Yanga kupanda kutoka nafasi ya 75-28 ni rekodi ya Afrika

mwarabu feki

JF-Expert Member
Joined
Feb 16, 2023
Posts
811
Reaction score
1,811
Huu ni mwanzo tu wa rekodi nyingi zitakazowekwa na Yanga msimu huu. Ndani ya msimu mmoja tu wa mashindano ya CaF, timu imepanda viwango kwa zaidi ya nafasi 47, wakati kuna timu inayojiita ina mafanikio kimataifa yenyewe imeganda palepale kwa misimu karibu mitatu sasa.

Niwaambie tu mpaka kutamatika kwa michuano hii ya CaF msimu huu, Yanga itakuwa pale juu na miamba kama Al Ahly, Waydad na Mamelodi..

Povu ruksaa
 
Hujui hata namna points zinavyopatikana..

Jiulize, pamoja na kuflop kwa Al Ahly kwa nini bado yeye ndiye namba moja kwa Afrika? Na itachukua miaka mingi yeye kushuka, kwa sababu alishajijengea points nyingi hapo awali. Unamuna Berkane? Hayupo katika mashindani yeyote ya Kimataifa msimu huu lakini still yupo top 10, kwa nini? Akili kichwani, siyo kule kulipo Mwiko..

Unashangaa Yanga kupanda kwa pupa? Sikiliza, mfano wote mkawa na alama moja. Msimu mwingine wewe ukawa na alama 4 maana yake utawapita wengi mliokuwa mnafanana.

Nakuambia hivi, hata mkishinda Ubingwa wa Kombe la Losers top 10 hamtaingia.
 
Wakati ukijisifia kutoka nafasi ya 78 hadi 28
Simba ipo nafasi ya 8
 
Hujui hata namna points zinavyopatikana..

Jiulize, pamoja na kuflop kwa Al Ahly kwa nini bado yeye ndiye namba moja kwa Afrika? Na itachukua miaka mingi yeye kushuka, kwa sababu alishajijengea points nyingi hapo awali..
Haya ndio mapovu niliyoyaruhusu[emoji1787][emoji1787]
 
Kupanda nafasi 47 si jambo dogo tena ndani ya Msimu mmoja ambao bado haujatamatika
Angalia nafasi ya simba kabla ya kuingia makundi 2018 alikuwa nafasi ya ngapi?na alipanda hadi nafasi ya ngapi? Tatizo lenu mihemko imezidi.

Na ndio maana juzi mmejitoa ufahamu mnasema yanga ndio timu ya kwanza kwa timu za Tanzania kuongoza makundi.Mmesahau simba aliongoza kundi lililokuwa na bingwa mtetezi Al Ahly na Al Ahly huyohuyo ndie aliyebeba ubingwa msimu ule.

Nyie mmeongoza kundi ambalo mmeikuta mazembe ipo ICUπŸ˜€πŸ˜€πŸ˜€
 
Wivu mbaya sana, kwaio wewe umeumizwa sana na Yanga kupanda nafasi 47??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…