Naona wewe uijui simba kamuulizie mtu mmoja anaitwa Hassan Mbashiri je mkono wake umekuwa mkubwa kwa ajili ya nini...Muulize Hassan Dalali kafukia vitu vingapi yeye na Marehemu mzee Matuga katika makaburi ya Magomeni Mwinyimkuu. Au wakati Simba wanaruka ukuta ulikuwa haupo mkuu...mpira wa Tanzania huo ushirikina ndio unaotawala kila siku mkuu..au Muulize Aveva aliajiri wapenzi wa Simba pale Embassy hotel kwa ajili ya nini?
Naona wewe uijui simba kamuulizie mtu mmoja anaitwa Hassan Mbashiri je mkono wake umekuwa mkubwa kwa ajili ya nini...Muulize Hassan Dalali kafukia vitu vingapi yeye na Marehemu mzee Matuga katika makaburi ya Magomeni Mwinyimkuu. Au wakati Simba wanaruka ukuta ulikuwa haupo mkuu...mpira wa Tanzania huo ushirikina ndio unaotawala kila siku mkuu..au Muulize Aveva aliajiri wapenzi wa Simba pale Embassy hotel kwa ajili ya nini?
Toa ushahidi mkuu...kuongea tu kwa hearsay kila mtu anaweza.....huo uzi uliotuelekeza utaukimbia mwenyewe tu hata usiwe na haraka
Let exhibits speak themselves.
Na ile iliyomvua mtu bukta uwanjani kule Tanga kwa imani za kishirikina na hata baada ya kumdhalilisha mjeda wa watu bado litimu lao likachezea kichapo ilikuwa ni ya daraja la ngapi vile?Kwani ile timu iliyotishia kuuhama uwanja wa ccm kirumba kule mwanza kwa madai kuwa wanalogwa na timu ya toto africa na kusababisha kupoteza michezo mitatu mfululizo sio ya ligi kuu!!!!?
Msimu huu ni nani aliyepigwa faini alipokwenda Shinyanga kwa kuruka ukuta wa uwanja kisa imani za kishirikina?Mkuu usihangaike sana, records zimeandikwa klabu ya Simba ilipigwa faini mwaka Jana kwa kuendekeza mno matendo ya kishirikina viwanjani.
... Matunda ya kupaisha juu ya lango lililo wazi!Mbuyu wenye matunda ndio unaopondwa mawe kama siyo rungu!...
Kidogo Cannavaro anajitahidi kufikiri japo na yeye bado hayupo sawasawa. Hivi Yanga mnashindwa kweli kufikiri japo kidogo kama punje moja ya vumbi kweli! Hivi kama kweli uchawi ungekuwa dili katika soka Timu za Mikoa ya Rukwa, Katavi na Bagamoyo (Pwani) zingekuwa hapo zilipo kweli?
MASTRAIKA wawili wa Yanga wamekumbana na uchawi wa aina yake. Kpah Sherman ambaye ni Mliberia amedai kuyabaini maji ya ushirikina yaliyokuwa uwanjani, lakini mwenzake Danny Mrwanda akayachukua akayanywa huku kipa aliyeyaweka akiwashangaa.
Kpah ambaye si mzungumzaji sana, alifichua tukio hilo lililotokea kwenye mechi yao ya Ligi Kuu Bara dhidi ya Ndanda kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam ambapo timu hizo hazikufungana.
Lakini mlinda mlango wa Ndanda, Wilbert Mweta, ambaye ni kipa wa zamani wa Simba, aliposikia maneno ya Sherman akashangaa. Katika mchezo huo, washambuliaji wa Yanga; Sherman, Mrwanda na Simon Msuva walikosa mabao ya wazi wakiwa peke yao mbele ya lango, kila walipopiga mipira ilipaa na kutoka nje hali ambayo iliwashangaza wapenzi wa soka na mashabiki waliofika uwanjani hapo. Hata hivyo kocha wa Yanga, Hans Pluijm, amepuuza madai hayo na kusema ni uzembe tu wa wachezaji wake.
