kavulata
JF-Expert Member
- Aug 2, 2012
- 13,778
- 14,214
Yanga ilifungwa na Azam lakini wanaYanga wanaona poa tu. Kufungwa huku sio udhaifu bali ni mwanzo wa wachezaji na walimu kuongeza umakini na juhudi kwenye mechi.
Bila ya hivyo kiburi na kujiamini kulikopitiliza kungetamalaki kikosini. Hata wasanii wa hovyo walitunga nyimbo za kuwaaminisha wachezaji, walimu, viongozi na mashabiki kuwa Yanga haiwezi kufungwa, bila shaka nyimbo za aina hii zimejimaliza zenyewe baada ya Yanga kupoteza mechi dhidi ya Azam.
Hata hivyo, pamoja na kufungwa lakini Azam ndio waliokuwa wanaomba mechi iishe kwa ushindi wa tugoli tumoja dhidi ya Yanga yenyewe wachezaji pungufu.
Hii ni kuonyesha kuwa timu zote nchini zinaiheshimu sana Yanga.
Natabiri kuwa baada ya mchezo ule Yanga haitapoteza tena na itafungua ukurasa wa magoli mengi dhidi ya wapinzani na hkuna mchezaji atakaeshangaa wala kuhoji kama Gamondi atamsugulisha mbao ndefu kikosini.
Amepata sababu ya kuwanyima namba wachezaji wasiojituma na wanaopoteza nafasi za wazi.
Bila ya hivyo kiburi na kujiamini kulikopitiliza kungetamalaki kikosini. Hata wasanii wa hovyo walitunga nyimbo za kuwaaminisha wachezaji, walimu, viongozi na mashabiki kuwa Yanga haiwezi kufungwa, bila shaka nyimbo za aina hii zimejimaliza zenyewe baada ya Yanga kupoteza mechi dhidi ya Azam.
Hata hivyo, pamoja na kufungwa lakini Azam ndio waliokuwa wanaomba mechi iishe kwa ushindi wa tugoli tumoja dhidi ya Yanga yenyewe wachezaji pungufu.
Hii ni kuonyesha kuwa timu zote nchini zinaiheshimu sana Yanga.
Natabiri kuwa baada ya mchezo ule Yanga haitapoteza tena na itafungua ukurasa wa magoli mengi dhidi ya wapinzani na hkuna mchezaji atakaeshangaa wala kuhoji kama Gamondi atamsugulisha mbao ndefu kikosini.
Amepata sababu ya kuwanyima namba wachezaji wasiojituma na wanaopoteza nafasi za wazi.