Yanga kukata rufaa dhidi ya adhabu ya Dr Aucho

Labani og

JF-Expert Member
Joined
Sep 15, 2020
Posts
19,637
Reaction score
29,473
SIKU moja tu tangu Kamati ya Kusimamia na Kuendesha Ligi ya Bodi ya Ligi (TPLB) kutangaza kumfungia kiungo wa Yanga, Khalid Aucho kwa mechi tatu na kumlima faini ya Tsh 500,000 kwa kosa la utovu wa nidhamu, mabosi wa klabu hiyo wapo kwenye mchakato wa kukata rufaa.

Akizungumza na Mwanaspoti, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano ya Yanga, Rodgers Gumbo alisema uongozi haujakubaliana na uamuzi huo wa kamati hiyo ya bodi ukiona kiungo huyo amehukumiwa mara mbili.

Gumbo alisema wanalazimika kutaka rufaa kutokana na kuwa waliwahi kuiandikia Bodi ya Ligi siku za nyuma juu ya beki wa Simba, Henock Inonga aliyefanya kosa kama hilo, lakini walijibiwa mwamuzi alishachukua hatua ndani mchezo kwa kuonyeshwa kadi ya njano, ila safari hii Aucho hilo limesahaulika.

NB hawajamaliza Wana Yanga ......mlete aucho
 
Kuna Lijamaa moja puuzi sanaaa.....muda utaongeaaa
 
Mechi ya Ihefu alipiga kiwiko, mechi ya Coastal kapiga kiwiko. Makosa yote mawili yalistahili red cards ambazo hakupewa. Kadi ya njano siyo adhabu ni onyo. Cha msingi Yanga wanapaswa kumpa adhabu mchezaji wao badala ya kulalama maana matukio yamekuwa ya kujirudia kwa mchezaji yuleyule. Kumkingia kifua ni kuhalalisha anachokifanya. Kosa moja halihalalishi kosa jingine
 
Sisi kama viongozi tunataka wachezaji watemi kama Aucho


Sasa unasemaje?
 
Mzazi gan atampa adhabu mwanae mpendwa[emoji23][emoji23]
 
uko sahihi ila yanga wana uliza kuna mchezaji aliwahi fanya utovu wa nidhamu akapewa njano hivyo hakuna adhabu nyingine, aucho kafanya faulo na kapewa adhabu asa ya nini tena kumfungia mbona yule hakufungiwa
 
Timu kama taasisi itashughulikia waajiriwa wake kwenye vikao vyao vya ndani ila huku nje lazima waoneshe kuwa wamoja hata wewe mkeo akikosea sio busara kumfokea mbele za watu, hata ivyo yanga wana hoja kwanini kosa ilo ilo lishughulikiwe tofauti?, kiukweli lile kosa la Aucho alistahili kupewa red card pale pale uwanjani ila nilishangaa nilivyosikia Aucho kapigwa nyundo na TFF wakati alishapewa kadi ya njano uwanjani. Refa aliechezesha mechi alifanya makosa, TFF wamefanya makosa na Aucho pia anatakiwa kujirekebisha michezo yake michafu hii sio mara ya kwanza.
 
Mkuu kadi ya njano moja haijawahi kuwa adhabu kwenye mpira wa miguu, ni onyo
 
uko sahihi ila yanga wana uliza kuna mchezaji aliwahi fanya utovu wa nidhamu akapewa njano hivyo hakuna adhabu nyingine, aucho kafanya faulo na kapewa adhabu asa ya nini tena kumfungia mbona yule hakufungiwa
Kosa moja halihalalishi jingine. Kutomfungia wa kwanza lilikuwa kosa pia. Pengine kaadhibiwa kwa kuwa karudia kosa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…