazee wasomi
Unalo tu hilo hayo mengine ni kujipoza tu kubali Yanga dume lenu tu .mnahesabu lakini
 
Tumepigwa tungepiga tusingeandika porojo.
Tulikuwa tunaongea sana na hii ni jadi yetu hasa watani wa jadi...hakuna aliyemkamia mwenzake tuligongwa vyema sana jana.

Watani wangelikamia game tusingelitoboa kabisa jana kwa ule mshtuko wa Mauya.
 
Kama Yanga ni zero tu, mlishindwa nini ku score magoli mengi? Kagoli kamoja then mnarudi nyuma
 
Mimi nikiwa mwana Simba napenda kuwapongeza wachezaji wetu kwani walijitahidi kutengeneza nafasi sana hasa kipindi cha pili lakini bahati haikuwa yetu.

Yanga kama akina Mwadui,Prison,na wengineo kama hawa,hupata faraja sana kuifunga Simba kwani wanajua ukubwa wake.
Wao huikamia sana na wakipata goli moja hutumia nguvu zote kulilinda.

Hawa hawa yanga wamepata nafasi nyingi sana kucheza kimataifa kuliko Simba lakini Simba ndiye anabaki kuwa timu yenye mafanikio zaidi kuliko timu yoyote hapa nchini kimataifa.Hapa ndio tunapima ubora wa timu na si mechi ya derby.

Yote kwa yote niwapongeze watani kwa kufanikiwa kuikamia mechi na kufunga goli moja.
Kama unajua mtu anakukamia na wewe si umkamie yaishe? kwenye soka ni ushamba kuamini mtu anakukamia na wewe ukalegea tu, ndio maana huwezi kumkuta kocha wala wachezaji wanasema wamefungwa kwasababu walikamiwa, nyambaaaaafu
 
Inaonesha hujui maana ya Derby.. Dabi haiwezi kuwa lelemama hata kama timu Fulani iko mkiani mwa ligi.. Yanga imecheza ikijua wako kwenye dabi na Si mazoezi..
Nijijibu kulingana na heading yako.. Huo utopolo wako wa chini sijasoma niwie radhi kwa hilo
mkuu dabi maana yake nini? liver na man u sio dabi lakini shughuli si unaiona, kmc na yanga ni dabi lakini mbona hakuna jipya
 
Duh!Kuna watu mnajiamini sana na maumbile yenu.Ni kama mlijadiliana na Mungu muwe hivyo mlivyo.

Hata hivyo hapa naongelea kweli( facts) hivyo usiumie sana.Yanga wamepata nafasi nyingi sana kimataifa kuliko Simba, lakini takwimu zinaonesha Simba ni bora kimataifa kuliko timu yoyote hapa nchini
Simba haina ubora wowote ule sema upepo umewapitia tu. Kwa Tanzania mpira bado sana kwa sababu hakuna uwekezaji wowote wa maana zaidi ya kujaza wachezaji wa nje tena wazee alafu unajisifu. Tanzania hakuna timu zenye uwekezaji wa maana kuanzia viwanja bora vya mechi, miundombinu bora ya mazoezi kwa wachezaji, vituo bora vya michezo kwa vijana na watoto kwa maendeleo ya mpira, uongozi wenye sifa, malengo na ushubutu, rasilimali zote muhimu kama fedha bila kutegemea wafadhili unless other wise mpira na michezo Tanzania ni bora liende kwasababu bado michezo haijawa biashara yenye kuchangia uchumi kwa mapana zaidi
 
Back
Top Bottom