Sherman ameiambia Mwanaspoti kwamba kwenye goli la Ndanda kulikuwa na maji ya ushirikina na aliyatoa kwa mikono yake baada ya kugundua kwamba kipa huyo aliyanyunyizia kwenye goli na baadaye akayabakiza mengine na kuyaweka pembeni ya mlingoti wa lango.
Baada ya Mliberia huyo kuyatoa maji hayo na kuyatupa nje, bado yalikuwa magumu kwao kisha Mrwanda aliyafuata na kuyanywa. Hata hivyo haikusaidia chochote kwani ndio kwanza wapinzani wao walizidi kukaba huku wakijiangusha kupoteza muda.
Sherman aliiambia Mwanaspoti akisema: "Mimi ni Mwafrika moja kwa moja naamini maji yale yaliwekwa vitu tu vya kishirikina ikawa sababu ya kutukosesha mabao, ndiyo maana niliamua kuyatupa nje, haiwezekani mtu na goli unapaisha.
"Pia nilimwona kwa macho yangu yule kipa, yale maji aliyamimina (anaonyesha kwa ishara) kuanzia mwanzo wa goli hadi mwishoni kwa nini alifanya vile ndio yalikuwa kikwazo kwetu,"alisema Sherman ambaye Yanga wanamchukulia kuwa ndiye straika namba moja wa timu yao.
Ingawa Mrwanda hakupenda kufafanua hilo, kipa Mweta alijitetea akisema: "Ule ni mpira ndiyo maana tunafanya mazoezi, hakuna ushirikina wala nini.
"Nimeshangaa sana kuona mchezaji mkubwa kama yule kuamini mambo hayo ya kishirikina badala ya kucheza mpira, anajua kiwango chake ni kidogo?"
Kocha Pluijm alisema hawezi kuwalaumu washambuliaji wake kutokana na kitendo cha kushindwa kufunga mabao na badala yake anaulaumu mfumo wa makuzi ya soka waliyokulia wachezaji hao tangu utoto wao.
Pluijm alisema suala la kufunga ndiyo jambo kubwa alilokuwa akiwaelekeza katika kipindi chote cha mazoezi yao na walikuwa wanafanya vizuri mazoezi. Alisema aligundua tatizo hilo katika michezo waliyocheza na Polisi Morogoro na Ruvu Shooting.
"Hatufungi, sina wasiwasi na safu ya ulinzi lakini kwa washambuliaji tatizo lao ni ufungaji, nimekuwa nikilifanyia kazi kwa siku zote kwenye mazoezi yetu na wachezaji walikuwa wanafanya vizuri," alisema kocha huyo.
"Siwezi kuwalaumu wachezaji wangu kwa nini hawafungi, unaona ni tatizo ambalo lilitokana na makuzi yao tangu walipokuwa wadogo, kwa sababu wanafuata maelekezo na wanafika golini, yuko yeye na kipa, anashindwa kufunga, anapiga mpira unapaa juu.
"Lakini umakini nao haukuwepo ingawa natambua pamoja na kufunga mazoezini, hali huwa inakuwa tofauti na mnapokuwa mnacheza mechi."
Nahodha wa Yanga, Nadir Haroub ‘Cannavaro' aliwataka mastraika wake kuwa makini na kuhakikisha wanafunga mabao kwani kwa sasa hawafanyi kazi hiyo kikamilifu.
"Si mimi tu, hata wenzangu wanashangazwa na hali ya timu kutopata mabao. Naamini hili linatokana na safu ya ushambuliaji kukosa umakini," alisema.
" Binafsi, mimi na safu yangu ya ulinzi tunatimiza kazi yetu ya kuzuia kikamilifu na hilo ni dhahiri kwa kuwa tunajitahidi kutoruhusu mpira kufika kwenye goli letu.
"Lakini Yanga ina washambuliaji wengi ambao wote wameletwa kwa kazi moja ya kufunga mabao. Naamini wanatakiwa kuifanya kazi hiyo wakishirikiana na sisi, lakini wao ndiyo wanalo jukumu la kufunga zaidi yetu, sisi mabeki kazi yetu ni kuzuia."
Beki huyo wa kutegemewa wa Yanga huwa anafunga kati ya mabao matatu hadi saba kila msimu wa Ligi.
