Yanga kuelekea msimu mpya

Smt016

JF-Expert Member
Joined
Jan 11, 2016
Posts
3,012
Reaction score
4,300
Habari zenu wana michezo mliomo humu ndani, hakika msimu wa mwaka 2020/2021 umeisha na pongezi kwa timu zilizoweza kufikisha malengo kwa asilimia mia moja na waliokaribia asilimia mia. Ila pole kwa walioshindwa kutimiza malengo yao na niseme tu nafasi ya kujipanga kuelekea msimu mpya ni huu.

Twende moja kwa moja kwenye mada. Binafsi kama shabiki wa Yanga kuna vitu nilivitegemea kufanyika kabla la jambo lolote ile kama kweli uongozi wa Yanga upo serious juu ya kufanya vyema katika msimu mpya ikiwa pamoja na kuijenga timu kiushindani.

Baada ya mchakato wa mabadiliko kukamilika kisha washabiki, wanachama, serikali na wadau wengineo kuridhia na kubariki mchakato wa mabadiliko nilitegemea Yanga iingie katika mfumo rasmi kabisa kulingana na katiba yao mpya inavyosema ikiwa pamoja na kuwapa timu hao wawekezaji, na kuundwa kwa uongozi mpya kulingana na katiba mpya ya Yanga.

Sasa ni jambo la ajabu mchakato umekamilika lakini hakuna kinachoendelea, wanaoendesha usajili ni wale wale akina GSM wa siku zote inamaana Yanga inaanza msimu kwa strategic zile zile za misimu ya nyuma. Ila mfumo mpya ungekuwa umeanza pengine huyo Makambo asingechukuliwa wangekuja wachezaji ambao ni zaidi ya makambo kwavile tu tayari wawekezaji wameshaweka fungu kubwa kwaajili ya usajili hivyo wangesajili kwa matakwa ya ripoti ya benchi la ufundi. Huu ndio ulikuwa wakati sahihi kwa mfumo mpya kuanza sasa.

Kwa wale wanaotegemea makubwa kutoka kwa Yanga msimu wa 2021/2022;basi mjiandae tu kwa maumivu maana mambo yanaendelea katika yale yale ya misimu ya nyuma. Yanga imefanikiwa kusaini dili nono na Azam ilikuwa ni wakati sahihi sasa kuwa na wawekezaji na uongozi mahiri wanaoweza kupangilia contents nzuri na pia kuanza kuonesha update za miradi mbali mbali. Hiyo miradi yote inahitaji ela sasa kutoa ela kwaajili ya kufanikisha miradi hiyo ni moja ya majukumu ya wawekezaji.
 
Mvumilivu hula mbivu, subira yavuta heri
 

Kuna mtu humu anaitwa Shujaa Mwendazake, yeye anasema tayari Yanga ina mwekezaji Azam TV ambaye amewekeza fedha nyingi kuliko Mo wa Simba !!! Maajabu hayataweza kuisha!
 
Paap,,,picha linaanza wamemsajili Konde boy feki.mara tena paap kujakushtuka sio wachezaji bali ni wanamuziki wa kutoka Congo D.R.C.
 
Umemunderate sana makambo na sijuhi kwa hapa bongo umemfananisha na nan? Alafu kama mwaka jana hujakuwa naye jilinganishe msimu akiwepo, ni vitu viwili sawa kweli?
 
Umemunderate sana makambo na sijuhi kwa hapa bongo umemfananisha na nan? Alafu kama mwaka jana hujakuwa naye jilinganishe msimu akiwepo, ni vitu viwili sawa kweli?
Yanga inaenda kushiriki michuano ya klabu bingwa tambua hilo. Hivyo inatakiwa isajili wachezaji bora zaidi. Ukimwangalia makambo kwa kiwango cha hivi karibuni amekuwa sio mchezaji tegemeo kwenye timu ya Hororya. Kasajiliwa Yanga kwavile alifanya vizuri akiwa Yanga kipindi hiko sio kwa kufuata uwezo alikuwa nao kwa hivi karibuni.
 
Inshu sio kusajili wachezaji bora, kwani hao sio vipuri vya mashine, unafika na kuanza kuviunganisha tu, mashine tayari!!huwezi ukawa kila msimu una sajili karibia 3/4 ya timu , utegemee , kuwa na timu bora!!na viongozi wao wameshawajua mashabiki mnataka nini basi, itakuwa hivyo hivyo, miaka yote, kuna kiongozi mwingine leo yupo burundi, anatafuta kifaaa!!!
 
