Yanga kubandua nembo ya Haier kimkataba

Kwanza bonus huwa inatolewa kwa kufikia target flani na pale hiyo target ikifikiwa inakua sio reward tena bali inakua lazima na ndo maana inaandikwa kwenye mkataba.
Huo ulazima unakuja baada ya kuahidiwa

Ahadi ni deni

Usipo ahidiwa hutapata hiyo nguvu ya ku demand

Na ndio maana ipo mikataba imewekwa bila offer ya bonus lakini ikatokea ume achieve kitu kikubwa kumfurahisha mfadhili basi utakuta umepewa reward ambayo haikuwepo kwenye mkataba
 
Yanga kuingia makundi kunaipa mileage Sportpesa in terms of numbers of matches to bet.
Na mechi hzo siyo kama za Yanga na kurugenzi ambapo odds zake zipo rahisi.
So, of course kuna mechi sita za high profile ambazo betting inahitajika na hiyo inaongeza pato la Sportpesa by far by just being associated with Yanga.
 
Hebu acha ujuaji wa kijinga
Mbona maelezo yangu hapo juu yanaeleweka kabisa sasa hapa hueleweki unapinga au unaelezea nini?

Bonus imewekwa kwenye mkataba kabisa kwamba nikishika nafasi ya 1 napata hiki sasa nimepata nafasi hiyo bonus hapo ni lazima inipewe sio reward tena.
 
Yanaeleweka na nani?

Yangu mimi ndio hayaeleweki? Mbona unapinga?

Unaelewa maana ya bonus kwanza?

Kuweka bonus kwenye mkataba ndio kumeihalalisha ionekane ni ya lazima lakini ingewezekana kusaini mkataba bila ya bonus na mkaendelea kuchukua pesa za uwekezaji tu
 
Mileage kwa namna gani wakati nembo hai display kwenye Jersey?
 
Kwahiyo hapa unachobisha nini sasa?
 
Soka la Tanzania.
Wananchi wanamiliki timu kubwa mbili na hazijawahi kupoa kwenye hekaheka za kijinga jinga

Wananchi hao hao wanazo timu wanazoshabikia kwa mahaba niue zilizopo ligi za ulaya na huwasikii wakiandamana kutaka uchaguzi wala kutimuliwa kwa benchi la ufundi.

Serikali imeona soka hili la bongo kwa stayle hii lina mashiko makubwa sana hivyo imekaa mkao wa kuwakwamisha wawekezaji wanaotamani kuliendeleza soka la Bongo kitija
 
Ingewezekana na pia isingewezekana. Usielemee upande mmoja.
Unapotoa proposal, unajumuisha kila kitu, if that proposal is attractive (meaning the sponsorship package is attractive) watu watatia saini.

Ila kama package siyo attractive, watu watakataa. So, it was imperative for Sportspesa kuweka bonus ili kuifanya package iwe attractive.

Kama wachina wameweka 1.5B kwa mechi sita, imagine wanaweza kuweka kiasi gani kwenye ligi nzima ambayo ni mechi zaidi ya 30 pamoja na ASFC. Sportpesa haimfanyii Yanga favor wakitaka waondoke.

Yanga sasa hivi ni bussiness, siyo mambo ya serikali. itabidi tuondoke huko, bussiness is bussiness.
 
Mileage kwa namna gani wakati nembo hai display kwenye Jersey?
Sportspesa ipo associated na Yanga. Kuna kundi kubwa sana la washabiki wanaotumia Sportpesa just because they are associated with Yanga. Thats a guaranteed mileage.

Kuna washabiki wameacha kubet MBet kwa sababu ya Simba. Sports fans are a very loyal consumer group na wana tabia hizo, usibishe tu mambo kujiridhisha.

Kuwa na nembo kifuani au kutokuwa, watu wanajua Sportpesa ni mdhamini mkuu wa Yanga. Sasa kama hutakuwa na nembo kifuani (Yaani huruhusiwi), basi usitupangie.
 
Nimekuuliza SportPesa wanapataje mileage kwenye Jersey ambayo hakuna nembo yao?

Nimekushangaa hapo kwenye paragraph ya mwisho ulipoandika "Kuwa na nembo kifuani au kutokuwa, watu wanajua Sportpesa ni mdhamini mkuu wa Yanga"

Hivi ni wewe umeandika hicho kitu ukiwa na utimamu wako kabisa?