Source: Mwanaspoti 04 feb 2015
Yanga mbona mnakuwa wachawi kiasi hicho....timu zingine zote hazilalamikii uchawi ila nyie tu Makoye Matale Bantu lady mkolaj Deo Corleone sembo Amavubi grafani11 Masuke Sibonike barafuyamoto Revocatus Kashaga
Nani anapiga mawe mbuyu wenye kilinge cha kishirikina?Mbuyu wenye matunda ndio unaopondwa mawe kama siyo rungu!
Imani za uchawi zinavyoangamiza soka, nini kifanyike kwa sasa? - Fikra PevuFikra Pevu
...kaka mkubwa unapoteza NISHATI kwa huyo kashanga..jamaa ni empty kabisa katika mpira....Facebook kule huwa anajiandikia upuuzi tu...jana kaja na porojo za yanga kufungwa na coastal hatima yake...kasahau hata ku update UZI alioanzisha
Mkuu umeweka picha nyingi unfortunately hizo picha za hapo watu hapo juu wenye kuku hatuoni sura zao....Nani anaweza kujua kuwa ni simba? kwa sababu tu wamevaa nguo nyekundu? mbona Coastal pia wanavaa?
Hilo jeneza ni ushabiki wa kawaida tu...kama wewe unadhania huo ni ushirikina basi tatizo liko kwako unayedhania
Mkuu Freeland nakushukuru kwa mawazo yako ukijaribu kuibua shaka (maana huhitaji ku-prove your innocence), naomba twende pamoja kwenye picha ya chini ambapo kuna maneno 'Mganga afunguka nyota Simba, Yanga wanavyoroga makaburini' baada ya maneno hayo kulia kuna picha ndogo 2 (picha hizo ni zile zile zinazoonekana mwishoni mwa mstari wa kwanza, picha ya 3 na ya 4 kutoka kushoto, picha hizi ni mwendelezo wa picha ya 1 na ya 2); ya kwanza kuna mtu ameshikilia mpira na mwingine kaning'niza kuku, ya pili kuna watu wawili wameshikilia kitu kilichofunikwa. Naomba uzitazame kwa umakini picha hizo kisha linganisha na yale maneno niliyonukuu hapo juu.
Maneno yametaja Simba, Yanga (yakimaanisha Simba na Yanga wote ni washirikina, hakuna Coastal Union wala Nyota Nyekundu hapo): Kwa ushahidi wa picha hizo hakuna shaka yoyote kuwa klabu iliyokuwa inawanga ni Simba.
Kwa upande mwingine, nashukuru kwa kuwa umetambua kwamba jeneza la Okwi (akiwa Yanga) haukuwa ushirikina isipokuwa kwa yule anayedhania hivyo. Kauli hii hii itumike pia kwa vitendo vya kuchukua gloves, taulo au hata maji ya kunywa si ushirikina isipokuwa kwa yule anayedhani hivyo.
