Yanga nendeni kucheza kibayarn Munich tu kule tunisia

kwisha

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2021
Posts
1,779
Reaction score
4,982
Unajua Wale wa Tunisia kule kwao watacheza mpira wa kushambulia saana ili kutafuta matokeo
Sasa na Yanga wasicheze mpira wa kuzuia maana watakula mengi saana
Ila wakicheza mpira wa kushambulia na wale wa Tunisia watalazimika kucheza mpira ya kuzuia na kwa mashambulizi ya kushtukiza yaani wakiona yanga ana washambulia watajaa nyuma saana kuzuia ili wawe wana stukiza
 
Yanga wanaweza kutwaa hili kombe kama watakuwa serious

Wafanye uchunguzi kujua kombe limehifadhiwa wapi, wakishajua liko wapi waanze sasa maandalizi.

Wana Azizi Ki, huyu ni Mr ufunguo kwa maana ya kwamba zile sehemu zenye milango yenye kufuli nzito walipohifadhia kombe anaweza kutumika ku crack hiyo milango.

Baada ya hapo kuna yule beki wao ambaye ni mfupi, huyu atakuwa na kazi moja ya kunyata kuingia ndani punde tu baada ya Azizi Ki kufanikiwa kufungua milango.

Kwa ufupi wake alionao akinyata kimya kimya kuelekea mahala lilipo kombe hakuna mtu anaweza akamuona.

Huyu akishafanikisha kuchukua kombe atatakiwa kulipitisha kwa dirisha kwa kulirusha ambapo litadakwa moja kwa moja na Dgjui Diarra ambaye atakuwa yupo chini kisha taratibu ataanza kujongea mpaka getini.

Akiwa getini atapokelewa na Kisinda mzee wa mikimbio ambapo kupitia mbio zake hakuna atayeweza kuthubutu kumfukuza na hapo ndio itakuwa mwisho wa shughuli

Mshindwe nyinyi tu ila hili kombe kila nikiangalia naliona linaelekea Jangwani
 
Kwenye soka kila kitu kinawezekana, lakini mafanikio yoyote huja kwa kuwekewa mikakati na siyo porojo.

Akienda kama ambaye hana cha kupoteza maana tayari ameshapoteza, anaweza kupata matokeo mazuri.
 
We jamaaa una utani sana aseeeh 🙌
 
Na hizo key zikigoma kufungua wanae nondo..watatumia kuvunjia
 
Kwenye soka kila kitu kinawezekana, lakini mafanikio yoyote huja kwa kuwekewa mikakati na siyo porojo.

Akienda kama ambaye hana cha kupoteza maana tayari ameshapoteza, anaweza kupata matokeo mazuri.
Mzee wale jamaa haki yanga wakienda vibaya eti wajiamini wakashambulie tu hawana cha kupoteza watachakazwa kipigo cha Kipanga kwa kuwa Yanga hawana beki.Usiwadangaye waambie watafute sare ya aina yoyote ile. Na waarabu wanataka kuwatoboa dk za mwanzo tu kuwachanganya.
Yanga tafuteni la mapema

Sent from my LM-Q730 using JamiiForums mobile app
 
🚮
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…