Yanga sc 3-1 Ruvu shooting | ligi kuu | Benjamin Mkapa

Kama ilivyo ada kuna mengi yakushangaza, endelea kutufuatilia
 
mkuu una pointi nzuri ila imepoteza maana kwani hukuyasema haya kwenye mechi za Simba vs Biashara, Dodoma jiji, Polisi Tanzania na Coastal Union ambapo wote kwa macho yetu tuliona michongo lakini ulikaa kimya.
 
Mukokoooooo! Dk ya 75 Yanga 3 Ruvu Shooting 1!
 
Sasa si wangechukua point tu ,kuna haja gani ya kucheza wakati wameshamalizana
 
Unabonga sana aise
 
Mukokoooooo! Dk ya 75 Yanga 3 Ruvu Shooting 1!
Mukokoooo dakika ya 75 anaiandikia yanga goal la tatu wakati ruvu shooting akiwa na goal 1 na hiyo inatufundisha kua ni vema kufika bei na refa kuliko kufanya jeuri

Naa naam tuendelee kuinjoi, mpira ni mzuri na refa anaendelea kubaki katika kiwango chake kile kile
 
Huyu refa vipi mbona yuko nje ya makubaliano, tulimwambia dakika ya 80 tuwe na penalty mbili sasa hivi ni dakika ya 86 na hajafanya chochote
 
Kauli ya Manara ifanyiwe kazi ..kwanini Yanga & Simba hawawezi shinda bila kubebwa kwa Penati na kadi nyekundu kwa timu pinzani?....
 
Huu msimu mtapata tabu sana! Maana Yanga sijui ina hela kiasi gani!! Waamuzi tuwahonge sisi, wachezaji tuwahinge sisi, timu kama timu mfano Biashara United tuihonge sisi!

Na sasa tunajipanga kumhonga Moo! Ili tuwapige goli za kutosha mechi zijazo.
 
Kauli ya Manara ifanyiwe kazi ..kwanini Yanga & Simba hawawezi shinda bila kubebwa kwa Penati na kadi nyekundu kwa timu pinzani?....

Nilikuwa naangalia mechi baina ya Yanga na Ruvu na mpira ulikuwa umebalance huku Ruvu wakimiliki mchezo vyema hadi pale refaree kwa mapenzi binafsi alipoamua kuharibu mpira kwa kuwazawadia Yanga penati ya bure bila kufuata kanuni 17 za mpira wa miguu achilia mbali kumtoa nje mchezaji wa Ruvu kipindi cha kwanza kwa Red card ambayo haikuwa na ulazima...Nipo bar napiga kinywaji nikitafakari kauli ya Waziri mkuu jana alipokutana na viongozi wa vilabu hapa nchini akijaribu kuhamasisha jinsi ya kuisadia timu ya Taifa kufanya vizuri kwenye mashindano ya kutafuta nafasi ya kushiriki Kombe la dunia wakati nawaza ilo nikakumbuka kuwa na yeye jana mara baada ya kikao na vilabu aliishia kupiga picha na viongozi wa Yaga naSimba peke yao ...Mungu wangu aliyeturoga watanzania alikuwa ni mchawi hatareeeee.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…