Wenzako wako bize kuukosoa uwekezaji wa Mo kule Simba.
 
Na ndio maana nimetamka kuwa tunaenda kuwa Yanga ile ile ya misimu ya nyuma. Wangeanza katika mfumo mpya kabla ya kuanza msimu wa 2021/2022 hao wawekezaji wangeunda majopo yao ya watalaamu (viongozi) ambao wangewasilisha short and long term planning. Kungekuwa na mikakati na mipango madhubuti ili kufikia hayo malengo. Yaani ilishajulikana kabisa kuwa ili kupata mafanikio mfumo wa wawekezaji ndio suluhisho pekee halafu unajisahaulisha unaanza msimu mpya kwa desturi ile ile ya siku zote.
 
Kwenye kusajili mchezaji wa soka Kuna Mambo mengi, mfano Simba wamesajili wachezaji watatu dirisha dogo wote wame feli, Peter Maduhlwa, Junior Lukosa, Chikwende. Yanga waliwahi kumsajili Juma balinya akiwa mfungaji Bora Uganda, Michael Saprong akifanya vizuri Lwanda, Wazir Junior mfungaji Bora wa Mbao FC lakin wote wamechemsha.
Kwaiyo kusajiri kitu kingine na mchezaji kufanya vizuri ni kitu kingine.
Angalia mifano hii Mateja Keizman, Shevshenko, Fernando Tores n.k wote walikua wakali uko walipotoka lakini walichemka pale Chelsea.
 
Unaumia ukiwa wapi ? Ujuaji mwingi kumbe kichwani box tupu
 
Upo sahihi lakini tumejijengea tamaduni za kuanza upya kila msimu. Kwa maelezo yako ni kwamba kuna wachezaji ambao walikuwa ni bora walipotoka lakini wamefeli walipokuja Yanga inawezekana kunasababu nyingi inayowafanya wafeli mfano ugeni wa ligi na kutokuwa na chemistry nzuri baina ya wao kwa wao. Lakini hoja yangu kuu ni namna Yanga tunaendelea na utaratibu ule ule wa zamani. Badala ya kuanza rasmi kuwapa wawekezaji waitengeneze Yanga mpya kwa kuanzia msimu mpya wa 2021/2022 na kuendelea.
 
Unaumia ukiwa wapi ? Ujuaji mwingi kumbe kichwani box tupu
Sawa kabisa mimi kichwani box. Embu mweleweshe huyu kichwa box akuelewe basi. Kama hujui kujibu hoja endelea kukuna nazi au nenda kachambane facebook na Instagram JF sio kwaajili yako.
 

Kuna mtu humu anaitwa Shujaa Mwendazake, yeye anasema tayari Yanga ina mwekezaji Azam TV ambaye amewekeza fedha nyingi kuliko Mo wa Simba !!! Maajabu hayataweza kuisha!
Yanga bado hawajawapa timu wawekezaji. Labda jamaa hakujua ule mkataba wa Yanga na Azam unahusu nini.
 
Mi nafikiri ungekuwa makini na michakato ya uwekezaji ndani ya yanga usingeongea hicho unachokiongea, taratibu za uwekezaji zinakwenda hatua kwa hatua usifikiri kwamba yanga kupitisha katiba ndo kesho yake angekabidhiwa mwekezaji akuna kitu Kama icho rafiki yangu, kuna taratibu lazima zifatwe ikiwemo kupeleka katiba husika kwenye mamlaka husika waipitie ambao ni baraza la michezo ikiwemo wizara ya michezo, kuna kufanya tathmini ya kujua thamani ya yanga ni ipi, baada ya hayo ndo itatangazwa zabuni kwa wawekezaji wanaotaka kuwekeza kulingana na thamani itayotangazwa na klabu, hivyo usifikilie ni jambo la kukurupuka tu siku mbili tatu anapewa mwekezaji akuna kitu Kama icho aisee
 
Wawekezaji gani? Ninachojua ni mkwamba mchakato wa kampuni bado,nadhani ungekamilika wawekezaji hao kwenye hizo hisa ndio wangekuwa na hizo short and Long plan
Vinginevyo usishangae mfumo wa usajiri unaotumika kwa sababu hawajashift kwenda huko unakotaka kwa 100
Nafikiri tuwape muda kwa kuwa wameanza vizuri na naamini wanajua safari Yao watapitia wapi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…