Siisemei Yanga, ila naomba kuweka sawa mambo 4. (1) Kuna tofauti baina ya ushirikina na kuamini uchawi. Ushirikina ni kuabudu asiyekuwa Mwenye enzi Mungu, uchawi ni kuamini ama kuogopa nguvu za giza au chochote kisichoeleweka. Timu zetu zinaangukia kwenye hili la pili. Ila haziko peke yao kwenye hilo, kwa hivyo ni ujinga, ushamba na upuuzi kuzibeza timu zetu tu huku tukitukuza wengine wafanyao zaidi ya hayo, kwa sababu tu si Watanzania wala Waafrika. (2) kitendo chochote kinachoipa timu ama mchezaji kujiamini kwenye mchezo wake ni msaada kwa mchezaji na timu hiyo. Muhimu tu kisipingane na ustaarabu, sheria, kanuni na taratibu zetu na za kimpira. (3) Kwa nini wastaarabu wanaolaani ushirikina wa Yanga wasijiulize zaidi mambo rahisi ya msingi: (a) kwa mechi ya Mapinduzi Cup dhidi ya Shaba, je ni kawaida golikipa kubaki na glovu za akiba chini ya goli, hasa ndani ya nyavu? Si vifaa vyote vya akiba vinabaki na wachezaji wa akiba kwenye dawati la ufundi? Marefa ilikuwaje wasilione hilo? (b) Kwa mechi ya Ndanda, ni kawaida golikipa kubaki na chupa ya maji akiwa golini? Na kama ni kwa matumizi yake, kwa nini ayasokomeke nyuma ya nyavu ambako hata kuyafikia ni taabu kwake? (4) Hivi kuondoa glovu ama maji hayo inakuwa ni jambo kubwa kuliko yafuatayo? (a) Michael Jordan alikuwa ni lazima avae kaptura yake ya Chuo Kikuu cha Carlifonia ndani ya bukta ya timu kwenye kila mechi ya Chicago Bulls, jambo lililomlazimisha kuvaa bukta kubwa zaidi kuliko kawaida. Hatimaye bukta hizo kubwa ukawa ndio mtindo wa NBA nzima. (b) kabla ya kila msimu wa Wimbledon, Bjorn Borg aliwacha kunyoa ndevu zake. Akaishia kutwaa taji hilo mfululizo 1976 - 1980. (c) Serena Williams amezoea kuenda na malapa yake ya msalani hadi kwenye uwanja anaochezea mashindano, ni lazima adunde mpira mara 5 kabla ya 'serve' yake ya kwanza na mara 2 kwa 'serve' ya pili. (d)Kolo Toure lazima awe wa mwisho kuingia uwanjani kwenye mechi yoyote. Mechi ya fainali ya Ulaya dhidi ya AC Roma aligoma kuingia mwanzoni mwa kipindi cha pili hadi Gallas aliyekuwa akitibiwa alipoingia. Toure akalimwa kadi ya njano alipoingia baada ya hapo. (e) John Terry kwenye kila mechi huegesha gari yake mahali hapohapo, anatumia vikinga ugoko hivyohivyo kwa miaka 10 mfululizo mpaka vilipopotea kwenye mechi ya ugenini dhidi ya Barcelona. (f) laurent Blanc alikuwa akibusu upara wa golikipa wake Barthez kabla ya kila mechi ya Kombe la Dunia 1998. (g) wakati mmoja Pele alimvulia jezi shabiki mmoja baada ya mechi. Mechi zilizofuata kiwango chake kikaonekana kupungua, mpaka alipomwomba rafiki yake kuifuatilia jezi hiyo. Baada ya hapo mambo yakajipa tena, ingawa kuna habari kwamba jezi aliyorejeshewa haikuwa ileile. (h) Kipa Sergio Goycochea wa Argentina alikuwa akikojoa kiwanjani kila ulipofikia wakati wa penalti tanotano. Akaitoa Yugoslavia kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia 1990, akaitoa na Italia kwenye nusu fainali. Wakazitoa Columbia na Brazil kwenye kombe la Marekani Kusini 1993. (i) Rais wa klabu ya Piza alikuwa akimwaga chumvi kabla ya kila mechi ya mashindano kiwanjani kwao, dhidi ya watani wao wakubwa wa Cesena alimwaga kilo 26 nzima. Na kadhalika. Na kadhalika. Kwa nini iwe nongwa kufanyika hapa kwetu tu, tena madogo kuliko hayo? Acheni hizo!kwanini Yanga wanaamini ktk ushirikina? ndio maana timu haiendelei kamwe asilani
