Yanga kumsajili Okrah ni sawa na kuweka kiraka kikuu kwenye nguo mpya!

Yanga kumsajili Okrah ni sawa na kuweka kiraka kikuu kwenye nguo mpya!

mbingunikwetu

JF-Expert Member
Joined
Feb 17, 2015
Posts
13,897
Reaction score
18,477
Ni suala la muda tu itakapodhihirika kuwa walichokifanya ni sawa na kuweka kiraka kikukuu kwenye nguo mpya! Ni hayo hayo Bernard Morrison! Soka la kisasa nidhamu inapewa kipau mbele kuliko kipaji!! Nidhamu mbovu huua kipaji na kuleta hasara kwa timu na mchezani, yetu macho!!
 
Ntibazokiza alifukuzwa Yanga kwa ajili ya nidhamu mbovu aliyoonyesha wakiwa Mwanzaa, lakini akaja kuwa lulu kwa simba
Kwa sababu alikua lulu Simba, hiyo siyo sababu ya kuwafanya wengine wasifanye maamuzi juu ya mchezaji?
Unataka vilabu viwe mateka ya wachezaji.
 
Kwa sababu alikua lulu Simba, hiyo siyo sababu ya kuwafanya wengine wasifanye maamuzi juu ya mchezaji?
Unataka vilabu viwe mataka ya wachezaji.
Mpira unataka matokeo tu ndugu yangu; Morrison alikuwa na nidhamu mbovu sana lakini anapokuwa uwanjani analeta matokea na timu zote Yanga na simba zilisajiri.
 
Mpira unataka matokeo tu ndugu yangu; Morrison alikuwa na nidhamu mbovu sana lakini anapokuwa uwanjani analeta matokea na timu zote Yanga na simba zilisajiri.
Nidhamu ndiyo kila kitu. Mchezaji hata awe mzuri vipi, nidhamu ikiwa mbovu ni sahihi vilabu kuachana naye.
Morrison alikua ni msumbufu zaidi, hakuhatarisha umoja au malengo ya club
 
Nidhamu ndiyo kila kitu. Mchezaji hata awe mzuri vipi, nidhamu ikiwa mbovu ni sahihi vilabu kuachana naye.
Morrison alikua ni msumbufu zaidi, hakuhatarisha umoja au malengo ya club
Inategemea na level ya nidhamu. Kuna nidhamu ya kazini na nidhamu binafsi. Wachezaji wengi wana nidhamu nzuri wawapo mafunzoni na kwenye mechi (nidhamu ya kazini), lakini wawapo katika maisha yao binafsi wana nidhamu za hovyo sana (nidhamu binafsi). Timu hujali sana nidhamu za kazini siyo hizo za maisha ya wachezaji binafsi. Neymar ana nidhamu ya hovyo sana wakati mwingine anachanganya nidhamu binafsi na nidhamu kazini kwa kukubali red cards za kijinga lakini timu zinamvumilia
 
Kama kiraka kipo kwenye msamba kuna ubaya gani? Ni nani atayejua nguo ina kiraka?
 
Wameshasahau ya SAIDOO aliyeachwa Yanga kwa utovu wa nidhamu, Sasa hivi ana ufalme wake pale koloni.

Morrison mkasema anaongoza kwa nidhamu baada tu ya kuja Simba!
 
Yanga wakimsajili Mudathir Yahaya akiwa hana hata timu yupoyupo tu kifupi alionekana mpira umeisha lkn wao wakamchukua sote sasa ni mashahidi wa kazi ya Mudathir pale klabuni. Kifupi yawezekana simba walishindwa kumtumia Okrah na yanga wao wameona matumizi yake. Tusubiri wakati utatoa hukumu
 
Ni suala la muda tu itakapodhihirika kuwa walichokifanya ni sawa na kuweka kiraka kikukuu kwenye nguo mpya! Ni hayo hayo Bernard Morrison! Soka la kisasa nidhamu inapewa kipau mbele kuliko kipaji!! Nidhamu mbovu huua kipaji na kuleta hasara kwa timu na mchezani, yetu macho!!
Wewe unaumia kitu Gani na wahusika ni wengine? Waliomtaka ndio watapata hasara Kama nidhamu yake ni mbovu na mshahara wanalipa wao sio wewe!
 
Nidhamu ndiyo kila kitu. Mchezaji hata awe mzuri vipi, nidhamu ikiwa mbovu ni sahihi vilabu kuachana naye.
Morrison alikua ni msumbufu zaidi, hakuhatarisha umoja au malengo ya club
Kwani morisoni uko aliko achezi mpira?..Au mnataka muwe na mchezaji mtakatifu.Acheni watu watafute maisha.hayo mengine niyakawaida kwasababu mpira sio njia yakwenda peponi kwamba lazima mtu awe mtakatifu.
 
Kwani morisoni uko aliko achezi mpira?..Au mnataka muwe na mchezaji mtakatifu.Acheni watu watafute maisha.hayo mengine niyakawaida kwasababu mpira sio njia yakwenda peponi kwamba lazima mtu awe mtakatifu.
JItahidi uwe unasoma na kuelewa
 
Shida ya team zetu zote tu naongelewa kwa ujumla, wakisajili mchezaji wanampa ustar kabla hata hajaonesha kitu uwanjani nadhani na hii inachangia sana wachezaji kufail. Mpira wa sasa sio wa miaka ya 80 mpaka 90 maana tuliegemea Radio na magazeti tu, sasa mtangazaji akitaka kumkuza mtu sisi sote tunamuamini na kujengwa taswira ya mchezaji sio wa kawaida. wangapi tumewatukuza wachezaji zamani na sifa kibao na wengi mpaka wameacha mpira hatukuwahi kuwaona wakicheza. Anyway kwa ufupi kusajili sawa ila kama mchezaji hajathibitisha kama bora tumwache kwanza aoneshe uwanjani atatukuzwa tu bila promo maana mipira tunaiona hatutegemei Radio tu tunaona live, labda kama tumesajili mchezaji toka team kubwa na kishaonesha yeye ni nani hapo tufanye mbwembwe zote ila hawa kama betting tuache kwanza.
 
Back
Top Bottom