HPAUL
JF-Expert Member
- Jan 18, 2011
- 410
- 567
Itakumbukwa mwaka jana wakati ligi kuu ipo hatua za mwanzo, Simba ilifungwa na Mbao jijini Mwanza na Aussems kocha wa Simba alirushiwa chupa na wapenzi wa Simba waliochukizwa na matokeo, huku wakiamini Masoud Juma aliyekuwa kocha msaidizi ambaye aliachwa Dar anapigwa zengwe na Aussems. Safari hii mechi imekuwa zamu ya Yanga jijini Mwanza ambayo juzi ilisawazisha bao dakika za usiku ilipocheza mechi ya kirafiki dhidi ya timu ya daraja la kwanza Pamba ambayo muda mwingi wa mchezo ilicheza ikiwa na wachezaji pungufu. Washabiki wa Yanga walimtaka Zahera aondoke Yanga na mchezaji wake Moringa "Falcao" ambaye walimwita ni mcheza shoo wa Fally Ipupa.
salehjembe.blogspot.com