Yanga Kukosa Magoli Ushirikina Unatumika

Yanga Kukosa Magoli Ushirikina Unatumika

Wajinga mashabiki wa utopolo na viongozi wao.
Wanahonga ili washinde mechi halafu wanajidanganya timu nzuri.
Haya sasa timu zinaogopa kushuka daraja,bahasha imekataliwa mnasingizia uchawi wakati ninyi ndio mliochimbia hirizi wazi wazi uwanjani
 
Wanajiroga wenyewe!
 
Hiyo yanga walitaka kuua ule uchawi,yaonyesha nao wamestuka...na kizuri Manara anajua mipango mingi
Kwahiyo Ni loga nikuloge.

Kwahiyo wengine wanaokosa magoli si kwamba ni mpira bali ni uchawi.

Na yanga yy hawezi kukosa magoli.

Chezeni, mpira, timu zinapambana kuepuka kushuka daraja. Hii ni lala salama.

Mnafikiri mtapata kitonga tu, kwamba mnashinda nyie tu wengine hawahitaji alama.

Acha ujinga!
 
Hakuna uchawi bahati haikuwa yetu
Ndivyo mpira ulivyo popote pale. Tatizo ni hii mentality kwamba lazima Yanga ishinde. Hakuna hali ya hivyo.

Na mechi zilizobaki zitazidi kuwa ngumu kila timu itaona kumbe inawezekana. Na Yanga nao presha itakuwa juu na kuzidi kuongeza ugumu.

Sisi Simba wala hatuna shida tumerilax wakija tunajipigia tu.

BTW kila mtu ashinde mechi zake
 
Wengi hawataamini lakini ukweli ndio huu,
Hali ya kukosa mabao kwa Yanga leo imeingia katika mechi dhidi ya Tanzania Prison, kabla ya hapo zimekuwepo mechi kadhaa ambapo Yanga mbali ya kucheza vizuri na kupata nafasi mipira imekua haiingii golini,

Tukianza na mchezo baina ya Yanga na Simba washambuliaji wa Yanga wameshindwa nafasi za wazi kabisa kuingiza mpira wavuni, Mfano zile chance za Denis Nkane

Mechi na Jkt Ruvu pale Kigoma pia goli lilionekana zito mpira kuvuka na kuingia ndani ya nyavu, ikumbukwe siku ile Jesus Moroco alikosa nafasi mbili tatu za wazi,Fiston Mayele aligongesha bomba mara mbili na nafasi nyingine mpira alioupiga ukaenda nyavu ndogo

Mechi hii na Prison Mayele anashindwa kufunga nafasi za wazi ikiwemo penati, Faisal naye..Makambo eti anashindwa kuusukumia ndani mpira japo kwa kuugusa tu!

Ukichukulia ki kawaida utaona labda ni kawaida lakini ukifikiri deep utagundua hapo kuna mikono ya kishirikina tu ambapoo kuna watu ama kikundi cha watu hawapendi na hawataki Yanga iendelee kushinda game zake zilizobaki
Mayele si wa kiwango hicho na hili linajulikana.Yaani hadi unaona wachezaji wanapigwa butwaa!

Ila tunasema mwisho wa siku mchawi atajulikana.

Mimi nadhani mmojawapo au baadhi ya hawa ndugu zako ni washirikina: baba/ mama yako, babu zako wa pande zote au shangazi zako. Maana haiwezekani hadi karne hii mtu mwenye akili timamu aamini mambo ya kishirikina kwenye mpira. Ingekuwa hivyo, Tanzania tungekuwa na makombe hadi ya world cup achilia mbali makombe ya Africa hapa.
 
Alaa!! Mie nikajua nimeweka video ya uchawi wa yanga, au wameniroga mpaka mimi [emoji23][emoji1787]

Djuma shaban kafukia kitu katikati ya kiwanja, halafu kuna mzee anamwaga mwaga maji.
Boss unamasikhara sana[emoji23]
 
... mipira imekua haiingii golini... Tukianza na mchezo baina ya Yanga na Simba washambuliaji wa Yanga wameshindwa nafasi za wazi kabisa kuingiza mpira wavuni, Mfano zile chance za Denis Nkane
Yanga haikupiga shot on target hata moja, inakuwaje useme Denis Nkane alipata nafasi ya wazi? Krosi ni nafasi ya wazi ambayo mpira 'umekataa' kuingia wavuni?
 
Malalamiko fc hivi raisi mnakutana nae lini au mmehairisha na kuhusu kuloga umeiona ile video ya juma shabani jana anavyofukia vitu uwanjani au mnajitoa ufahamu.
 
Back
Top Bottom