Anyway

Unaelewa hii Jersey mpya imepewa ukubwa na hadhi ya juu kuliko Jersey ya mdhamini mkuu?

Means ipo kwenye nafasi kubwa ya kuifunika jersey ya zamani yenye nembo ya SportPesa

Na mashabiki tunafahamu jinsi wanavyopenda kuwa updated, mpaka saizi tayari inaonekana kuvaa jersey yenye nembo ya SportPesa ni kuwa outdated

Haier anaenda kunufaika kupitia mgongo wa SportPesa tena kwa pesa ndogo tu aliyowekeza.
 
Hao Utopolo labda wametengeneza crisis ili wapate upenyo wa mjadala wa kimaslahi toka sportpesa kwenye eneo ambalo wanahisi hawakuwa makini au wanadhulumiwa.
Crisis intended for recouping an oversight interests.
 
Dar es Salaam. Uongozi wa SportPesa mapema leo Februari Mosi, 2023, umetoa taarifa ya kusikitishwa na uongozi wa Yanga kukiuka makubaliano ya kimkataba na kuzindua jezi mpya zenye nembo ya mdhamini mwingine.

Mwananchi Digital imefanya jitihada ya kuutafuta uongozi wa Yanga kutolea ufafanuzi suala hilo na kumpata kiongozi mmoja wa juu ambaye hakutaka jina lake litajwe na kusema wameshangaa hatua ya wadhamini wao wakuu, SportPesa kulalamika juu ya uamuzi huo, na kwamba mapema waliwatafuta kwa nyakati tofauti na kuwaeleza juu ya nia yao hiyo.

Kiongozi huyo alisema kila hatua ya kuingia mkataba wa mechi sita na kampuni ya vifaa vya kielektroniki ya Haier waliwajulisha SportPesa ingawa hawakuonyesha kukubaliana na mdhamini huyo.

"Tuliwatafuta mara nyingi kuanzia Novemba mwaka jana baada ya kufuzu hatua ya makundi, tukawaambia kimaandishi kwamba tunatafuta namna ya kuisaidia klabu kwa sababu kubwa kuwa wao hawataruhusiwa kikanuni.


"Wakatuambia tuwapelekee uthibitisho kwamba CAF hawairuhusu SportPesa, tukamtuma mtu wetu CAF akapewa uthibitisho huo na tukarudi na kuwasilisha kwao, hawakujibu, tukawakumbusha hawakujibu.

"Baada ya muda, mwaka huu mapema tukawajulisha kwamba bado tunawatambua wao kuwa wadhamini wetu wakuu, lakini tumepata mdhamini maalumu ambaye hana mgongano nao wa kimaslahi ili tumtumie kwenye hizi mechi sita tu za hatua ya makundi," alisema kiongozi huyo.

Yanga ilitambulisha jezi hizo Januari 30, 2023, ambazo zina mdhamini mpya kampuni ya vifaa vya nyumbani ya Haier, ambayo imesaini kumpa Yanga Sh1.5 bilioni kwa mechi za mashindano ya Kombe la Shirikisho Afrika.
 
Siyo yote.
However, sasa kwanini mnajifanya mnaujua mkataba na kulaumu upande mmoja?
Sisi tunafanya reasoning kupitia kauli zao tu

Yanga wanapotambulisha jezi mpya walisema wamefikia makubaliano na SportPesa kuwaruhusu waingie dili na mfadhili mwingine.

Na watu wengi tulijua hili limeidhinishwa na SportPesa

SportPesa wamekuja kukanusha kwamba waliwapa Yanga option moja ya kuweka Visit Tanzania tu

Na wamefika mbali kuwapa Yanga siku 3 wawe wametoa nembo ya yule mdhamini

Mpaka hapa inaonesha kuna shida upande wa Yanga

Ajabu mashabiki wengi wa Uto wamekomaa na hoja ya bonus kama big issue wakati uongozi wa Yanga una recognize nafasi ya SportPesa kwenye hii ishu na ndio maana walienda kuomba ruhusa
 
Yanga ni wazee wa matatizo kwenye mikataba,kila siku Wao tu,wanasheria wa Yanga ni wa kuokota jalalani🤣🤣🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…