Siisemei Yanga, ila naomba kuweka sawa mambo 4. (1) Kuna tofauti baina ya ushirikina na kuamini uchawi. Ushirikina ni kuabudu asiyekuwa Mwenye enzi Mungu, uchawi ni kuamini ama kuogopa nguvu za giza au chochote kisichoeleweka. Timu zetu zinaangukia kwenye hili la pili. Ila haziko peke yao kwenye hilo, kwa hivyo ni ujinga, ushamba na upuuzi kuzibeza timu zetu tu huku tukitukuza wengine wafanyao zaidi ya hayo, kwa sababu tu si Watanzania wala Waafrika. (2) kitendo chochote kinachoipa timu ama mchezaji kujiamini kwenye mchezo wake ni msaada kwa mchezaji na timu hiyo. Muhimu tu kisipingane na ustaarabu, sheria, kanuni na taratibu zetu na za kimpira. (3) Kwa nini wastaarabu wanaolaani ushirikina wa Yanga wasijiulize zaidi mambo rahisi ya msingi: (a) kwa mechi ya Mapinduzi Cup dhidi ya Shaba, je ni kawaida golikipa kubaki na glovu za akiba chini ya goli, hasa ndani ya nyavu? Si vifaa vyote vya akiba vinabaki na wachezaji wa akiba kwenye dawati la ufundi? Marefa ilikuwaje wasilione hilo? (b) Kwa mechi ya Ndanda, ni kawaida golikipa kubaki na chupa ya maji akiwa golini? Na kama ni kwa matumizi yake, kwa nini ayasokomeke nyuma ya nyavu ambako hata kuyafikia ni taabu kwake? (4) Hivi kuondoa glovu ama maji hayo inakuwa ni jambo kubwa kuliko yafuatayo? (a) Michael Jordan alikuwa ni lazima avae kaptura yake ya Chuo Kikuu cha Carlifonia ndani ya bukta ya timu kwenye kila mechi ya Chicago Bulls, jambo lililomlazimisha kuvaa bukta kubwa zaidi kuliko kawaida. Hatimaye bukta hizo kubwa ukawa ndio mtindo wa NBA nzima. (b) kabla ya kila msimu wa Wimbledon, Bjorn Borg aliwacha kunyoa ndevu zake. Akaishia kutwaa taji hilo mfululizo 1976 - 1980. (c) Serena Williams amezoea kuenda na malapa yake ya msalani hadi kwenye uwanja anaochezea mashindano, ni lazima adunde mpira mara 5 kabla ya 'serve' yake ya kwanza na mara 2 kwa 'serve' ya pili. (d)Kolo Toure lazima awe wa mwisho kuingia uwanjani kwenye mechi yoyote. Mechi ya fainali ya Ulaya dhidi ya AC Roma aligoma kuingia mwanzoni mwa kipindi cha pili hadi Gallas aliyekuwa akitibiwa alipoingia. Toure akalimwa kadi ya njano alipoingia baada ya hapo. (e) John Terry kwenye kila mechi huegesha gari yake mahali hapohapo, anatumia vikinga ugoko hivyohivyo kwa miaka 10 mfululizo mpaka vilipopotea kwenye mechi ya ugenini dhidi ya Barcelona. (f) laurent Blanc alikuwa akibusu upara wa golikipa wake Barthez kabla ya kila mechi ya Kombe la Dunia 1998. (g) wakati mmoja Pele alimvulia jezi shabiki mmoja baada ya mechi. Mechi zilizofuata kiwango chake kikaonekana kupungua, mpaka alipomwomba rafiki yake kuifuatilia jezi hiyo. Baada ya hapo mambo yakajipa tena, ingawa kuna habari kwamba jezi aliyorejeshewa haikuwa ileile. (h) Kipa Sergio Goycochea wa Argentina alikuwa akikojoa kiwanjani kila ulipofikia wakati wa penalti tanotano. Akaitoa Yugoslavia kwenye robo fainali ya Kombe la Dunia 1990, akaitoa na Italia kwenye nusu fainali. Wakazitoa Columbia na Brazil kwenye kombe la Marekani Kusini 1993. (i) Rais wa klabu ya Piza alikuwa akimwaga chumvi kabla ya kila mechi ya mashindano kiwanjani kwao, dhidi ya watani wao wakubwa wa Cesena alimwaga kilo 26 nzima. Na kadhalika. Na kadhalika. Kwa nini iwe nongwa kufanyika hapa kwetu tu, tena madogo kuliko hayo? Acheni hizo!
Inawezekana, kwa mujibu wa vigezo vyako. Maana yake ni kwamba ili uweze kunitathmini hivyo, wewe ni zaidi ya mimi kwenye yote mawili mkuu.Bro una matatizo makubwa sana
Wewe ni mchawi na wewe ni mshirikina